Zaburi
Kwa kiongozi; umepatanishwa na sauti ya Sheminithi.* Muziki wa Daudi.
12 Niokoe, Ee Yehova, kwa maana mtu mshikamanifu hayupo tena;
Watu waaminifu wametoweka kutoka miongoni mwa wanadamu.
3 Yehova ataikata kabisa midomo yote inayosifusifu
Na ulimi unaojigamba kupindukia,+
4 Wale wanaosema: “Tutashinda kwa ndimi zetu.
Tunatumia midomo yetu tupendavyo;
Ni nani atakayekuwa bwana mkubwa wetu?”+
5 “Kwa sababu wale wanaoteswa wanakandamizwa,
Kwa sababu ya kilio cha uchungu cha maskini,+
Nitainuka na kutenda,” asema Yehova.
“Nitawaokoa kutoka kwa wale wanaowatendea kwa dharau.”*
Ni kama fedha iliyosafishwa katika tanuru la udongo,* iliyosafishwa mara saba.