Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • re sura 31 kur. 215-220
  • Kazi za Yehova—Kubwa na za Ajabu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kazi za Yehova—Kubwa na za Ajabu
  • Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wimbo wa Musa na wa Mwana-Kondoo
  • Malaika Wenye Mabakuli
  • Yehova Katika Patakatifu Pake
  • Mabakuli na Mipigo ya Tarumbeta
  • Kutazama Ufunuo kwa Njia ya Uchunguzi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ufunuo—II
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Kitabu cha Biblia Namba 66—Ufunuo
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Njozi Zenye Kusisimua Zinazoimarisha Imani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
re sura 31 kur. 215-220

Sura ya 31

Kazi za Yehova—Kubwa na za Ajabu

Njozi ya 10—Ufunuo 15:1–16:21

Habari: Yehova akiwa katika patakatifu pake; mabakuli ya hasira-kisasi yake yamwagwa ndani ya dunia

Wakati wa utimizo: 1919 hadi Har–Magedoni

1, 2. (a) Ni ishara gani ya tatu anayoripoti Yohana? (b) Ni daraka gani la kimalaika ambalo watumishi wa Yehova wamejua kwa muda mrefu?

MWANAMKE akizaa mtoto wa kiume! Drakoni mkubwa akitafuta kumeza huyo mtoto! Hizo ishara mbili za kimbingu, zikionyeshwa kitaswira kwa njia iliyo wazi sana katika Ufunuo sura ya 12, zilitusisitizia kwamba lile bishano la muda mrefu linalohusu Mbegu ya mwanamke wa Mungu na Shetani na mbegu yake ya roho waovu linafikia upeo walo. Katika kukazia vifananisho hivi, Yohana anasema? “Na ishara kubwa ilionwa katika mbingu . . . Na ishara nyingine ikaonwa.” (Ufunuo 12:1, 3, 7-12, NW) Sasa, Yohana anaripoti ishara ya tatu: “Na mimi nikaona katika mbingu ishara nyingine, kubwa na ya ajabu, malaika saba wakiwa na tauni saba. Hizi ndizo za mwisho, kwa sababu kwa njia yazo kasirani ya Mungu inaletwa kwenye tamati.” (Ufunuo 15:1, NW) Ishara hii ya tatu vilevile ina maana ya umuhimu kwa watumishi wa Yehova.

2 Angalia madaraka ya maana waliyo nayo malaika katika kutimiza penzi la Mungu. Uhakika huu umejulikana na watumishi wa Yehova kwa muda mrefu. Kwani, chini ya uvuvio mwandikaji wa zaburi wa kale hata alinena kwa malaika kama hao, akiwahimiza: “Barikini Yehova, O nyinyi malaika zake, wenye uweza katika nguvu, mtimizao neno lake, kwa kusikiliza sauti ya neno lake”! (Zaburi 103:20, NW) Sasa, katika mandhari mpya hii, malaika wanapewa mgawo wa kumimina tauni saba za mwisho.

3. Ni nini zilizo tauni saba, na kuzimimina kunaonyesha nini?

3 Hizi ni tauni gani? Kama vile ile mipigo saba ya tarumbeta, hizo ni matamko makali ya hukumu yakitangaza peupe maoni ya Yehova ya sura tofautitofauti za ulimwengu huu na kuonya juu ya tokeo la mwisho la maamuzi yake ya kihukumu. (Ufunuo 8:1–9:21) ‘Kumiminwa kwazo kunaelekeza kwenye kutekelezwa kwa hukumu hizo, wakati vitu vya hasira-kisasi ya Yehova vinapoharibiwa katika siku ya kasirani yake yenye kuwaka. (Isaya 13:9-13; Ufunuo 6:16, 17) Hivyo, kwa njia yazo “kasirani ya Mungu inaletwa kwenye tamati.” Lakini kabla ya kueleza huko ‘kumiminwa kwa tauni,’ Yohana anatuambia juu ya binadamu fulani ambao hawataathiriwa vibaya nazo. Wakiwa wamekataa alama ya hayawani-mwitu, washikamanifu hawa wanaimbia Yehova sifa wanapopiga mbiu ya siku yake ya kisasi.—Ufunuo 13:15-17, NW.

Wimbo wa Musa na wa Mwana-Kondoo

4. Sasa ni kitu gani kinachokuja katika mtazamo wa Yohana?

4 Sasa picha nzuri ajabu inakuja katika mtazamo wa Yohana: “Na mimi nikaona kilichoonekana kuwa kama bahari ya kioo yenye kutangamana na moto, na wale ambao hutoka wakiwa washindi wa hayawani-mwitu na mfano wake na nambari ya jina lake wakisimama karibu ya bahari ya kioo, wakiwa na vinubi vya Mungu.”—Ufunuo 15:2, NW.

5. Ni nini inayotolewa picha na “bahari ya kioo yenye kutangamana na moto”?

5 “Bahari ya kioo” ni ile ile ambayo Yohana aliona mapema zaidi, ikiwa mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu. (Ufunuo 4:6, NW) Inafanana na “bahari ya kuyeyushwa,” au chombo cha kuwekea maji cha hekalu la Solomoni, ambamo makuhani walipata maji wajisafishe wenyewe. (1 Wafalme 7:23, NW) Hivyo hiyo ni kiwakilishi kizuri cha “mwosho wa maji,” yaani, Neno la Mungu, ambalo Yesu hutumia kusafisha kundi la kikuhani la Wakristo wapakwa-mafuta. (Waefeso 5:25, 26; Waebrania 10:22, NW) Hii “bahari ya kioo” ni “yenye kutangamana na moto,” kuonyesha kwamba wapakwa-mafuta hawa hutahiniwa na kutakaswa wanapotii kiwango cha juu walichowekewa. Na zaidi, hutukumbusha kwamba pia Neno la Mungu lina semi za hukumu zenye moto dhidi ya maadui wake. (Kumbukumbu 9:3; Sefania 3:8) Baadhi ya hukumu hizi zenye moto zinadhihirishwa katika tauni saba ambazo zi karibu kumiminwa.

6. (a) Ni nani walio waimbaji wanaosimama mbele ya bahari ya kioo, na sisi tunajuaje? (b) Ni katika njia gani wao ‘wametoka wakiwa washindi’?

6 Uhakika wa kwamba bahari ya kuyeyushwa katika hekalu la Solomoni ilikuwa ya kutumiwa na makuhani huonyesha kwamba wale waimbaji wanaosimama mbele ya bahari ya kioo ya kimbingu ni wa jamii ya kikuhani. Wana “vinubi vya Mungu,” na kwa hiyo sisi tunawatambulisha na wazee 24 na 144,000, kwa kuwa vikundi hivi viwili pia huimba kwa kufuatanisha na kinubi. (Ufunuo 5:8; 14:2) Waimbaji ambao Yohana huona “hutoka wakiwa washindi wa hayawani-mwitu na mfano wake na nambari ya jina lake.” Kwa hiyo lazima wao wawe wa wale 144,000 wanaoishi duniani wakati wa siku za mwisho. Wakiwa kikundi, kweli kweli wao hutoka wakiwa washindi. Kwa karibu miaka 90 tangu 1919, wao wamekataa kukubali alama ya hayawani-mwitu au kutegemea mfano wake kuwa tumaini pekee la binadamu kwa ajili ya amani. Wengi wao tayari wamevumilia kwa uaminifu mpaka kifo, na hawa, sasa wakiwa katika mbingu, pasipo shaka wanafuata kwa upendezi wa pekee wimbaji wa ndugu zao ambao wangali dunani.—Ufunuo 14:11-13.

7. Kinubi kilitumiwaje katika Israeli wa kale, na kuwapo kwa vinubi vya Mungu kwapasa kutuathirije sisi?

7 Washindi washikamanifu hawa wana vinubi vya Mungu. Katika hili, wao wako kama Walawi wa hekalu wa kale, ambao waliabudu Yehova kwa wimbo kwa kufuatanisha na vinubi. Baadhi yao walitoa unabii kwa kufuatanisha na kinubi. (1 Nyakati 15:16; 25:1-3) Zile sauti tamu za kinubi zilitia uzuri nyimbo za Israeli za shangwe na sala za sifa na za kutoa shukrani kwa Yehova. (1 Nyakati 13:8; Zaburi 33:2; 43:4; 57:7, 8) Katika nyakati za simanzi au utekwa, kinubi hakikusikiwa. (Zaburi 137:2) Kuwapo kwa vinubi vya Mungu katika njozi hii kwapasa kuchochee taraja letu la wimbo wa kuchachawa, wa ushindi wenye shangwe na sifa na utoaji-shukrani kwa Mungu wetu.a

8. Ni wimbo gani unaoimbwa, na maneno yao ni yapi?

8 Huo ndio anaoripoti Yohana: “Na wao wanaimba wimbo wa Musa mtumwa wa Mungu na wimbo wa Mwana-Kondoo, kusema: ‘Kubwa na za ajabu ni kazi zako, Yehova Mungu, Mweza Yote. Za uadilifu na za kweli ni njia zako, Mfalme wa umilele. Ni nani ambaye kwa kweli hatahofu wewe, Yehova, na kutukuza jina lako, kwa sababu wewe pekee ni mshikamanifu? Kwa maana mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako wewe, kwa sababu amri zako za uadilifu zimefanywa zidhihirike.”—Ufunuo 15:3, 4, NW.

9. Ni kwa nini kwa sehemu, wimbo huo huitwa “wimbo wa Musa”?

9 Washindi hawa huimba “wimbo wa Musa.” yaani, wimbo kama ule alioimba Musa katika hali zilizo kama hizo. Baada ya Waisraeli kuwa wameshuhudia tauni kumi katika Misri na uharibifu wa jeshi lote la Misri katika Bahari Nyekundu, Musa aliwaongoza katika wimbo kama huo wa ushindi wenye shangwe kwa sifa ya Yehova, akipiga mbiu hivi: “Yehova atatawala akiwa mfalme kwa wakati usio dhahiri, hata milele.” (Kutoka 15:1-19, NW) Inafaa kama nini kwamba waimbaji katika njozi ya Yohana, wakiwa wametoka wakiwa washindi wa hayawani-mwitu na wakiwa wanahusika katika kupiga mbiu ya tauni za mwisho saba, wamepaswa pia kuimbia “Mfalme wa umilele”!—1 Timotheo 1:17, NW.

10. Ni wimbo gani mwingine uliotungwa na Musa, na mstari wao wa mwisho unahusuje umati mkubwa wa leo?

10 Katika wimbo mwingine, uliotungwa Waisraeli walipokuwa wakijitayarishia kushinda Kanaani, Musa mwenye umri wa uzee aliambia taifa hilo: “Mimi nitajulisha wazi jina la Yehova. Nyinyi mhesabieni ukuu Mungu wetu!” Mstari wa mwisho wa wimbo huu uliwapa pia kitia-moyo wasio Waisraeli, na maneno ya Musa yaliyovuviwa yanafika chini moja kwa moja mpaka kwenye umati mkubwa wa leo: “Iweni na nderemo, enyi mataifa, pamoja na watu wake.” Na kwa nini wawe na nderemo? Kwa sababu sasa Yehova “atalipiza kisasi cha damu ya watumishi wake, na yeye atarudisha kisasi kwa mahasimu wake.” Utekelezo huu wa hukumu ya uadilifu utaleta shangwe kwa wale wote ambao huitibari katika Yehova.—Kumbukumbu 32:3, 43; Waroma 15:10-13; Ufunuo 7:9, NW.

11. Wimbo aliosikia Yohana unaendeleaje kuwa na utimizo?

11 Jinsi Musa mwenyewe angalishangilia kuwa katika siku ya Bwana sasa, akiimba pamoja na korasi ya kimbingu: “Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako wewe”! Wimbo huo ulio bora unaendelea kuwa na utimizo mzuri ajabu leo kama tuonavyo, si katika njozi tu bali ukiwa uhalisi ulio hai, mamilioni kutoka “mataifa” ambao wanakuja makundi makundi kwa shangwe kwenye tengenezo la Yehova la kidunia.—Ufunuo 1:10, NW.

12. Ni kwa nini wimbo wa washindi huitwa wimbo wa Mwana-Kondoo?

12 Hata hivyo, huu si wimbo wa Musa tu bali pia “wa Mwana-Kondoo.” Jinsi gani hivyo? Musa alikuwa nabii wa Mungu kwa Israeli, lakini Musa mwenyewe alitoa unabii kwamba Yehova angeinua nabii mwingine kama yeye. Huyu alithibitika kuwa Mwana-Kondoo, Yesu Kristo. Ingawa Musa alikuwa “mtumwa wa Mungu,” Yesu alikuwa Mwana wa Mungu, kwa kweli, Musa Mkubwa Zaidi. (Kumbukumbu 18:15-19; Matendo 3:22, 23; Waebrania 3:5, 6, NW) Kwa sababu hiyo, waimbaji huimba pia “wimbo wa Mwana-Kondoo.”

13. (a) Inakuwaje kwamba Yesu, ajapokuwa mkubwa zaidi ya Musa, yu kama yeye? (b) Sisi tunaweza kuunganaje na waimbaji hao?

13 Kama Musa, Yesu aliimba sifa za Mungu peupe na akatoa unabii kuhusu ushindi Wake juu ya maadui wake. (Mathayo 24:21, 22; 26:30; Luka 19:41-44) Yesu vilevile alitazamia wakati ambapo mataifa wangekuja na kusifu Yehova, na akiwa “Mwana-Kondoo wa Mungu” mwenye kujidhabihu, yeye alilaza chini uhai wake wa kibinadamu ili kuwezesha hilo. (Yohana 1:29; Ufunuo 7:9; linga Isaya 2:2-4; Zekaria 8:23.) Na kama vile Musa alivyokuja kuthamini jina la Mungu, Yehova, na kuhimidi jina hilo, vivyo hivyo Yesu alifanya jina la Mungu lidhihirike. (Kutoka 6:2, 3; Zaburi 90:1, 17; Yohana 17:6) Kwa kuwa Yehova ni mshikamanifu, ahadi zake tukufu ni hakika zitatimizwa. Basi, hakika sisi tuna umoja na waimbaji hawa washikamanifu, pamoja na Mwana-Kondoo, na pamoja na Musa, katika kuchangia maneno ya wimbo: “Ni nani kweli ambaye hatahofu wewe, Yehova, na kutukuza jina lako?”

Malaika Wenye Mabakuli

14. Ni nani ambao Yohana huona wakiibuka kutoka patakatifu, na wanapewa nini?

14 Inafaa tusikie wimbo wa hawa washindi wapakwa-mafuta. Kwa nini? Kwa sababu wametangaza peupe duniani hukumu zilizokuwa katika mabakuli yaliyokuwa yamejaa kasirani ya Mungu. Lakini kumiminwa kwa mabakuli haya kunahusu zaidi ya binadamu wa vivi hivi tu, kama Yohana aendeleavyo kuonyesha: “Na baada ya vitu hivi mimi nikaona, na patakatifu pa hema ya ushahidi palifunguliwa katika mbingu, na malaika saba wakiwa na tauni saba waliibuka kutoka patakatifu, wakiwa wamevaa kitani safi, nyangavu na wamefunga kifuani mishipi ya dhahabu. Na mmoja wa viumbe hai wanne akawapa malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyokuwa yamejaa kasirani ya Mungu, ambaye huishi milele na milele.”—Ufunuo 15:5-7, NW.

15. Kwa nini haishangazi kwamba malaika saba huibuka kutoka patakatifu?

15 Kwa habari ya hekalu la Israeli, ambalo lilikuwa na viwakilishi vya vitu vya kimbingu, ni kuhani mkuu pekee angeweza kuingia Patakatifu Zaidi Sana, panapoitwa hapa “patakatifu.” (Waebrania 9:3, 7, NW) Panawakilisha kuwapo kwa Yehova katika mbingu. Hata hivyo, katika mbingu yenyewe, si Kuhani Mkuu Yesu Kristo tu aliye na pendeleo la kuingia mbele za Yehova bali pia malaika hufanya hivyo. (Mathayo 18:10; Waebrania 9:24-26) Basi, haishangazi kwamba malaika saba wamepaswa kuonekana wakitoka katika patakatifu katika mbingu. Wao wana utume kutoka kwa Yehova Mungu mwenyewe: Mimineni mabakuli yanayojaa kasirani ya Mungu.—Ufunuo 16:1, NW.

16. (a) Ni nini kinachoonyesha kwamba hao malaika saba wanastahili sana kufanya kazi yao? (b) Ni nini kinachoonyesha kwamba wengine wanahusika katika hii kazi kubwa ya kumimina mabakuli ya ufananisho?

16 Malaika hawa wanastahili sana kufanya kazi hii. Wao wanavaa kitani safi, nyangavu, kuonyesha kwamba wao ni safi kiroho na ni watakatifu, waadilifu katika mwono wa Yehova. Pia, huvaa mishipi ya dhahabu. Kwa kawaida mishipi inatumiwa wakati mtu anapojifunga mwenyewe kwa ajili ya kazi inayopasa kutimizwa. (Walawi 8:7, 13; 1 Samweli 2:18; Luka 12:37; Yohana 13:4, 5) Kwa hiyo malaika wamejifunga mishipi kwa ajili ya kutimiza mgawo. Zaidi ya hayo, mishipi yao ni ya dhahabu. Katika tabenakulo ya kale, dhahabu ilitumiwa kuwakilisha vitu vya kimungu, vya kimbingu. (Waebrania 9:4, 11, 12) Hiyo inamaanisha kwamba malaika hawa wana utume wa utumishi wa kimungu, wenye thamani sana kuufanya. Wengine wanahusika vilevile katika kazi hii kubwa. Mmoja wa viumbe hai wanne anawapa mabakuli yenyewe. Pasipo shaka, huyu alikuwa kiumbe hai wa kwanza, ambaye alishabihi simba, kufananisha ujasiri na ushujaa usiotishika unaohitajiwa ili kupiga mbiu ya hukumu za Yehova.—Ufunuo 4:7, NW.

Yehova Katika Patakatifu Pake

17. Yohana hutuambia nini sasa juu ya patakatifu, na hilo hutukumbushaje sisi juu ya patakatifu katika Israeli wa kale?

17 Mwishowe, akimaliza sehemu hii ya njozi, Yohana anatuambia: “Na patakatifu pakajawa na moshi kwa sababu ya utukufu wa Mungu na kwa sababu ya nguvu zake, na hakuna mmoja ambaye aliweza kuingia ndani ya patakatifu mpaka tauni saba za malaika saba zilipokuwa zimekwisha.” (Ufunuo 15:8, NW) Kulikuwako vipindi katika historia ya Israeli wakati wingu lilifunika patakatifu halisi, na udhihirisho huu wa utukufu wa Yehova ulizuia makuhani kuingia humo. (1 Wafalme 8:10, 11; 2 Nyakati 5:13, 14; linga Isaya 6:4, 5.) Hizi zilikuwa nyakati Yehova alipokuwa anahangaikia sana matukio duniani.

18. Hao malaika saba watarudi lini kutoa ripoti kwa Yehova?

18 Vilevile, sasa Yehova anapendezwa sana na vitu vinavyotukia duniani pia. Yeye anataka malaika saba watimize mgawo wao. Ni wakati wa upeo wa hukumu, kama inavyoelezwa kwenye Zaburi 11:4-6, NW: “Yehova yumo katika hekalu takatifu lake. Yehova—kiti cha ufalme chake kimo katika mbingu. Macho yake mwenyewe huona, macho yake mwenyewe yenye kung’aa huchunguza wana wa binadamu. Yehova mwenyewe huchunguza mwadilifu na pia mwovu na yeyote mwenye kupenda jeuri nafsi Yake hakika huchukia. Yeye atanyesha chini juu ya waovu mitego, moto na salfa na upepo wenye kuunguza, kuwa aria ya kikombe chao.” Mpaka tauni saba hizi ziwe zimemiminwa juu ya waovu, malaika saba hawatarudi kwenye kuwapo kulikotukuka kwa Yehova.

19. (a) Ni amri gani inayotolewa sasa, na inatolewa na nani? (b) Ni lazima kumiminwa kwa mabakuli ya ufananisho kuwe kulianza lini?

19 Amri yenye kutia hofu yatokeza mngurumo: “Na mimi nikasikia sauti kubwa kutoka patakatifu ikisema kwa malaika saba: ‘Endeni na kumimina mabakuli saba ya kasirani ya Mungu ndani ya dunia.’” (Ufunuo 16:1, NW) Ni nani anayetoa amri hii? Ni lazima awe Yehova mwenyewe, kwa kuwa mng’aro wa utukufu na nguvu zake ulizuia mwingine yeyote kuingia patakatifu. Yehova alikuja kwenye hekalu lake la kiroho kwa ajili ya hukumu katika 1918. (Malaki 3:1-5) Basi, lazima iwe ilikuwa muda mfupi baada ya tarehe hiyo kwamba yeye akatoa hiyo amri ya kumimina “mabakuli ya kasirani ya Mungu.” Kwa kweli, hukumu zilizo katika mabakuli ya ufananisho zilianza kupigiwa mbiu kwa mkazo mkubwa katika 1922. Na leo ukubwa wa sauti za mbiu yao unazidi kuongezeka.

Mabakuli na Mipigo ya Tarumbeta

20. Mabakuli ya kasirani ya Mungu yanafunua na kuonya juu ya nini, nayo humiminwaje?

20 Mabakuli ya kasirani ya Mungu hufunua sura za mandhari ya ulimwengu kama Yehova anavyoziona na kuonya juu ya hukumu ambazo Yehova atatekeleza. Malaika humimina mabakuli kupitia uwakili wa kundi la Wakristo wapakwa-mafuta duniani, wanaoimba wimbo wa Musa na wa Mwana-Kondoo. Wanapokuwa wakipiga mbiu ya Ufalme kuwa habari njema, jamii ya Yohana imefunua kwa ujasiri yaliyomo ndani ya mabakuli haya ya kasirani. (Mathayo 24:14; Ufunuo 14:6, 7) Hivyo, kazi yao ya kuhubiri yenye sehemu mbili imekuwa yenye amani katika kupiga mbiu ya uhuru kwa aina ya binadamu lakini kama vita katika kuonya juu ya “siku ya kisasi upande wa Mungu wetu.”—Isaya 61:1, 2, NW.

21. Shabaha za mabakuli manne ya kwanza ya kasirani ya Mungu hulinganaje na yale ya mipigo minne ya kwanza ya tarumbeta, na hutofautiana katika nini?

21 Shabaha za mabakuli manne ya kwanza ya kasirani ya Mungu zinalingana na zile za mipigo minne ya kwanza ya tarumbeta, yaani, dunia, bahari, mito na vibubujiko vya maji, na machimbuko ya kimbingu ya nuru. (Ufunuo 8:1-12) Lakini mipigo ya tarumbeta ilitangaza tauni juu ya “theluthi moja,” hali sehemu nzima husumbuliwa na mmimino wa mabakuli ya kasirani ya Mungu. Hivyo, ingawa Jumuiya ya Wakristo, ikiwa ile “theluthi moja,” imepokea uangalifu wa kwanza wakati wa “siku ya Bwana,” hakuna sehemu moja ya mfumo wa Shetani iliyoepushwa isipate kusumbuliwa na jumbe za hukumu zenye kukera za Yehova na masikitiko zinayoleta.

22. Ile mipigo mitatu ya mwisho ya tarumbeta ilikuwa tofauti jinsi gani, na inahusianaje na mabakuli matatu ya mwisho ya kasirani ya Mungu?

22 Ile mipigo mitatu ya mwisho ya tarumbeta ilikuwa tofauti, kwa kuwa iliitwa ole. (Ufunuo 8:13; 9:12) Mbili za kwanza za hizo zilikuwa hasa zenye nzige na majeshi ya wapanda-farasi, hali wa tatu ulijulisha uzawa wa Ufalme wa Yehova. (Ufunuo 9:1-21; 11:15-19, NW) Kama tutakavyoona, mabakuli matatu ya mwisho ya hasira-kisasi yake pia huhusu baadhi ya pande hizi, yako tofauti kidogo na ole tatu. Acheni sasa tutoe uangalifu wa karibu sana kwa mafumbuo ya kidrama yanayotokana na kumiminwa kwa mabakuli ya kasirani ya Yehova.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa kupendeza, katika 1921 ile jamii ya Yohana ilitoa msaada wa funzo la Biblia The Harp of God, uliopata mwenezo wa nakala zaidi ya milioni tano kwa lugha zaidi ya 20. Ulisaidia kuleta ndani waimbaji zaidi wapakwa-mafuta.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki