Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 1/8 kur. 26-27
  • Ni Nani Huenda Mbinguni?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Huenda Mbinguni?
  • Amkeni!—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wale Wasio Mbinguni
  • Yesu Alifungua Njia
  • Ufalme wa Kimbingu
  • Kikundi cha Watawala Wachaguliwa
  • Ni Nani Wanaoenda Mbinguni, na kwa Sababu Gani?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Serikali ltakayoleta Amani Duniani Pote
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Sababu Kwanini “Kundi Dogo” Huenda Mbinguni
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Je, Watu Wote Wazuri Wanaenda Mbinguni?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 1/8 kur. 26-27

Maoni ya Biblia

Ni Nani Huenda Mbinguni?

BOMU la maharamia lararua vipande ndege ikiwa mwendoni, na kuua wote waliomo. Jamaa na rafiki za majeruhi wanaambiwa kwamba wapendwa wao wako mbinguni, kama kwamba ni kulipia kifo chao cha jeuri na kisichotazamiwa.

Mwanamuziki apendwaye na wengi afa na asemekana kuwa ‘anapiga tarumbeta pamoja na malaika mbinguni.’

Ugonjwa, njaa, au aksidenti yanyang’anya vitoto vichanga uhai, na makasisi wasema kuwa vinafurahia raha ya kimbingu, huenda hata vikiwa malaika!

Je! Mungu anasahihisha ukosefu wa haki kwa wachanga na watu wazima kwa kuwachukua wote hao kwake katika amani ya kimbingu? Je, ruhusa ya kuingia mbinguni ni njia ya Mungu tu ya kuhifadhi yote yaliyo mema na yenye kusifika katika jamii ya kibinadamu? Ni nini yaliyo maoni ya Biblia?

Wale Wasio Mbinguni

Taarifa ya Biblia iko wazi: “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu?” (1 Wakorintho 6:9) Hata hivyo, Biblia pia husema kuhusu waadilifu wengi na majeruhi wa ukosefu wa haki ambao hawatazirithi mbingu.

Yesu mwenyewe alisema hivi kuhusiana na Yohana Mbatizaji aliyekaribia kuuawa kwa sababu ya imani: “Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.” (Mathayo 11:11) Wavulana wote wenye miaka miwili na chini katika Bethlehemu na wilaya zake walichinjwa kikatili na Mfalme mwovu Herode katika jaribio lake la kumharibu mtoto Yesu. (Mathayo 2:16) Tena, Yesu alisema: “Wala hakuna mtu [mwanamume au mwanamke au mtoto] aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu [Yesu].” (Yohana 3:13) Kwa sababu gani Yesu hakusema kuhusu hawa majeruhi wa ukosefu wa haki kuwa mbinguni?

Yesu Alifungua Njia

Yesu alijiita “njia, na kweli, na uzima” na alitajwa na Paulo kuwa “matunda ya kwanza kati ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo.” (Yohana 14:6; 1 Wakorintho 15:20, NW) Kwa sababu hiyo, hakuna yeyote ambaye angaliweza kumtangulia kuingia mbinguni. Lakini Yesu alipopaa mbinguni yapata siku 40 baada ya ufufuo wake, je, baadaye alifuatwa na wanaume wastahiki wenye imani waliokufa tayari? Siku kumi baadaye, mtume Petro alisema kuhusiana na Mfalme Daudi kwamba “alikufa na pia akazikwa na kaburi lake limo miongoni mwetu hadi siku hii. . . . Hakika Daudi hakupaa hadi mbinguni.”—Matendo 2:29, 34, NW.

Hivyo basi, ruhusa ya kuingia mbinguni inahusisha zaidi ya malipo tu ya kuteseka kutokana na ukosefu wa haki au hata kuthawabishwa kwa uaminifu wa kibinafsi. Badala yake, inaandaa kuundwa kwa kikundi cha watawala wenye makao mbinguni kilichofanyizwa kwa idadi ya wanadamu wawakilishi chini ya mwongozo wa Kristo, waliotiwa mafuta kwa roho takatifu.—Warumi 8:15-17; Ufunuo 14:1-3.

Ufalme wa Kimbingu

Yesu aliutaja utawala huu, au serikali, kuwa “ufalme wa mbinguni” au “ufalme wa Mungu.” (Mathayo 5:3, 20; Luka 7:28) Haikukusudiwa kwamba sehemu kubwa ya wanadamu iingizwe ndani ya kikundi hiki cha kutawala. Hivyo, Yesu alikitaja kuwa “kundi dogo.” (Luka 12:32) Katika lugha ya awali iliyotumiwa kwenye sehemu hii ya Biblia, neno “dogo” (mi·krosʹ) ni kinyume cha kubwa (meʹgas), na utumizi walo katika Luka 12:32 hurejezea wingi au uchache katika idadi. Kwa hiyo, ushirika katika “ufalme wa mbinguni” hauruhusu kuwako kwa idadi isiyo na kikomo. Kwa kutoa kielezi: Ikiwa ungeulizwa kumwaga maji machache katika gilasi (bilauri), ungehakikisha kwamba haikufurika. Hivyo, pia lile “kundi dogo” haliwezi kufanyizwa kwa idadi za watu zenye kufurika. Ufalme wa Mungu una idadi iliyowekwa (‘ndogo’) ya watawala-wenzi pamoja na Kristo.

Nambari kamili ya watawala hawa, 144,000, ilifunuliwa kwa mtume Yohana. (Ufunuo 14:1, 4) Mapema katika Ufunuo hawahawa husemekana ‘kutoka kila kabila na lugha na kikundi cha wanadamu na taifa, wawe ufalme na makuhani kwa Mungu wetu,’ nao watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia. (Ufunuo 5:9, 10, NW) Kikundi hiki cha utawala chenye kushirikiana na Yesu Kristo ndio Ufalme aliofunza wafuasi wake kuuomba. Ndio pia njia ambayo kupitia kwayo kutawala kubaya kwa dunia kutakomeshwa, hivyo kurudisha haki na amani katika makao ya mwanadamu, dunia, vilevile uhai usio na mwisho kwa wakaaji wayo.—Zaburi 37:29; Mathayo 6:9, 10.

Kikundi cha Watawala Wachaguliwa

Kwa kuwa tawala za kibinadamu ambazo Ufalme unachukua mahali pazo zimejawa na ufisadi, je, hatuwezi kuona ni kwa nini wale watiwao ndani ya serikali hiyo ya kimbingu lazima wachaguliwe kwa uangalifu na kutahiniwa na Mungu? Hali ya sasa ya jamii ya kibinadamu yaweza kulinganishwa na ile ya mamia ya abiria waliomo ndani ya ndege kubwa iliyoharibika katika hali mbaya ya hewa. Katika hali hiyo hatari, ungetaka waongoza-ndege wachanga wasio na uzoefu? Sivyo hata kidogo! Hali hiyo ingetaka waongoza-ndege waliochaguliwa ifaavyo kulingana na viwango vigumu.

Kwa habari ya wale watakaotumikia mbinguni pamoja na Kristo Yesu, tunafarijiwa kujua kwamba “Mungu amevitia viungo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka.” (1 Wakorintho 12:18) Tamaa ya kibinafsi au kujitakia cheo katika Ufalme silo suala liamualo. (Mathayo 20:20-23) Viwango hususa vya imani na mwenendo vimewekwa na Mungu ili kuzuia kuingia kwa watu wasiostahili. (Yohana 6:44; Waefeso 5:5) Maneno ya kufungua ya Mahubiri ya Mlimani ya Yesu yaonyesha kwamba watawala wenzi pamoja na Kristo lazima wathibitike kuwa wakaziao akilini mambo ya kiroho, wenye tabia pole, wapendao uadilifu, wenye rehema, waliotakata moyo, na wenye kufanya amani.—Mathayo 5:3-9; ona pia Ufunuo 2:10.

Kwa kufurahisha, walio wengi sana wa wanadamu, ingawa hawajachaguliwa na Mungu kuwa miongoni mwa kikundi hiki kiwakilishi cha kimbingu cha watawala, hawaachwi bila tumaini. Watakaa katika dunia hii yenye kupendeza wafurahie manufaa za utawala wake wa kimungu. Majeruhi wa ukosefu wa haki waliokufa kitambo watarudishwa kwenye uhai waishi pamoja na wale watakaookoka ili kuuona Ufalme wa Mungu ‘ukija’ katika maana halisi. Ahadi hii itatimizwa: “Wanyofu watakaa katika nchi, na wakamilifu watadumu ndani yake.”—Mathayo 6:9, 10; Mithali 2:21; Matendo 24:15.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki