Zaburi
Kwa kiongozi. Ya Daudi.
14 Asiye na akili amesema katika moyo wake:
“Hakuna Yehova.”+
Wametenda kwa uharibifu,+ wametenda kwa njia yenye kuchukiza katika shughuli zao.
Hakuna yeyote anayefanya mema.+
2 Kutoka mbinguni Yehova amewatazama wana wa binadamu walio chini,+
Ili aone kama kuna yeyote ambaye ana ufahamu, yeyote anayemtafuta Yehova.+
3 Wote wamegeuka kando,+ wote ni wafisadi kwa njia ileile;+
Hakuna yeyote anayefanya mema,+
Hakuna hata mmoja.+
4 Je, hakuna yeyote kati ya wale wanaotenda mambo yenye kuumiza ambaye ana ujuzi,+
Wakila watu wangu kama vile ambavyo wamekula mkate?+
Hata hawajamwitia Yehova.+