Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g98 6/8 uku. 3
  • Mtoto Aliyeitwa Maskini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mtoto Aliyeitwa Maskini
  • Amkeni!—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Wafungwa wa Umaskini
    Amkeni!—1998
  • Umaskini Unaoongezeka—Tisho kwa Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Jitihada za Kumaliza Umaskini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Karibuni, Hakuna Atakayekuwa Maskini!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1998
g98 6/8 uku. 3

Mtoto Aliyeitwa Maskini

KATIKA kijiji kimoja kidogo cha Kiafrika, mwanamume mmoja aliyeitwa Okot na mke wake, Matina, walifurahia kuzaliwa kwa mtoto wao wa kwanza, aliyekuwa binti. Jamaa na marafiki walisafiri hadi kijijini ili kupeleka zawadi na kumtakia mtoto huyo maisha marefu na yenye furaha.

Wenzi hao waliishi maisha magumu na ya umaskini. Walilima shamba dogo, na nyumba yao ambamo alijifungulia Matina, ilikuwa ya matope na paa ya nyasi. Waliazimia kufanya kazi kwa bidii ili mtoto wao wa kwanza asipate magumu kama wao. Ili kujikumbusha mradi huu, walimwita binti yao Acan, linalomaanisha “Mimi Ni Maskini.”

Kuna wakati ujao wa aina gani kwa Acan? Ikiwa maisha yake yatafuata kigezo cha maisha ya wengi katika nchi yao, huenda asijifunze kamwe kusoma na kuandika. Atakapokuwa mtu mzima, ikiwa atapata kazi, aweza kupata mshahara unaokaribia dola 190 tu kwa mwaka. Katika nchi yao, matarajio ya muda wa kuishi ni miaka 42 pekee.

Hali mbaya ya Acan si ya kipekee. Kati ya watu wanaokaribia bilioni 6 duniani, wapatao bilioni 1.3 hupata pesa zipunguazo dola 370 kwa mwaka. Wastani katika nchi tajiri ni dola 21,598. Kila siku, watu 67,000 zaidi hujiunga na umati wa maskini, karibu milioni 25 kila mwaka. Wengi huishi katika nchi zinazositawi—katika Afrika, Asia, na Amerika ya Latini. Lakini hata katika mataifa tajiri, kuna sehemu ndogo-ndogo zilizo na umaskini. Na watu 7 kati ya 10 miongoni mwa walio maskini zaidi ulimwenguni ni wa kike.

Watu wengi hawaepuki ufukara kamwe. Huwanyima mahitaji yao yaliyo ya msingi zaidi—chakula, mavazi, na makao. Unaweza kuwapokonya uhuru, adhama, elimu, na afya njema. Shirika la Afya Ulimwenguni lasema: “Umaskini hutawala kwa njia yenye kuharibu kila hatua ya maisha ya binadamu, kuanzia wakati wa utungaji wa mimba hadi kaburini. Huungana na maradhi hatari zaidi na yenye maumivu zaidi ili kusababisha maisha duni kwa wote wanaoteseka kutokana nao.”

Lakini je, kiwango cha maisha hakiendelei kuboreka katika mataifa yanayositawi? Katika baadhi ya mataifa hayo, ndiyo. Katika mengine mengi, sivyo. Gazeti la ukuzi wa kibinadamu Choices hufafanua wazo la kwamba “pengo kati ya maskini na matajiri linapungua kwa sababu hali ya maskini inaboreka” kuwa ‘ngano hatari.’ Badala yake linataarifu: “Twaishi katika ulimwengu ambao kwa kweli umegawanyika kiuchumi, miongoni mwa nchi na ndani ya nchi hizo.”

Je, umaskini utaendelea kutaabisha jamii ya kibinadamu milele? Katika makala mbili zifuatazo, Amkeni! yachunguza habari hii iliyo tata na kuonyesha utatuzi utakuwa nini.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki