Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 10/22 uku. 8
  • Kwa Nini Tunazeeka na Kufa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Tunazeeka na Kufa?
  • Amkeni!—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mfumo wa Utendaji Wenye Kasoro
  • Jibu Ni Nini?
  • Tuliumbwa Tuishi Milele
    Amkeni!—1995
  • Kwa Nini Sisi Huzeeka?
    Amkeni!—2006
  • Kutafuta Chembe ya Urithi “Isiyokufa”
    Amkeni!—2000
  • Je, Unaweza Kuepuka Kuzeeka?
    Amkeni!—2006
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 10/22 uku. 8

Kwa Nini Tunazeeka na Kufa?

“MBALI na ugunduzi kwamba mabadiliko ya umri hutukia ndani ya chembe moja-moja,” akiri Dakt. Leonard Hayflick, “hatujui kwa kadiri kubwa zaidi leo kuhusu kisababishi cha msingi cha kuzeeka kuliko tulivyojua karne moja iliyopita.” Kwa hakika, yeye asema: “Hatujui sababu nzuri kwa nini kuzeeka kunapaswa kutokea.”

Majaribio ya maabara yaliyofanywa miaka 30 hivi iliyopita yalifunua kwamba wakati chembe za kawaida za binadamu zilizotolewa kutoka kijusu zilipofanywa zikue chini ya mazingira fulani katika hali bora kabisa, kifo kilitokea baada ya chembe kugawanyika mara 50 hivi. Kwa upande ule mwingine, chembe zilizotolewa kutoka mtu mzee mno hugawanyika kati ya mara mbili na kumi tu kabla ya kufa. Hivyo, kitabu cha National Geographic Society The Incredible Machine kilionelea hivi: “Uthibitisho wa majaribio huunga mkono wazo la kwamba kifo kimepangwa kwetu sote wakati wa kuzaliwa.”

Hata hivyo, je, kukoma kwa mgawanyiko wa chembe ni jambo lisiloepukika? La, sivyo. “Kwa uhakika,” wakatoa maoni wataalamu wawili juu ya kuzeeka, Maprofesa Robert M. Sapolsky na Caleb E. Finch, “inaonekana kwamba kutozeeka ndiko kulikuwa hali ya awali ya viumbe-hai duniani.” Zaidi ya hilo, hata baadhi ya chembe za binadamu zenye kasoro hazizeeki.

Kitabu The Body Machine, kilichoandikwa na Dakt. Christiaan Barnard, aliyefanya mpachiko-moyo wa kwanza kutoka binadamu mmoja hadi mwingine, alieleza hivi: “Ugunduzi wa ‘chembe zisizoweza kufa’ ulileta tatizo lenye kutaabisha sana kwa wanabiolojia wanaotaka kujua hali ya kuzeeka, hadi ilipokuwa wazi kwamba chembe hizo zilikuwa na kasoro.” Ndiyo, aina fulani za chembe zenye kansa zaweza kutegemezwa kupitia migawanyiko isiyokwisha chini ya mazingira fulani yenye kuendelea! The World Book Encyclopedia kilitaarifu hivi: “Ikiwa wanasayansi wanaweza kupambanua jinsi chembe hizo zenye kasoro zinavyoendelea kuishi, wanaweza kupata ufahamu wenye kina kuhusu taratibu ya kuzeeka kwa chembe.” Hivyo, leo baadhi ya chembe za kansa zaweza kuzaana bila kukoma katika maabara, lakini chembe za kawaida zilizofanywa zikue huzeeka na kufa.

Mfumo wa Utendaji Wenye Kasoro

Je, kama The Body Machine kinavyosema, kuzeeka kwa binadamu na kufa kunasababishwa na “kupotea kwa uwezo wa uzaaji katika idadi [ya kawaida] ya chembe”? Ikiwa ndivyo, kitabu hicho kilisema, “ni jambo la maana kutafuta na kufahamu mfumo wa utendaji unaodhibiti uwezo huu usio na mwisho wa kujirudia ili kuweza kuutumia katika jaribio la kuongeza muda wa uhai wa binadamu.”

Kama uwezavyo kukumbuka katika makala iliyotangulia, Dakt. Hayflick alisema juu ya “miujiza inayotupata kutoka kutungwa mimba hadi kuzaliwa na kisha hadi upevuko wa kingono na utu uzima.” Kisha yeye akarejezea “mfumo wa utendaji ulio sahili zaidi wa kudumisha tu miujiza hiyo milele.”

Licha ya miaka mingi ya jitihada zilizounganishwa, wanasayansi wamekosa kugundua mfumo wa utendaji ambao utadumisha uhai milele. “Visababishi vya kuzeeka vinabaki vikiwa fumbo,” chakiri kitabu The Incredible Machine.

Hata hivyo, kisababishi cha kuzeeka na kifo kwa kweli si siri. Jibu lapatikana.

Jibu Ni Nini?

Aliye na jibu ndiye aliyefanya “miujiza inayotupata kutoka kutungwa mimba hadi kuzaliwa,” Muumba wetu mwenye hekima yote, Yehova Mungu. “Wewe ndiwe asili ya uhai,” Biblia yasema kumhusu. “Jueni kwamba BWANA [“Yehova,” New World Translation] ndiye Mungu; ndiye aliyetuumba.”—Zaburi 36:9, HNWW; 100:3.

Wazia jinsi kwa ajabu sana Yehova Mungu alipanga ukuzi wako katika mji wa mimba, akiandika, kitamathali, kitabu cha maagizo ya kukufanya wewe uwe mtu wa kipekee! “Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, uliniunga tumboni mwa mama yangu,” akaandika mtunga-zaburi wa Biblia. “Mifupa yangu haikusitirika kwako, . . . macho yako yaliniona kabla sijakamilika; chuoni mwako ziliandikwa zote pia.” (Zaburi 139:13, 15, 16, italiki ni zetu.) Bila shaka, mwili wetu ulioumbwa kwa njia ya ajabu si tokeo la nasibu tu!

Hata hivyo, ikiwa Yehova Mungu alituumba tukiwa wakamilifu ili tuweze kuishi milele, kwa sababu gani tunazeeka na kufa? Jibu lapatikana katika katazo alilowekewa mwanadamu wa kwanza, Adamu, ambaye Mungu alimweka katika makao yenye kupendeza duniani. Mungu alimwamuru hivi: “Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.”—Mwanzo 2:16, 17, italiki ni zetu.

Ni nini kilichotokea? Badala ya kutii Baba yake wa kimbingu, Adamu alikosa kutii, akijiunga na mke wake, Hawa, katika kula matunda ya mti huo. Wao waliamini kwa uchoyo ahadi ya uwongo ya mwasi wa kimalaika. (Mwanzo 3:1-6; Ufunuo 12:9) Kwa hiyo, kama Mungu alivyowaonya, walikufa. Ingawa Adamu na Hawa waliumbwa wakiwa na uwezo wa kuishi milele, hilo lilitegemea kumtii Mungu. Kwa kutotii, wao walitenda dhambi. Kisha, wakiwa watenda-dhambi, walipitisha kasoro yenye kuleta kifo katika miili yao kwa wazao wao wote. “Hivyo kifo kimeenea katika jumuiya yote ya binadamu.”—Warumi 5:12, HNWW; Ayubu 14:4.

Hata hivyo, hili halimaanishi kwamba hakuna tumaini la kushinda kuzeeka na kifo. Haipasi kuwa vigumu kuamini kwamba Muumba wetu mwenye hekima yote anaweza kutibu hali zozote zisizo za kawaida za urithi wa kijeni na kutoa nguvu ya kuendeleza maisha zetu milele. Lakini yeye atafanyaje hivyo? Na ni lazima tufanye nini ili tufurahie ahadi zake za uhai udumuo milele?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki