Hesabu
24 Balaamu alipoona kwamba Yehova alifurahia* kuwabariki Waisraeli, hakwenda tena kutafuta ishara za msiba,+ bali aliugeuza uso wake kutazama nyikani. 2 Balaamu alipotazama na kuwaona Waisraeli wakiwa wamepiga kambi kulingana na makabila yao,+ roho ya Mungu ikamjia.+ 3 Kisha akasema maneno haya ya kishairi:+
“Maneno ya Balaamu mwana wa Beori,
Na maneno ya mwanamume ambaye macho yake yamefunguliwa,
4 Maneno ya mtu anayesikia neno la Mungu,
Aliyeona maono ya Mweza-Yote,
Aliyeinama chini macho yakiwa yamefumbuliwa:+
6 Yameenea mbali kama mabonde,+
Kama bustani kando ya mto,
Kama mimea ya udi iliyopandwa na Yehova,
Kama mierezi kando ya maji.
7 Maji yanaendelea kutiririka kutoka katika ndoo zake mbili za ngozi,
8 Mungu anamtoa Misri;
Yeye ni kama pembe za fahali mwitu kwa Waisraeli.
Atayala mataifa, wale wanaomkandamiza,+
Na mifupa yao ataitafuna-tafuna, naye atawapasua-pasua kwa mishale yake.
9 Amejikunyata, amelala chini kama simba,
Na kama simba, ni nani anayethubutu kumwamsha?
Wale wanaokubariki wamebarikiwa,
Na wale wanaokulaani wamelaaniwa.”+
10 Ndipo Balaki akamkasirikia sana Balaamu. Akapiga makofi kwa dharau na kumwambia Balaamu: “Nilikuita uwalaani maadui wangu,+ badala yake umewabariki mara tatu. 11 Sasa rudi nyumbani mara moja. Nilitaka kukuthawabisha sana,+ lakini Yehova amekunyima thawabu.”
12 Balaamu akamwambia Balaki: “Je, sikuwaambia hivi wajumbe uliowatuma kwangu: 13 ‘Hata Balaki akinipa nyumba yake mwenyewe iliyojaa fedha na dhahabu, siwezi kwa hiari yangu* kukiuka jambo lolote ambalo Yehova ameniagiza nifanye, liwe jambo zuri au baya. Nitasema tu jambo ambalo Yehova ataniambia’?+ 14 Na sasa naenda kwa watu wangu. Njoo nikwambie* mambo ambayo watu hawa watawatendea watu wako wakati ujao.”* 15 Kwa hiyo akasema maneno haya ya kishairi:+
“Maneno ya Balaamu mwana wa Beori,
Na maneno ya mwanamume ambaye macho yake yamefunguliwa,+
16 Maneno ya mtu anayesikia neno la Mungu,
Na yule anayemjua Aliye Juu Zaidi,
Aliona maono ya Mweza-Yote
Alipokuwa akiinama chini macho yake yakiwa yamefunguliwa:
17 Nitamwona, lakini si sasa;
Nitamtazama, lakini si hivi karibuni.
Naye hakika atapasua paji la uso la Moabu+
Na fuvu la kichwa la wana wote wa vurugu.
20 Alipowaona Waamaleki, aliendelea kusema maneno yake ya kishairi:
21 Alipowaona Wakeni,+ aliendelea kusema maneno yake ya kishairi:
“Makao yenu yako salama, yamejengwa juu ya mwamba.
22 Lakini mtu fulani atawateketeza Wakeni.*
Ni muda gani unaobaki kabla ya Ashuru kuwachukua mateka?”
23 Akaendelea kusema maneno yake ya kishairi:
“Lo! Ni nani atakayeokoka Mungu atakapofanya hivyo?
Lakini wao pia wataangamia* kabisa.”
25 Kisha Balaamu+ akaondoka na kurudi kwake. Balaki pia akaenda zake.