Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yy sura 1 kur. 4-8
  • Kuishi kwa Ajili ya Leo na Kesho

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuishi kwa Ajili ya Leo na Kesho
  • Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MISAADA YA KUONGOZEA MWENDO WAKO
  • TUMIA NJIA ZA KUPASHANA HABARI
  • Vijana, Je, Mnajitayarisha kwa Ajili ya Wakati Ujao?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Vijana—Sehemu Yenu Katika Jamaa Yenye Furaha, Yenye Umoja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Itikio la Wasomaji kwa Kitabu ”Young People Ask”
    Amkeni!—1991
  • Jinsi ya Kufanikisha Ujana Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Kupata Faida Zote za Ujana Wako
yy sura 1 kur. 4-8

Sura ya 1

Kuishi kwa Ajili ya Leo na Kesho

1-5. Sababu gani ujana umepaswa uwe wakati wenye furaha? Hata hivyo ni nini kinachoufanya uwe wenye magumu?

UJANA wako umepaswa uwe wakati wa maisha ulio mzuri sana. Ni kama masika ya mwaka. Ujana ni wakati wa nguvu za uchanga. Wakati huo mwili wako unazidi kupata nguvu na vilevile akili zako zinaongezeka. Nafasi nyingi za kujifunza na kufanya vitu zinapatikana. Hivyo kuna sababu nyingi za kufanya ujana uwe wakati wenye furaha na wenye kuchangamsha.

2 Lakini, je utakuwa na wakati kama huo, au unao sasa? Kuna mambo mengi yanayoweza kukusaidia au kukuzuia usiwe na wakati huo. Mengine kati ya hayo ni mambo usiyoweza kuzuia. Lakini unaweza kuzuia mengi. Kitabu hiki kimeandikwa kikusaidie upate faida zote za ujana wako.

3 Ujana ni wakati wenye magumu. Kama unavyojua, maisha ya leo yana vizuizi vingi. Uhodari unatakiwa ili uvishinde. Lakini ukijifunza mapema namna ya kuvishinda, ndipo sehemu nyingine ya maisha yako inapokuwa nyepesi zaidi. Uhodari wako utaongezeka kila utakaposhinda gumu.

4 Afadhali kushinda magumu ya ujana kuliko kuacha yakupotoe. Ndiyo, ingekuwa vyepesi kuwaza au kujipumbaza tu ukidhani kwamba maisha ni tofauti na yalivyo. Lakini mwishowe, wale wanaofanya hivyo wataingia katika taabu. Hapo inaweza kuwa vigumu sana kutoka katika taabu hiyo na kusonga mbele. Wakati wa maana sana ungepotea, kwa sababu huwezi kurudia ujana tena.

5 Sasa hivi uko katika wakati wa mageuzo mengi. Kwa mfano, mwili wako unaelekea kukomaa. Lakini haufikii hali hiyo mpaka unapokuwa mwenye umri wa miaka kati ya 20 na 23. Bado inaweza kuchukua muda mrefu zaidi uweze kuyaongoza vizuri maoni yako ya moyoni. Labda mengine kati ya mageuzo ya mwili wako yanaweza kukuvuruga akili au kukutia wasiwasi. Unapoona mikazo mingine ikiongezeka katika mwili wako, unafanyaje? Kitabu hiki kinazungumza mageuzo hayo yanayotukia wakati wa ujana na namna ya kuyaweza. Unaweza hata kufurahia kupatwa na magumu yanayoletwa na mageuzo hayo, kwa maana yote ni sehemu ya matukio ya maana ya kugeuka kuwa mtu aliye pekee, yaani, Wewe.

MISAADA YA KUONGOZEA MWENDO WAKO

6-9. Unaweza kupata faida namna gani kwa kujifunza mambo ambayo watu wengine wamefanya?

6 Labda nyakati nyingine itaonekana kama maisha yako yanazuiwa sana, utaona kama yamejaa sheria nyingi za kukuamuru ufanye hivi au usifanye hivi. Lakini ujue kwamba unapokuwa kijana, una uhuru ambao hutakuwa nao wakati ujao. Mahali pa kulemewa na madaraka mengi kama watu wazima, wewe una uhuru wa kutumia wakati mwingi upate maarifa na kusitawisha akili zako na kujua ufundi mwingi zaidi wa kujifunza na kufikiria mambo ambayo watu wengine wamefanya au wanayafanya. Unaweza kujifunza juu ya mambo waliyoweza kutimiza na yale waliyoshindwa kutimiza, unaweza kuona mambo ya akili au makosa ya kipumbavu waliyofanya. Hii inaweza kukusaidia ujue upande ambao unataka kuelekea katika maisha.

7 Je! unaweza kuamua upande ambao unataka kuelekea bila msaada wo wote? Je! lingekuwa jambo la akili kujaribu kufanya hivyo? Ona mifano fulani:

8 Tuseme unataka kuunda mtambo (injini) wa motokaa. Je! ungeanza kufanya hivyo peke yako bila kuomba kwanza maoni ya mafundi wa mitambo wenye ujuzi? Ikiwa ungefanya hivyo, ile motokaa ingekuwaje? Au ungejaribu kushona vazi la karamu ikiwa hujamwona mtu akishona, au bila mfano wa kufuata? Unajua namna vazi hilo lingekuwa.

9 Basi, ni wazi kwamba maisha ya kibinadamu ni magumu kufahamika kuliko mtambo wa motokaa au vazi la karamu, sivyo?

TUMIA NJIA ZA KUPASHANA HABARI

10-16. (a) Sababu gani vijana wengine hawataki kujifunza kwa watu wazima? Wewe waonaje hilo? (b) Zaidi ya kuwasikiliza watu wazima, sababu gani twahitaji vilevile chanzo kingine ili tupate habari juu ya maisha?

10 Ni jambo la kawaida kwamba kila mmoja wetu anaongeza maarifa yake kwa kujifunza mambo ambayo wengine waliotutangulia walijifunza. Lakini huwezi kufanya hivyo pasipo njia ya kupashana habari. Pasipo kupashana habari—pasipo kusema, pasipo kusoma, pasipo kuona wengine wanavyofanya—huwezi kupata maarifa wala ujuzi ambao wengine wamepata.

11 Ili upate faida zote za ujana wako ni lazima ujifunze mambo ambayo wengine wamejifunza. Hilo ni pamoja na mambo kama kutunza mwili wako vizuri sana, namna ya kufanya urafiki na kushirikiana na watu ambao ni wazuri kweli kweli, maongozi yanayofaa juu ya matembezi ya wavulana pamoja na wasichana na uchumba, na majibu ya maulizo juu ya ndoa, ngono na matumizi ya vileo au dawa zenye kulevya. Yote hayo yanazungumzwa katika kitabu hiki.

12 Lakini labda unafikiria yale unayoona leo mahali unapoishi. Kuna choyo kingi. Watu wengi wanaonewa. Tena kuna udanganyifu mwingi, uchafu, uvunjaji wa sheria, vita na unafiki. Basi, labda utauliza hivi : ‘Nawezaje kujifunza kwa watu wazima, nao ndio wameharibu sana mambo?’

13 Kweli, leo watu wazima wengi wana hatia ya kuleta hali hizo. Ama wanashiriki mabaya hayo ama wanayakubali na kuziunga mkono taratibu zinazofanyiza hali hizo.

14 Kwa upande mwingine, je! hawako watu wazima wengi wanaochukizwa sana kama wewe wanapoona namna mambo yanavyotendeka? Hata hivyo, magumu hayo hayakuanza kusitawi katika kizazi kimoja tu. Wazazi wako walipokuwa na umri kama wewe, waliiona hali ya ulimwengu kuwa yenye kuvunja moyo vilevile. Kwa muda wa nusu karne iliyopita, zaidi tangu vita ya kwanza ya ulimwengu ya mpaka 1914 mpaka 1918, watu wanaendelea kupata mambo yanayozidi kuwa magumu sana.

15 Kuwa mtu mzima au kuwa na ujuzi zaidi tu hakuondoi kabisa magumu ya maisha. Kama ni hivyo mambo yangekuwa yakiendelea kuwa mazuri zaidi kila mahali. Lakini sivyo yalivyo. Basi, zaidi ya kupata ujuzi kutoka kwa wengine, je? kuna chanzo kingine cha habari na msaada kilicho bora zaidi unachoweza kuendea?

16 Ndiyo, kiko. Sasa tutazungumza juu yake.

[Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 4]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki