Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
2 Nitaweka upinzani katika nafsi yangu mpaka wakati gani,
Huzuni katika moyo wangu wakati wa mchana?
Adui yangu atainuliwa juu yangu mpaka wakati gani?+
3 Unitazame; unijibu, Ee Yehova Mungu wangu.
Uyafanye macho yangu yang’ae,+ ili nisilale usingizi katika kifo.+
4 Ili adui yangu asiseme: “Nimemshinda!”
Ili wapinzani wangu wasishangilie kwa sababu nimefanywa niyumbe-yumbe.+
6 Nitamwimbia Yehova, kwa maana amenitendea kwa njia ya kunipa thawabu.+