-
Matendo 14:12-15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Wakaanza kumwita Barnaba Zeu, naye Paulo wakamwita Herme, kwa kuwa ndiye aliyeongoza katika mazungumzo. 13 Naye kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa kwenye mwingilio wa jiji, akawaleta ng’ombe dume na mashada ya maua kwenye malango, naye alitaka kutoa dhabihu pamoja na umati.
14 Hata hivyo, mitume Barnaba na Paulo waliposikia jambo hilo, wakayararua mavazi yao na kuruka ndani ya umati wakisema kwa sauti kubwa: 15 “Wanaume, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi pia ni wanadamu tulio na udhaifu kama wenu.+ Nasi tunawatangazia habari njema, ili mgeuke kutoka katika mambo haya ya bure mje kwa Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na dunia na bahari na vitu vyote vilivyomo.+
-
-
Ufunuo 22:8, 9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Basi mimi, Yohana, ndiye niliyekuwa nikisikia na kuona mambo haya. Niliposikia na kuyaona, nikaanguka chini kuabudu miguuni pa yule malaika aliyekuwa akinionyesha mambo haya. 9 Lakini yeye akaniambia: “Uwe mwangalifu! Usifanye hivyo! Mimi ni mtumwa mwenzako tu na wa ndugu zako manabii na wa wale wanaoshika maneno ya kitabu hiki cha kukunjwa. Mwabudu Mungu.”+
-