Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • be uku. 33-uku. 38 fu. 4
  • Jinsi ya Kufanya Utafiti

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kufanya Utafiti
  • Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kutumia Biblia, Kitabu Chetu Kikuu cha Utafiti
  • Kujifunza Kutumia Vifaa Vingine vya Utafiti
  • Maktaba Nyingine za Kitheokrasi
  • Hifadhi Nakala Zako za Habari
  • Zungumza na Watu
  • Chunguza Matokeo
  • Kifaa Kipya cha Kufanyia Utafiti
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Kutimiza Huduma Yetu ya Ufalme kwa Msaada wa Index
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • ‘Kutafuta Maneno Yapendezayo, Yaliyo Sahihi’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Maktaba ya Jumba la Ufalme Inaweza Kutunufaisha Jinsi Gani?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
Pata Habari Zaidi
Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
be uku. 33-uku. 38 fu. 4

Jinsi ya Kufanya Utafiti

MFALME SOLOMONI ‘alitafakari, akatafuta-tafuta, akatunga mithali nyingi.’ Kwa nini? Kwa sababu alitaka kuandika “maneno ya kweli.” (Mhu. 12:9, 10) Luka ‘alifuatisha kwa uangalifu mambo yote tangu awali kwa usahihi’ ili asimulie kwa utaratibu matukio ya maisha ya Kristo. (Luka 1:3) Watumishi hao wa Mungu walifanya utafiti.

Utafiti ni nini? Utafiti ni kuchunguza kwa makini habari inayohusu jambo fulani. Unatia ndani kusoma na kufuata kanuni za kujifunza. Pia unaweza kutia ndani kuhoji watu.

Tufanyie utafiti mambo gani? Ifuatayo ni mifano michache. Unapokuwa na funzo la binafsi au unaposoma Biblia, huenda ukapata mambo yanayotokeza maswali muhimu. Labda ungependa kupata habari fulani ili ujibu swali la mtu ambaye ulimhubiria. Au huenda umepewa mgawo wa kutoa hotuba.

Ebu fikiria kuhusu mgawo huo wa kutoa hotuba. Huenda ikaonekana kwamba hotuba hiyo ina mambo ya kawaida tu. Unaweza kufanyaje ili hotuba hiyo ifae hali za kwenu? Uiboreshe kwa kufanya utafiti. Ukitumia habari chache zinazohusu idadi katika hotuba au ukitumia mfano mzuri unaohusu wasikilizaji, jambo ambalo huenda lilionekana kama ni la kawaida tu linakuwa lenye kufundisha, na hata lenye kuchochea moyo. Habari zilizo katika hotuba yako huenda zilichapishwa kwa manufaa ya wasomaji ulimwenguni pote, lakini inatakikana uonyeshe faida ya hotuba hiyo kwa kuifafanua, kutumia mifano, na kwa kuonyesha jinsi kutaniko au mtu mmoja-mmoja anavyoweza kufuata mashauri yake maishani. Ufanyeje?

Kabla ya kuanza kufanya utafiti, uwafikirie wasikilizaji. Tayari wamejua nini? Wanahitaji kujua nini? Na kusudi lako ni nini? Je, ni kufafanua habari hiyo? ni kusadikisha? ni kukanusha? au ni kuchochea? Kufafanua kunamaanisha kuandaa habari zaidi ili jambo lieleweke wazi. Ingawa huenda mambo makuu yanaeleweka, inafaa kuonyesha wasikilizaji wakati wanapoweza kutumia habari hiyo au jinsi wanavyoweza kutumia habari hiyo. Kusadikisha kunamaanisha kutoa uthibitisho unaoonyesha kwa nini jambo tunalosema ni kweli. Ili tuweze kukanusha jambo, tunahitaji kujua kabisa pande zote mbili za suala hilo pamoja na kuchunguza kwa makini uthibitisho unaotumiwa. Bila shaka, hatutoi tu sababu zenye nguvu bali pia sisi hujaribu kutoa sababu kwa njia ya fadhili. Kuchochea kunahusu kufikia moyo. Kunamaanisha kuhimiza wasikilizaji na kufanya watamani kufuata mashauri ya hotuba yako. Mifano ya watu halisi ambao wamechukua hatua hiyo, hata wajapokabili magumu, inaweza kusaidia kufikia moyo.

Je, sasa u tayari kuanza? La, bado. Fikiria kiasi cha habari unachohitaji. Huenda ikawa muhimu kufikiria wakati. Kama utatoa hotuba hiyo mbele ya wengine, utaitoa kwa muda gani? Dakika tano? Dakika 45? Je, umewekewa wakati kama ilivyo na mikutano ya kutaniko au hujawekewa wakati, kama ilivyo na funzo la Biblia au ziara ya uchungaji?

Hatimaye, una vifaa gani vya kufanyia utafiti? Kwa kuongezea vifaa ulivyo navyo nyumbani, je kuna vifaa zaidi kwenye maktaba ya Jumba lenu la Ufalme? Je, ndugu ambao wamekuwa wakimtumikia Yehova kwa miaka mingi wanaweza kukuruhusu utumie vifaa vyao vya kufanyia utafiti? Je, kuna maktaba ya umma huko kwenu ambayo ina vitabu vya marejeo ambavyo vinaweza kutumiwa?

Kutumia Biblia, Kitabu Chetu Kikuu cha Utafiti

Ikiwa utafiti unaofanya unahusu maana ya andiko fulani, anza na Biblia yenyewe.

Chunguza Muktadha. Jiulize: ‘Andiko hili lilielekezewa nani? Mistari inayotangulia na inayofuata andiko hilo inaonyesha nini kuhusu sababu inayotajwa au inaonyesha nini kuhusu watu wanaotajwa?’ Mara nyingi mambo kama hayo yanaweza kutusaidia kuelewa andiko fulani, na pia yakitumiwa yanaweza kufanya hotuba yako ipendeze zaidi.

Kwa mfano, mara nyingi Waebrania 4:12 hunukuliwa kuonyesha uwezo wa Neno la Mungu wa kugusa mioyo na kubadili maisha. Muktadha unatusaidia kufahamu jambo hilo zaidi. Unasimulia mambo ambayo Waisraeli walipitia wakati wa ile miaka 40 wakiwa jangwani kabla hawajaingia katika nchi ambayo Yehova aliahidi Abrahamu. (Ebr. 3:7–4:13) “Neno la Mungu,” yaani ahadi yake ya kuwaleta mahali pa pumziko kulingana na agano lake pamoja na Abrahamu, halikuwa limeshindwa; bado lilielekea kutimizwa. Waisraeli walikuwa na sababu nzuri za kuliamini. Lakini, walirudia-rudia kuonyesha ukosefu wa imani kwa Yehova alipokuwa akiwatoa Misri na kuwaongoza hadi Mlima Sinai na kuelekea Nchi ya Ahadi. Basi, itikio lao kwa jinsi Mungu alivyotimiza neno lake, lilidhihirisha yaliyokuwa mioyoni mwao. Katika siku zetu vilevile, ahadi ya neno la Mungu huonyesha yaliyomo mioyoni mwa wanadamu.

Chunguza Marejeo. Baadhi ya Biblia zina marejeo. Je, yako inayo? Ikiwa inayo, hayo yanaweza kukusaidia. Ebu ona mfano mmoja katika New World Translation of the Holy Scriptures. Andiko la 1 Petro 3:6 linaonyesha kwamba Sara ni mfano ambao wake Wakristo wanastahili kuiga. Marejeo kwenye Mwanzo 18:12 yanakazia jambo hilo kwa kufunua kwamba Sara alimwita Abrahamu bwana “moyoni mwake.” Kwa hiyo, alitii kutoka moyoni. Mbali na ufahamu kama huo, marejeo yanaweza pia kukuelekeza kwenye maandiko ambayo yanaonyesha utimizo wa unabii wa Biblia au utimizo wa jambo lililofananishwa na agano la Sheria. Lakini, marejeo fulani hayakusudiwi kutoa maelezo kama hayo. Huenda ikawa yanaonyesha tu mawazo yanayolingana na habari hiyo, au maelezo ya maisha ya mtu au habari kuhusu mahali.

Tumia Itifaki ya Biblia. Itifaki ya Biblia ni orodha ya maneno ambayo yametumiwa katika Biblia. Orodha hiyo imepangwa katika alfabeti. Inaweza kukusaidia kupata maandiko yanayohusiana na habari unayofanyia utafiti. Unapoyachunguza, utajifunza mambo mengine yenye faida. Utaona uthibitisho wa kwamba kuna “kiolezo” cha kweli katika Neno la Mungu. (2 Tim. 1:13) Biblia ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ina orodha ya msingi ya “Maneno ya Biblia Yaliyofaharishwa.” Itifaki inayoitwa Comprehensive Concordance ina mambo mengi sana. Ikiwa inapatikana katika lugha unayoelewa, itakuonyesha maneno yote makuu yanayotumiwa katika Biblia.

Kujifunza Kutumia Vifaa Vingine vya Utafiti

Sanduku lililo kwenye ukurasa wa 33 lina orodha ya vifaa vingine vya kufanyia utafiti ambavyo vimeandaliwa na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45-47) Vifaa vingi vya kufanyia utafiti vina yaliyomo, na vingi vina faharisi upande wa nyuma ambayo imetayarishwa ikusaidie kupata habari fulani unayotaka. Mwishoni mwa kila mwaka, faharisi za habari, ambazo ni orodha za habari za mwaka mzima, huchapishwa katika Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

Kufahamu aina ya habari inayoandaliwa katika vichapo hivi vinavyosaidia kujifunza Biblia kunaweza kuharakisha utafiti. Kwa mfano, tuseme unataka kujua jambo kuhusu unabii, fundisho, mwenendo wa Kikristo, au namna ya kutumia kanuni za Biblia. Inaelekea Mnara wa Mlinzi litakuwa na habari unayotafuta. Amkeni! hushughulika na matukio ya sasa, matatizo ya wakati huu, dini, sayansi, na watu wa nchi mbalimbali. Maelezo ya kila tukio katika vitabu vya Injili na jinsi matukio hayo yalivyofuatana yanapatikana katika kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Mazungumzo ya mstari kwa mstari ya vitabu vizima vya Biblia yanapatikana katika vichapo kama Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, Sikiliza Unabii wa Danieli!, na mabuku mawili ya Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote. Katika Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko, mna majibu yenye kuridhisha ya mamia ya maswali ya Biblia ambayo kwa kawaida huulizwa katika utumishi wa shambani. Ili ufahamu zaidi dini nyingine mbalimbali, mafundisho yao, na historia zao, ona kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Kitabu Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu kina masimulizi ya kindani ya historia ya kisasa ya Mashahidi wa Yehova. Tazama Yearbook of Jehovah’s Witnesses cha karibuni zaidi uone ripoti ya maendeleo ya wakati huu ya kazi ya kuhubiri habari njema duniani kote. Kichapo Insight on the Scriptures kina habari za Biblia na ramani. Kitabu hiki ni bora sana ikiwa unahitaji kujua habari za watu, mahali mbalimbali, vitu, lugha, au matukio ya historia yanayohusiana na Biblia.

“Watch Tower Publications Index.” Hii Index, inayochapishwa katika zaidi ya lugha 20, itakusaidia kupata habari mbalimbali zinazopatikana katika vichapo vyetu. Ina faharisi ya habari na faharisi ya maandiko. Ili utumie faharisi ya habari, tafuta neno linalohusika na habari unayochunguza. Unapotaka kutumia faharisi ya maandiko, tafuta andiko unalotaka kuelewa vizuri kwenye orodha ya maandiko. Ikiwa jambo fulani limechapishwa katika lugha yenu kuhusu jambo hilo au andiko hilo katika miaka inayopatikana kwenye Index, utapata orodha ya marejeo ambayo unaweza kuchunguza. Ukurasa mmoja wa mbele katika Index una ufupisho wa majina ya vichapo. (Kwa mfano, w99-SW 3/1 15 inamaanisha Mnara wa Mlinzi la Machi 1, 1999, ukurasa wa 15.) Vichwa vikuu kama “Field Ministry Experiences” (“Mambo Yaliyoonwa Katika Huduma ya Shambani”) na “Life Stories of Jehovah’s Witnesses,” (“Masimulizi ya Maisha ya Mashahidi wa Yehova”) vinaweza kusaidia kutayarisha hotuba za kutaniko zenye kuchochea.

Kwa kuwa unaweza kuzama sana katika utafiti, uwe mwangalifu usikengeushwe. Kumbuka kusudi lako unapotafuta habari unayohitaji. Ikiwa Index imeonyesha kichapo fulani, fungua ukurasa uliotajwa, utumie vichwa vidogo na sentensi za kwanza za mafungu kukuelekeza kwenye habari unayotaka. Kama unachunguza maana ya andiko fulani la Biblia, kwanza ulitafute kwenye ukurasa ambao umeonyeshwa. Kisha chunguza muktadha wa andiko hilo.

“Watchtower Library” Kwenye CD-ROM. Kama una kompyuta, unaweza kufaidika kutumia Watchtower Library kwenye CD-ROM, ambayo ina vichapo vyetu vingi sana. Programu rahisi ya kutafuta habari inakuwezesha kutafuta neno moja, fungu la maneno, au andiko katika vichapo vyovyote vile vinavyopatikana katika Watchtower Library. Hata kama kifaa hiki cha utafiti hakipatikani katika lugha yenu, huenda ukaweza kukitumia katika lugha moja kubwa ya kimataifa ambayo unafahamu.

Maktaba Nyingine za Kitheokrasi

Paulo alipomwandikia kijana Timotheo barua ya pili iliyopuliziwa, alimwomba amletee kule Roma “hati-kunjo, hasa zile hati za ngozi.” (2 Tim. 4:13) Paulo alithamini maandishi fulani akayahifadhi. Wewe pia unaweza kufanya hivyo. Je, unahifadhi Mnara wa Mlinzi, Amkeni!, na Huduma Yetu ya Ufalme hata baada ya kuvitumia kwenye mikutano ya kutaniko? Ikiwa ndivyo, unaweza kuvitumia kufanya utafiti, pamoja na vichapo vyako vingine vya Kikristo. Makutaniko mengi yana vichapo vya kitheokrasi kwenye maktaba ya Jumba la Ufalme. Vichapo hivyo hufaidi wote kutanikoni, wanapovitumia wakiwa kwenye Jumba la Ufalme.

Hifadhi Nakala Zako za Habari

Uwe macho kuona mambo yanayopendeza ambayo unaweza kutumia unapotoa hotuba na kufundisha. Ukipata gazetini tukio fulani, habari fulani zinazohusu idadi, au mfano ambao unaweza kutumia katika huduma yako, uikate habari hiyo au uinakili. Tia ndani tarehe, jina la gazeti hilo, na labda jina la mwandishi au mchapishaji. Kwenye mikutano ya kutaniko, andika mifano na mambo ambayo yanaweza kukusaidia kuwaelezea wengine kweli. Je, umepata kufikiria mfano mzuri lakini ukakosa nafasi kuutumia wakati huo? Andika mfano huo na uuweke. Baada ya kuwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kwa muda fulani utakuwa umetayarisha hotuba nyingi. Badala ya kutupa maandishi yako ya hotuba hizo, yaweke. Utafiti ambao umefanya unaweza kukufaidi baadaye.

Zungumza na Watu

Watu wanajua mambo mengi. Luka alipokuwa akikusanya habari za masimulizi yake ya Injili, inaelekea alikusanya habari nyingi kwa kuwahoji watu waliojionea mambo hayo. (Luka 1:1-4) Labda Mkristo mwenzako anaweza kukuelewesha jambo fulani ambalo umekuwa ukijaribu kulifanyia utafiti. Kulingana na Waefeso 4:8, 11-16, Kristo hutumia “zawadi zikiwa wanadamu” ili kutusaidia kukua “katika ujuzi sahihi wa Mwana wa Mungu.” Unaweza kupata mawazo mazuri kwa kuwahoji wale ambao wamemtumikia Mungu kwa muda mrefu. Mazungumzo pamoja na watu pia yanaweza kufunua fikira zao, na jambo hilo linaweza kukusaidia kutayarisha habari ambayo kwa kweli inasaidia.

Chunguza Matokeo

Baada ya kuvuna ngano, mbegu zake huondolewa kwenye makapi. Ndivyo ilivyo na matokeo ya utafiti wako. Kabla ya kuyatumia, unahitaji kutenganisha mambo yenye thamani na yale ya ziada.

Kama utatumia habari hiyo katika hotuba, jiulize: ‘Je, jambo ambalo ninataka kutumia litasaidia kuboresha habari ninayozungumzia? Au, hata kama ni jambo lenye kupendeza, je, linaenda kando na habari ambayo napaswa kuzungumzia?’ Kama unafikiria kutumia matukio ya sasa au habari inayobadilika-badilika ya kisayansi au tiba, hakikisha kwamba habari hiyo ni ya karibuni. Kumbuka pia kwamba baadhi ya mambo yanayopatikana katika vichapo vyetu vya zamani huenda yamerekebishwa, basi chunguza habari ya karibuni zaidi iliyochapishwa kuhusu jambo hilo.

Unahitaji kujihadhari sana ukiamua kukusanya habari kwenye vichapo vya kilimwengu. Usisahau kamwe kwamba Neno la Mungu ndiyo kweli. (Yn. 17:17) Yesu ana fungu muhimu katika utimizo wa kusudi la Mungu. Kwa hiyo, andiko la Wakolosai 2:3 linasema: “Zenye kusitiriwa kwa uangalifu ndani yake ni hazina zote za hekima na za ujuzi.” Chunguza matokeo ya utafiti wako ukikumbuka jambo hilo. Jiulize hivi kuhusu utafiti uliofanya katika vichapo vya kilimwengu: ‘Je, habari hii imetiliwa chumvi, inakisia-kisia tu mambo, au haina mwelekeo? Je, iliandikwa kwa nia ya kudhuru au kwa kuchochewa na tamaa ya pesa? Je, vichapo vingine mashuhuri vinakubaliana nayo? Zaidi ya yote, je, inapatana na kweli ya Biblia?’

Andiko la Mithali 2:1-5 linatutia moyo kuendelea kutafuta ujuzi, busara, na ufahamu kama ‘fedha na hazina iliyositirika.’ Hilo ladokeza bidii na faida tele. Ili kufanya utafiti unahitaji bidii, lakini ukiufanya utajua maoni ya Mungu juu ya mambo mbalimbali, utasahihisha maoni yenye makosa, na kuishika kweli kabisa. Pia hotuba zako zitakuwa nzuri na changamfu, na utafurahi kuzitoa na wasikilizaji watapendezwa nazo.

UNA VIFAA GANI VYA KUFANYIA UTAFITI KATI YA HIVI VILIVYOPO HAPA?

  • New World Translation of the Holy Scriptures

  • Comprehensive Concordance

  • Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

  • Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko

  • Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu

  • Insight on the Scriptures

  • Watch Tower Publications Index

  • Watchtower Library kwenye CD-ROM

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki