Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wakorintho 12
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

1 Wakorintho—Yaliyomo

      • Zawadi za roho (1-11)

      • Mwili mmoja, viungo vingi (12-31)

1 Wakorintho 12:1

Marejeo

  • +1Ko 14:1

1 Wakorintho 12:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, watu wasio waamini.

Marejeo

  • +Zb 115:5; Hab 2:18; 1Ko 8:4; Gal 4:8; 1Th 1:9

1 Wakorintho 12:3

Marejeo

  • +1Yo 4:2, 3

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    7/15/2007, uku. 21

  • Fahirishi ya Machapisho

    w07 7/15 21

1 Wakorintho 12:4

Marejeo

  • +Efe 4:4

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Utatu, uku. 23

1 Wakorintho 12:5

Marejeo

  • +Efe 4:11

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Utatu, uku. 23

1 Wakorintho 12:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kazi.”

Marejeo

  • +1Pe 4:11

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    12/15/2011, kur. 24-25

    Utatu, uku. 23

  • Fahirishi ya Machapisho

    w11 12/15 24-25

1 Wakorintho 12:7

Marejeo

  • +1Ko 14:26

1 Wakorintho 12:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ujumbe wa.”

1 Wakorintho 12:9

Marejeo

  • +1Ko 13:2
  • +Mdo 3:5-8; 28:8, 9

1 Wakorintho 12:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ndimi.”

Marejeo

  • +Ebr 2:3, 4
  • +1Yo 4:1
  • +Mdo 10:45, 46; 1Ko 14:18
  • +1Ko 14:26

1 Wakorintho 12:12

Marejeo

  • +Ro 12:4, 5

1 Wakorintho 12:13

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Maswali ya Biblia Yajibiwa, makala 110

    Ufahamu,

    Ufahamu,

1 Wakorintho 12:14

Marejeo

  • +Efe 4:16

1 Wakorintho 12:15

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi (Funzo),

    8/2020, kur. 23-24

1 Wakorintho 12:16

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi (Funzo),

    8/2020, kur. 23-24

1 Wakorintho 12:18

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Ufahamu,

1 Wakorintho 12:21

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    7/15/1996, uku. 20

  • Fahirishi ya Machapisho

    w96 7/15 20

1 Wakorintho 12:22

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    6/15/2014, uku. 24

    10/15/1997, kur. 14-15

  • Fahirishi ya Machapisho

    w97 10/15 14-15

1 Wakorintho 12:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kiasi.”

Marejeo

  • +Mwa 3:7, 21

1 Wakorintho 12:24

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    2/15/1999, uku. 20

  • Fahirishi ya Machapisho

    w99 2/15 20

1 Wakorintho 12:25

Marejeo

  • +Ro 12:10; Gal 6:2; Efe 4:25

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Furahia Maisha Milele!, somo la 19

    Mnara wa Mlinzi,

    6/15/2007, uku. 20

    5/15/2004, uku. 19

    10/15/1986, uku. 14

  • Fahirishi ya Machapisho

    w07 6/15 20; w04 5/15 19

1 Wakorintho 12:26

Marejeo

  • +Ebr 13:3
  • +Ro 12:15

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Furahia Maisha Milele!, somo la 19

1 Wakorintho 12:27

Marejeo

  • +Efe 1:22, 23
  • +Ro 12:4, 5

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    7/1/1995, uku. 11

1 Wakorintho 12:28

Marejeo

  • +Efe 2:20
  • +Mdo 13:1
  • +Efe 4:11
  • +Gal 3:5
  • +Mdo 5:16
  • +Ebr 13:17
  • +Mdo 2:6, 7

1 Wakorintho 12:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “watafsiri.”

Marejeo

  • +1Ko 14:4
  • +1Ko 14:5

1 Wakorintho 12:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kujitahidi kupata.”

Marejeo

  • +1Ko 14:1
  • +1Ko 13:8

Fahirisi Mbalimbali

  • Mwongozo wa Utafiti

    Mnara wa Mlinzi,

    12/15/2009, kur. 26-27

    2/15/1999, kur. 22-23

  • Fahirishi ya Machapisho

    w09 12/15 26-27; w99 2/15 22-23

Tafsiri Mbalimbali

Bofya nambari ya mstari ili kuona mstari huo katika tafsiri mbalimbali za Biblia.

Jumla

1 Kor. 12:11Ko 14:1
1 Kor. 12:2Zb 115:5; Hab 2:18; 1Ko 8:4; Gal 4:8; 1Th 1:9
1 Kor. 12:31Yo 4:2, 3
1 Kor. 12:4Efe 4:4
1 Kor. 12:5Efe 4:11
1 Kor. 12:61Pe 4:11
1 Kor. 12:71Ko 14:26
1 Kor. 12:91Ko 13:2
1 Kor. 12:9Mdo 3:5-8; 28:8, 9
1 Kor. 12:10Ebr 2:3, 4
1 Kor. 12:101Yo 4:1
1 Kor. 12:10Mdo 10:45, 46; 1Ko 14:18
1 Kor. 12:101Ko 14:26
1 Kor. 12:12Ro 12:4, 5
1 Kor. 12:14Efe 4:16
1 Kor. 12:23Mwa 3:7, 21
1 Kor. 12:25Ro 12:10; Gal 6:2; Efe 4:25
1 Kor. 12:26Ebr 13:3
1 Kor. 12:26Ro 12:15
1 Kor. 12:27Efe 1:22, 23
1 Kor. 12:27Ro 12:4, 5
1 Kor. 12:28Efe 2:20
1 Kor. 12:28Mdo 13:1
1 Kor. 12:28Efe 4:11
1 Kor. 12:28Gal 3:5
1 Kor. 12:28Mdo 5:16
1 Kor. 12:28Ebr 13:17
1 Kor. 12:28Mdo 2:6, 7
1 Kor. 12:301Ko 14:4
1 Kor. 12:301Ko 14:5
1 Kor. 12:311Ko 14:1
1 Kor. 12:311Ko 13:8
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Soma katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
1 Wakorintho 12:1-31

Barua ya Kwanza kwa Wakoritho

12 Basi kuhusu zawadi za kiroho,+ akina ndugu, sitaki mkose kujua. 2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wa mataifa,* mlikuwa mkishawishiwa na kuziabudu sanamu zisizo na sauti,+ mkizifuata popote zilipowaongoza. 3 Sasa ningetaka mjue kwamba hakuna mtu yeyote ambaye anaposema kwa roho ya Mungu, husema: “Yesu amelaaniwa!” na hakuna mtu anayeweza kusema: “Yesu ni Bwana!” isipokuwa kwa roho takatifu.+

4 Basi kuna zawadi mbalimbali, lakini kuna roho ileile;+ 5 na kuna huduma mbalimbali,+ na bado kuna Bwana yuleyule; 6 na kuna utendaji* mbalimbali, na bado ni Mungu yuleyule anayefanya utendaji huo wote katika kila mtu.+ 7 Lakini roho hufunuliwa katika kila mmoja kwa kusudi lenye faida.+ 8 Kwa maana mtu mmoja hupewa maneno ya* hekima kupitia roho, mwingine maneno ya ujuzi kulingana na roho ileile, 9 mwingine imani+ kwa roho ileile, mwingine zawadi za uponyaji+ kwa roho hiyo moja, 10 naye mwingine hupewa utendaji wa matendo yenye nguvu,+ mwingine kutoa unabii, mwingine utambuzi wa maneno yaliyoongozwa na roho,+ mwingine lugha* mbalimbali,+ na mwingine fasiri ya lugha.+ 11 Lakini ni roho ileile inayofanya utendaji huu wote, ikimgawia kila mmoja kama vile inavyopenda.

12 Kwa maana kama vile mwili ni mmoja lakini una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili huo, ingawa ni vingi, ni mwili mmoja,+ ndivyo pia alivyo Kristo. 13 Kwa maana kwa roho moja sote tulibatizwa katika mwili mmoja, iwe ni Wayahudi au ni Wagiriki, iwe ni watumwa au ni walio huru, nasi sote tulinyweshwa roho moja.

14 Kwa maana kwa kweli, mwili una viungo vingi, si kiungo kimoja.+ 15 Ikiwa mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono, mimi si sehemu ya mwili,” hilo halifanyi usiwe sehemu ya mwili. 16 Na ikiwa sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, mimi si sehemu ya mwili,” hilo halilifanyi lisiwe sehemu ya mwili. 17 Ikiwa mwili wote ungekuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Ikiwa wote ungekuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi? 18 Lakini sasa Mungu amepanga kila kiungo cha mwili kama alivyopenda.

19 Ikiwa vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? 20 Lakini sasa viungo ni vingi, lakini mwili mmoja. 21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sikuhitaji wewe,” au tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Siwahitaji ninyi.” 22 Badala yake viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu zaidi ni muhimu sana, 23 na sehemu za mwili ambazo tunafikiri hazistahili kuheshimiwa sana, tunazipa heshima zaidi,+ basi sehemu zetu ambazo hazivutii tunazitendea kwa heshima* zaidi, 24 bali sehemu zetu zinazopendeza hazihitaji kitu chochote. Lakini hivyo ndivyo Mungu alivyouunganisha mwili, akiipa heshima zaidi sehemu iliyokuwa na upungufu, 25 ili kusiwe na mgawanyiko katika mwili, bali viungo vyake vitunzane.+ 26 Kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote huumia pamoja nacho;+ au kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vingine vyote hushangilia pamoja nacho.+

27 Basi ninyi ni mwili wa Kristo,+ na kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili huo.+ 28 Naye Mungu amewaweka watu mbalimbali katika kutaniko: kwanza, mitume;+ pili, manabii;+ tatu, walimu;+ kisha matendo yenye nguvu;+ kisha zawadi za uponyaji;+ huduma za kusaidia; uwezo wa kuelekeza;+ na lugha mbalimbali.+ 29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote hufanya matendo yenye nguvu? 30 Je, wote wana zawadi za uponyaji? Je, wote husema kwa lugha?+ Je, wote ni wakalimani?*+ 31 Lakini endeleeni kutafuta kwa bidii* zawadi zilizo kubwa zaidi.+ Na bado nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki