Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 13:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Ombolezeni kwa sauti, kwa maana siku ya Yehova iko karibu!

      Itakuja kama maangamizi kutoka kwa Mweza-Yote.+

  • Yeremia 25:33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 “‘Na wale ambao Yehova atawaua siku hiyo watatapakaa kutoka mwisho mmoja wa dunia mpaka mwisho wa pili wa dunia. Hawataombolezewa, wala kukusanywa wala kuzikwa. Watakuwa kama mbolea juu ya ardhi.’

  • Ezekieli 30:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Kwa maana siku hiyo iko karibu, naam, siku ya Yehova iko karibu.+

      Itakuwa siku ya mawingu,+ wakati uliowekwa wa mataifa.+

  • Yoeli 1:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Ole kwa sababu ya ile siku!

      Kwa maana siku ya Yehova iko karibu,+

      Nayo itakuja kama maangamizi kutoka kwa Mweza-Yote!

  • Yoeli 2:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 “Pigeni pembe Sayuni!+

      Pigeni kelele za vita katika mlima wangu mtakatifu.

      Wakaaji wote wa nchi* na watetemeke,

      Kwa maana siku ya Yehova inakuja!+ Iko karibu!

  • Yoeli 2:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Yehova atapaza sauti mbele ya jeshi lake,+ kwa maana jeshi lake ni kubwa sana.+

      Kwa maana anayetekeleza neno Lake ni mwenye nguvu;

      Kwa maana siku ya Yehova ni kuu na inaogopesha sana.+

      Ni nani anayeweza kuistahimili?”+

  • Sefania 1:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Siku hiyo ni siku ya ghadhabu,+

      Siku ya taabu na maumivu makali,+

      Siku ya dhoruba na ukiwa,

      Siku ya giza na utusitusi,+

      Siku ya mawingu na utusitusi mzito,+

  • 2 Petro 3:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Kwa kuwa vitu hivyo vyote vitayeyushwa kwa njia hiyo, fikirieni mnapaswa kuwa watu wa aina gani katika matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ujitoaji-kimungu,* 12 huku mkisubiri na kuweka karibu akilini* kuwapo kwa siku ya Yehova,*+ siku ambayo mbingu zitateketezwa+ kwa moto na vitu vya msingi vitayeyuka kwa joto kali!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki