Zaburi
Kwa kiongozi katika sauti ya nane ya chini.+ Muziki wa Daudi.
12 Uniokoe,+ Ee Yehova, kwa maana mshikamanifu amefikia mwisho;+
Kwa maana watu waaminifu wametoweka kutoka katikati ya wana wa binadamu.
2 Wao huendelea kusemezana mambo yasiyo ya kweli;+
Kwa midomo laini+ wao huendelea kusema wakiwa na mioyo miwili.+
4 Wale ambao wamesema: “Kwa ulimi wetu tutashinda.+
Midomo yetu iko pamoja nasi. Ni nani atakayekuwa bwana kwetu?”
5 “Kwa sababu ya kuporwa kwao wenye kuteseka, kwa sababu ya kuugua kwao maskini,+
Nitasimama wakati huu,” asema Yehova.+
“Nitamweka katika usalama mbali na mtu yeyote anayemdhihaki.”+
6 Maneno ya Yehova ni maneno safi,+
Kama fedha iliyosafishwa katika tanuru ya kuyeyushia kwenye udongo, iliyosafishwa mara saba.