Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 1/22 uku. 31
  • “Maoni Yangu ya Wajibu wa Daktari Yamebadilika”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Maoni Yangu ya Wajibu wa Daktari Yamebadilika”
  • Amkeni!—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu
    Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu
  • Kulinda Salama Watoto Wenu na Matumizi Mabaya ya Damu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Wala Wafanya-Mizungu Wala Miungu
    Amkeni!—1994
  • Maswali ya Funzo kwa Ajili ya Broshua Damu Yaweza Kuokoaje Uhai Wako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 1/22 uku. 31

“Maoni Yangu ya Wajibu wa Daktari Yamebadilika”

AKANE, msichana wa miaka minne katika Osaka, Japani, alikuwa na kasoro za moyo zilizotatanika—dosari ya veli ya vipinde vitatu vya moyo na ya kuta za vyumba vya damu moyoni—zilizomlazimisha kufanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo. Wazazi wake waliwasihi madaktari waufanye upasuaji huo bila damu.a

Upasuaji wa kufungua moyo wazi bila damu ni mgumu kufanyiwa watoto kwa sababu ya kiasi chao kidogo cha damu. Katika kisa cha Akane, madaktari walikubaliana kupasua bila damu. Ikionyesha stadi zao bora zaidi za kitiba, upasuaji wa Akane ulifaulu. Alipona upesi na sasa afurahia afya nyingi.

Mama ya Akane aliwaandikia madaktari walioshiriki katika upasuaji huo, akitia ndani picha ya Akane ya majuzi. Tabibu fulani wa nusu-kaputi alijibu kwa kuandikia mama ya Akane. Kwa sehemu, barua hiyo ilisomeka hivi:

“Pono la kustaajabisha la Akane latusisimua. Nilikuwa na wakati mgumu kuzuia machozi yasinitoke nilipoona ile picha ya kupendeza uliyotia ndani ya barua yako. Kilichonifadhaisha sana hakikuwa ugumu wa upasuaji huo bali ni tofauti iliyopo kati ya imani zenu na zangu. Sasa, kutokana na ono hili, maoni yangu ya wajibu wa daktari yamebadilika. Madaktari wapaswa kutumia uelewevu wao thabiti wa ujuzi wa kitiba kuokoa uhai, lakini yawapasa pia wastahi hali ya kujiheshimu na mapendezi ya mgonjwa.”

[Maelezo ya Chini]

a Kwa kupatana na Matendo 15:29, Mashahidi wa Yehova hujiepusha na damu, kutia na mitio-damu mishipani. Hata hivyo, wao hukubali utumizi wa tiba isiyo na damu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki