Zaburi
Kwa kiongozi. Ya Daudi.
Mnawezaje kuthubutu kuiambia nafsi yangu:
“Kimbieni kwenye mlima wenu kama ndege!+
2 Kwa maana, tazama! waovu huupinda upinde,+
Huutayarisha mshale wao juu ya kamba ya upinde,
Ili katika giza wawafyatulie walio wanyoofu moyoni.+
4 Yehova yumo katika hekalu lake takatifu.+
Yehova—kiti chake cha ufalme kiko mbinguni.+
Macho yake yanaangalia, macho yake yanayong’aa yanawachunguza+ wana wa binadamu.
5 Yehova humchunguza mwadilifu na pia mwovu,+
Na mtu yeyote anayependa jeuri nafsi Yake hakika inamchukia.+