Isaya
Kwa sababu limeharibiwa kwa usiku mmoja,
Jiji la Ari+ la Moabu limenyamazishwa.
Kwa sababu limeharibiwa kwa usiku mmoja,
Jiji la Kiri+ la Moabu limenyamazishwa.
Moabu inaombolezea Nebo+ na Medeba.+
Kila kichwa kimenyolewa upara,+ ndevu zote zimenyolewa.+
3 Wamevaa nguo za magunia katika barabara zake.
Kwenye paa zao na katika viwanja vyao vya jiji, wote wanaomboleza kwa sauti;
Wanashuka chini wakilia.+
Ndiyo sababu watu wenye silaha wa Moabu wanaendelea kupaza sauti.
Anatetemeka.*
5 Moyo wangu unamlilia Moabu.
Wakimbizi wake wamekimbia mpaka Soari+ na Eglath-shelishiya.+
Kwenye njia inayopanda kwenda Luhithi wanalia wakipanda;
Kwenye njia ya kwenda Horonaimu wanalia kwa sauti kwa sababu ya msiba.+
6 Kwa maana maji ya Nimrimu yamekuwa ukiwa;
Majani mabichi yamekauka,
Majani yamekwisha na hakuna chochote kibichi kilichobaki.
8 Kwa maana kilio kinasikika katika eneo lote la Moabu.+
Maombolezo yanafika Eglaimu;
Maombolezo yanafika Beer-elimu.
9 Kwa maana maji ya Dimoni yamejaa damu,
Nami nina mengi zaidi kwa ajili ya Dimoni:
Simba kwa ajili ya watu wa Moabu wanaoponyoka
Na kwa ajili ya wale wanaobaki nchini.+