Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • je kur. 6-7
  • Kundi la Kikristo la Karne ya Kwanza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kundi la Kikristo la Karne ya Kwanza
  • Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
  • Habari Zinazolingana
  • Twahitaji Tengenezo la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • ‘Mlango Unaoongoza Kwenye Utendaji Wafunguka’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Kutaniko na Lijengwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Mashahidi wa Kikristo wa Yehova Katika Karne ya Kwanza
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
je kur. 6-7

Kundi la Kikristo la Karne ya Kwanza

Wakati wa Pentekoste mwaka 33 W.K., roho takatifu ilimiminwa juu ya kikundi cha wanafunzi wa Yesu 120, nao wakaanza kusema juu ya mambo ya ajabu ya Mungu katika lugha nyingi. Huo ulikuwa ndio mwanzilisho wa kundi la Kikristo. Karibu wanafunzi wapya 3,000 walibatizwa siku hiyo. —Matendo sura 2.

Makundi katika mahali mbalimbali yaliongezeka hesabu wakati mitume na wengine walipoendelea kulisema Neno la Mungu kwa ujasiri. Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Matendo, bila kukawia kazi ya kuhubiri ilienea eneo lote la Mediterania, kutoka Babuloni na Afrika Kaskazini mpaka Roma na labda Hispania. —Warumi 15:18-29; Wakolosai 1:23; 1 Petro 5:13.

Ko kote ambako watu waligeuka wakawa wanafunzi, walianzisha makundi. Wanaume wenye kustahili, waliokomaa, waliwekwa kuwa wazee au waangalizi, ili wadumishe kiwango cha mafundisho ya kweli na mwenendo katika makundi. Lakini wao hawakuwa jamii ya makasisi; wao walikuwa wahudumu na wafanya kazi wa Ufalme wa Mungu. —Matendo 14:23; 20:28; 1 Wakorintho 3:5; 5:13; Wakolosai 4:11; 1 Timotheo 3:1-15; Waebrania 13:17; 1 Petro 5:1-4.

Mitume na wafanya kazi wenzao wengine wa karibu sana walitumikia wakiwa baraza linaloongoza. Waliongoza katika kazi ya kuhubiri. Walitatua matatizo katika kundi la Yerusalemu. Walituma ndugu wenye kustahili waende Samaria na Antiokia wakawatie nguvu huko waamini wapya. Walishughulikia ubishi juu ya tohara, wakipeleka uamuzi wao kwa makundi yote ili yaufuate. Hata hivyo wanaume hao hawakuwa mabwana juu ya wengine bali walikuwa watumishi na wafanyi kazi wenzi wa kundi lote. —Matendo 4:33; 6:1-7; 8:14-25; 11:22-24; 15:1-32; 16:4, 5; 1 Wakorintho 3:5-9; 4:1, 2; 2 Wakorintho 1:24.

Wanafunzi wa kwanza walijulikana kuwa Wakristo, wakiitwa hivyo kwa uongozi wa kimungu. Pia walikuwa na mafundisho yaliyowatofautisha; hayo yaliitwa mafundisho ya mitume, au kiolezo cha maneno yenye afya. Mafundisho hayo ya Kimandiko yalijulikana pia kuwa ukweli. —Yohana 17:17; Matendo 2:42; 11:26; Warumi 6:17; 1 Timotheo 4:6; 6:1, 3; 2 Timotheo 1:13; 2 Petro 2:2; 2 Yohana 1, 4, 9.

Wao walikuwa ushirika wa ndugu ulimwenguni pote ulioungana katika upendo. Walionyesha kupendezwa na waamini wenzao katika nchi nyingine. Walipokuwa wakisafiri kwenda nchi nyingine, waamini wenzao waliwakaribisha katika nyumba zao. Walidumisha kiwango cha hali ya juu cha mwenendo wa adili, wakiwa watu watakatifu waliojitenga na ulimwengu. Waliendelea kuuweka karibu akilini wakati wa siku ya kuwapo kwa Yehova na kwa bidii wakafanya tangazo peupe la imani yao. —Yohana 13:34, 35; 15:17-19; Matendo 5:42; 11:28, 29; Warumi 10:9, 10, 13-15; Tito 2:11-14; Waebrania 10:23; 13:15; 1 Petro 1:14-16; 2:9-12; 5:9; 2 Petro 3:11-14; 3 Yohana 5-8.

Hata hivyo, kama ilivyotabiriwa, ukengeufu mkuu (uasi-imani) ulianza kutokea, katika karne ya pili na ya tatu. Hilo likatokeza mifumo mikubwa ya makanisa ambayo hayakudumisha usafi ule wa kundi la Kikristo la kwanza juu ya mafundisho, mwenendo, tengenezo, na msimamo walo kuelekea ulimwengu. —Mathayo 13:24-30, 37-43; 2 Wathesalonike, sura ya 2.

Ingawaje, Yesu alitabiri kwamba kungekuwako kurudishwa kwa ibada ya kweli katika umalizio wa mfumo wa mambo. Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba kurudishwa huko kwaweza kuonwa katika utendaji wao wa ulimwenguni pote katika wakati wetu, karibu miaka 1,900 baada ya Yesu kutoa unabii wake. Kurasa zinazofuata zitaeleza sababu.

• Kundi la Kikristo lilianzishwaje, na lilikuaje?

• Kundi hilo lilisimamiwaje?

• Ni mambo gani yaliyotofautisha waziwazi Wakristo wa karne ya kwanza?

[Ramani katika ukurasa wa 7]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Bahari Nyeusi

Bahari Kaspiani

Bahari Kuu

Bahari ya Sham

Ghuba ya Ajemi

Maeneo yaliyofikiwa kwa habari njema katika karne ya kwanza

ITALIA

Roma

UGIRIKI

MELITA

KRETE

SAIPRASI

BITHINIA

GALATIA

ESIA NDOGO

KAPADOKIA

KILIKIA

SIRIA

ISRAELI

Yerusalemu

MESOPOTAMIA

Babuloni

Wengine kutoka maeneo haya wakawa waamini

ILIRIKO

UMEDI

PARTHIA

ELAMI

UARABUNI

LIBYA

MISRI

ETHIOPIA

[Picha katika ukurasa wa 7]

Wakristo wa kwanza walihubiri Neno la Mungu kwa ujasiri

Wakristo walikaribishwa katika nyumba za waamini wenzao ko kote walikosafiri

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki