Sababu Inayofanya Maaskofu wa Italia Waudhike
NA MLETA-HABARI WA AMKENI! KATIKA ITALIA
KATIKA Novemba 1993, mkutano wa maaskofu Waitalia ulitoa maelezo hasi kadhaa kuhusu Mashahidi wa Yehova. Ilisemekana kuwa hao si Wakristo na kwamba kuhubiri kwao nyumba kwa nyumba kulikuwa “kugeuza watu kidini kwa kulazimisha.”
Hata hivyo, si mamlaka zote za kidini zinakubali. Kwa kielelezo, Attilio Agnoletto, profesa wa historia ya Ukristo katika Chuo Kikuu cha Milan State, hueleza Mashahidi wa Yehova kuwa “harakati iliyo halali kabisa yenye nguvu, yenye kujitolea, ya Kibiblia ambayo katika hiyo hakuna chochote kisicho cha Kikristo.”
Namna gani “kugeuza watu kidini kwa kulazimisha”? “Neno ‘kwa kulazimisha’ halikubaliki hata kidogo,” profesa Agnoletto alieleza Amkeni! “Hiyo ingemaanisha kwamba kugeuza watu kidini kwa Yesu Kristo kulikuwa pia ‘kwa kulazimisha.’”
Kwa nini maaskofu hao wanaweka moyoni chuki ya aina hiyo dhidi ya Mashahidi wa Yehova? Profesa Agnoletto ahisi kwamba upinzani wao “hutokana na idadi yenyewe na mafanikio ya Mashahidi wa Yehova katika Italia leo,” ambayo, yeye aongeza, “yalingana na tatizo la uanadini wa Katoliki.”
Jamii ya makasisi leo hutafuta kuondolea sifa na kuzuia wale wanaotii amri ya Yesu ya kuhubiri. (Mathayo 28:19, 20; linganisha Mathayo 5:11, 12.) Gazeti-habari La Stampa laripoti kwamba japo upinzani, Mashahidi wa Yehova ndio kikundi cha kidini cha pili kwa ukubwa katika Italia, sasa wakiwa zaidi ya 200,000 na wakikua kwa kuendelea.
Kinyume cha hilo, Kanisa Katoliki limejionea hudhurio lenye kupungua katika miaka ya karibuni. Kwa hiyo mwanzoni mwa mwaka 1994, Papa John Paul 2 alisihi Wakatoliki Waitalia wawe waevanjeli watendaji, hata wahubiri nyumba kwa nyumba—sawa na wafanyavyo Mashahidi wa Yehova!a
[Maelezo ya Chini]
a Ona ukurasa 15.