10 Ndipo Yesu akamwambia: “Nenda zako, Shetani! Kwa maana imeandikwa: ‘Yehova* Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu,+ na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.’”+
25 Petro alipokuwa akiingia, Kornelio akamlaki, akapiga magoti miguuni pake, na kumsujudia.*26 Lakini Petro akamwinua, akisema: “Simama; mimi pia ni mwanadamu tu.”+
10 Ndipo nikaanguka chini mbele ya miguu yake ili kumwabudu. Lakini ananiambia: “Uwe mwangalifu! Usifanye hivyo!+ Mimi ni mtumwa mwenzako tu na wa ndugu zako walio na kazi ya kutoa ushahidi kumhusu Yesu.+ Mwabudu Mungu!+ Kwa maana kutoa ushahidi kumhusu Yesu ndilo kusudi la unabii.”+