Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g94 6/8 kur. 20-21
  • Je! Biblia Hukataza Uhuru wa Mawazo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Biblia Hukataza Uhuru wa Mawazo?
  • Amkeni!—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Mpende Yehova kwa Akili Zako Zote’
  • Njia ya Kujikinga
  • ‘Vitu Vyote Vimefunuliwa’
  • Uhuru wa Kweli wa Mawazo
  • Watu Huru Lakini Wanaotakwa Watoe Hesabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Uhuru Unaofurahiwa na Waabudu wa Yehova
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Mtumikie Yehova, Mungu wa Uhuru
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Usikose Kusudi la Uhuru wa Kupewa na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1994
g94 6/8 kur. 20-21

Maoni ya Biblia

Je! Biblia Hukataza Uhuru wa Mawazo?

MIALE ya moto yapepea kuelekea mbingu moto mkubwa umezapo vitabu vyenye thamani vinavyorushwa kwao na maofisa Wajerumani. Mandhari hiyo ilikuwa ya Nazi ya Ujerumani? Ndiyo, lakini pia ingeweza kuwa mandhari ya mwaka 1199, wakati kasisi-mkuu wa Katoliki ya Roma alipoagiza Biblia zote za lugha ya Kijerumani zichomwe.[1]

Kwa kweli, visa vya kuchoma vitabu—ishara ya ulimwengu mzima ya kukandamiza uhuru wa wazo na usemi—umetokea katika nchi nyingi na kwa karne nyingi.[2] Mara nyingi, kumechochewa na viongozi wengi wa kidini ambao waliogopa athari ambayo uhuru wa mawazo ungeleta kwa watu wa kawaida.[3]

Si ajabu kwamba watu wengi leo hufikiria Biblia imetoa amri ya vizuizi hususa inayokataza utafutaji wa kiakili. Lakini je, ni kweli hivyo? Je! Biblia hukataza uhuru wa mawazo?

‘Mpende Yehova kwa Akili Zako Zote’

Biblia haikatazi kutumia akili. Kwa kweli, Yesu alitia moyo kila mmoja wetu ‘ampende Yehova kwa akili zetu zote.’ (Marko 12:30, NW) Huduma yake yaonyesha kwamba alipendezwa sana na matukio ya karibuni (Luka 13:1-5), biolojia (Mathayo 6:26, 28; Marko 7:18, 19), ukulima (Mathayo 13:31, 32), na asili ya kibinadamu (Mathayo 5:28; 6:22-24). Vielelezo vyake vyaonyesha kwamba alielewa waziwazi kanuni zilizomo kwenye Neno la Mungu na malezi na kufikiri kwa wasikilizaji wake na kwamba aliwaza kwa uangalifu jinsi ya kuunganisha mambo hayo mawili pamoja.

Paulo alisihi Wakristo wote wampe Mungu utumishi wao kwa “nguvu zao za kufikiri.” (Warumi 12:1, NW) Aliwatia moyo Wathesalonike wasiache ‘semi zilizopuliziwa ziwatikise kutoka kwenye sababu yao.’ (2 Wathesalonike 2:2, NW) Yeye alikuwa na ujuzi fulani wa mashairi ya Kigiriki na Krete (Matendo 17:28; Tito 1:12) na silaha za kivita na hatua zazo (Waefeso 6:14-17; 2 Wakorintho 2:14-16). Naye alikuwa mchunguzi wa desturi za mahali.—Matendo 17:22, 23.

Ijapokuwa Yesu na Paulo walifurahia uhuru wa mawazo, wao hawakujiona wenyewe kuwa wenye mamlaka pekee ya kuamua yaliyo sawa na yaliyo mabaya. Badala ya kukataa Biblia akipendelea maoni yake mwenyewe, Yesu alinukuu Maandiko mara kwa mara. Jibu lake la mara moja na kali wakati Petro alipomsihi afikirie mwendo tofauti kutoka kifo cha kujidhabihu ambacho kilikuwa mapenzi ya Mungu kwake laonyesha kwamba hangethubutu kutafakari kufikiri kwa aina hiyo. (Mathayo 16:22, 23) Vivyo hivyo, Paulo aliwaambia Wakorintho: “Nilipokuja kwenu, sikuja kwa wonyesho wa ufasaha wa kusema au wa hekima ya binadamu, lakini kuwaambia tu yale ambayo Mungu ametoa uhakikisho.” (1 Wakorintho 2:1, The Jerusalem Bible) Kama vile Yesu, kusababu kwake kulitegemea sana Maandiko.—Matendo 17:2.

Biblia hutia moyo utumizi kamili wa akili ya mtu lakini si kwa kujizuia kabisa. Hata hivyo, mzigo wa daraka la kuweka kufikiri kwetu kupatane na kule kwa Yehova kunategemea Mkristo mmoja-mmoja, si kutaniko. Hivyo, wakati idadi fulani ya Waefeso ilipokataa zoea la uwasiliani-roho peupe na wakawa Wakristo, Paulo hakuchukua daraka hilo la kuchoma vitabu vyao, bali “wengi wao ambao walikuwa wamezoea mizungu walikusanya vitabu vyao na kuviteketeza motoni hadharani.” (Matendo 19:19, JB) Kwa nini Wakristo hawa waliona kuwa jambo la lazima kuchoma vitabu vyao?

Njia ya Kujikinga

Hebu fikiria kielelezo hiki. Kinga yenye mafanikio ya kijeshi hutia ndani njia kadhaa za kujikinga. Hakuna jenerali mwenye mafanikio anayeweza kuhisi kwamba yoyote kati ya hizo si ya maana na yapaswa kuachwa bila kupigana. Katika vita ya Mkristo dhidi ya dhambi, kuna njia kadhaa za kujikinga pia.

Yakobo 1:14, 15 husema kwamba “kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi.” Hatua ya kwanza kuelekea dhambi ni kusitawishwa kwa tamaa mbaya akilini. Hivyo, njia ya kujikinga ni kuepuka kusitawisha tamaa hiyo—kudhibiti kufikiri kwa mtu.

Ni kwa sababu ya ufungamanisho huu kati ya mawazo na matendo ndio Biblia hutuonya hivi: “Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.” (Wakolosai 3:2) Wakristo wakataapo kukazia akili ukosefu wa adili, uwasiliani-roho, au uasi-imani, wanafanya uamuzi huu, si kwa sababu ya kuogopa kwamba mawazo hayo yaweza kuthibitika kuwa makuu kuliko kweli za Biblia, bali kwa sababu wanataka kuepuka chochote ambacho kingeweza kuwavuta kwenye mwendo wa dhambi.

‘Vitu Vyote Vimefunuliwa’

Sababu nyingine muhimu ya kudhibiti kufikiri kwetu ni upendo wetu kwa Yehova na heshima kwa uwezo wake wa kujua mawazo yetu. Hebu wazia kama ungekuwa na rafiki au mtu wa ukoo umpendaye ambaye anaathiriwa upesi na uchafu au vumbi. Je! utakosa kumwalika rafiki yako nyumbani mwako, ukikataa kufanya usafi wa ziada ambao nyumba yako yahitaji? Je! upendo haungekuchochea ufanye jitihada za ziada za kuweka vitu viwe safi? Athirio la upesi la Yehova kwa mawazo yetu ya ndani laonyeshwa kwenye Zaburi 44:21: “Ndiye azijuaye siri za moyo.” Paulo alisema kwamba twatozwa hesabu kwa mawazo hayo: “Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu.”—Waebrania 4:13; Zaburi 10:4; Mithali 6:16, 18.

Ayubu alitambua daraka la mwanadamu kwa Mungu kwa ajili ya mawazo yake. ‘Ayubu . . . akasongeza sadaka za kuteketezwa . . . ; kwani, Ayubu alisema, Humkini kwamba hawa wanaangu wamefanya dhambi, na kumkufuru Mungu mioyoni mwao.’ (Ayubu 1:5)[4] Kuwazia kimakusudi juu ya mwendo mbaya kwaweza kuonwa na Yehova kuwa dhambi.[5]—Linganisha Kutoka 20:17.

Uhuru wa Kweli wa Mawazo

Biblia hutia moyo kila Mkristo aweke mradi ‘kuteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo.’ (2 Wakorintho 10:5) Hilo lafikiwa, si kupitia vizuizi vilivyowekwa na viongozi wa kidini, bali kupitia kujidhibiti kwa mtu mmoja-mmoja na kupitia upendo wake kwa Yehova na uelewevu wa kanuni Zake. Pamoja na kufikia mradi huu huja uhuru wa kweli wa mawazo, ukiwekewa mpaka tu na viwango vya kimungu na ukizidishwa na shangwe ya kujua kwamba, hata katika mawazo yetu, twampendeza Yehova.[6]

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 20]

Kutoka kitabu Bildersaal deutscher Geschichte

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki