Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 41
  • Nyoka wa Shaba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nyoka wa Shaba
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Ibada ya Nyoka—Nyakati za Kale na Sasa
    Amkeni!—2010
  • Uwongo wa Kawaida Kuhusu Nyoka
    Amkeni!—1998
  • Ngozi ya nyoka
    Amkeni!—2014
  • Kichaka Kinachowaka Moto
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 41
Waisraeli walioumwa na nyoka, wanamtazama nyoka wa Musa aliyefanyizwa kwa shaba

HADITHI YA 41

Nyoka wa Shaba

JE! HUYO anaonekana kama nyoka wa kweli aliyezungushwa juu ya mti? Hapana. Nyoka huyo amefanyizwa kwa shaba. Yehova alimwambia Musa amweke juu ya mti ili watu wamtazame waishi. Lakini nyoka wengine chini ni wa kweli. Wamewauma watu na kuwafanya wagonjwa. Unajua kwa nini?

Ni kwa sababu Waisraeli wamempinga Mungu na Musa. Wanalaumu hivi: ‘Kwa nini ulitutoa Misri ili tufe huku jangwani? Hakuna chakula wala maji huku. Tumechoka kula mana hii.’

Lakini mana hiyo ni chakula kizuri. Yehova amewapa mana hiyo kwa mwujiza. Na kwa mwujiza amewapa maji pia lakini watu hawamshukuru Mungu kwa vile alivyowaangalia. Basi Yehova anawapeleka nyoka hao wenye sumu ili awaadhibu Waisraeli. Nyoka hao wanawauma, na wengi wao wanakufa.

Mwishowe watu wanamwendea Musa na kusema: ‘Tumefanya dhambi, kwa sababu tumepinga Yehova na wewe. Basi mwombe Yehova awaondoe nyoka hawa.’

Musa anaombea watu. Naye Yehova anamwambia Musa afanyize nyoka huyu wa shaba. Anamwambia amweke juu ya mti, ili mtu anayeumwa amtazame. Musa anafanya kama anavyoambiwa na Mungu. Watu walioumwa wanamtazama nyoka wa shaba wanapona.

Kuna jambo la kujifunza kutokana na hayo. Sote tuko kama Waisraeli hao walioumwa na nyoka hao. Sote tuko katika hali ya kufa. Ebu tazama huku na huku, utaona kwamba watu wanazeeka, wanakuwa wagonjwa, na kufa. Ni kwa sababu yule mwanamume na mwanamke wa kwanza, Adamu na Hawa walijitenga na Yehova, na sote ni watoto wao. Lakini Yehova amefanya njia ili tuweze kuishi milele.

Musa na nyoka wa shaba

Yehova alimtuma Mwanawe, Yesu Kristo, duniani. Yesu aliwekwa juu ya mti, kwa sababu watu wengi walidhani alikuwa mbaya. Lakini Yehova alimtoa Yesu atuokoe. Tukimtazama, tukimfuata, ndipo twaweza kuwa na uzima wa milele. Lakini tutajifunza zaidi juu ya hilo baadaye.

Hesabu 21:4-9; Yohana 3:14, 15.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki