Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 42
  • Punda Anasema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Punda Anasema
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Punda wa Balaamu Anazungumza
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Mwanamume Aliyepinga Mapenzi ya Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Yehova Anawabariki Walio Waaminifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Tungefanya Nini Bila Punda?
    Amkeni!—2006
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 42
Punda anasema na Balaamu kwa sababu malaika anamzuia kupita

HADITHI YA 42

Punda Anasema

JE! UMEPATA kusikia kwamba punda anasema? ‘Hapana,’ labda unasema. ‘Wanyama hawawezi kusema.’ Lakini Biblia inasimulia hivyo. Na tuone ilivyokuwa.

Waisraeli wako karibu sana kuingia nchi ya Kanaani. Balaki, mfalme wa Moabu, anawaogopa Waisraeli. Basi anapeleka habari ili mtu mwerevu jina lake Balaamu awalaani Waisraeli. Balaki anaahidi kumpa Balaamu fedha nyingi sana, basi Balaamu anapanda punda wake kwenda kumwona Balaki.

Yehova hataki Balaamu alaani watu wake. Basi anamtuma malaika mwenye upanga mrefu akasimame njiani amzuie Balaamu. Balaamu hawezi kumwona malaika, lakini punda anamwona. Basi punda huyo anaepa-epa huyo malaika, na mwishowe analala njiani. Balaamu anakasirika sana, na kumpiga punda wake kwa fimbo.

Ndipo Yehova anamfanya Balaamu asikie punda wake akisema naye. ‘Nimekukosea nini hata unipige?’ punda anauliza.

‘Umenifanya mpumbavu,’ Balaamu anasema. ‘Kama ningekuwa na upanga ningekuua!’

‘Je! nimekufanyia hivyo zamani?’ punda anauliza.

‘Hapana,’ Balaamu anajibu.

Ndipo Yehova anamwonyesha Balaamu malaika aliye na upanga anasimama njiani. Malaika anasema hivi: ‘Kwa nini umempiga punda wako? Nimekuja nikuzuie njia usiende kulaani Waisraeli. Kama punda wako hangeniepa, ningekupiga ufe.’

Balaamu anasema: ‘Nimefanya dhambi. Sikujua kama ulikuwa ukisimama njiani.’ Malaika huyo anamruhusu Balaamu aende, naye Balaamu anaendelea na safari ya kumwona Balaki. Bado anajaribu kulaani Waisraeli, lakini, badala yake, Yehova anamwongoza abariki Waisraeli mara tatu.

Hesabu 21:21-35; 22:1-40; 23:1-30; 24:1-25.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki