Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 15 uku. 42-uku. 43 fu. 3
  • Yehova Hakumsahau Yosefu Kamwe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Hakumsahau Yosefu Kamwe
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • “Je, Mimi Niko Mahali pa Mungu?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Njaa Yenye Kuleta Kifo Katika Wakati wa Utele
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Kuhifadi Uhai Katika Wakati wa Njaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Je! Wewe U Mwenye Rehema Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 15 uku. 42-uku. 43 fu. 3
Yosefu anamwelezea Farao maana ya ndoto zake

SOMO LA 15

Yehova Hakumsahau Yosefu Kamwe

Yosefu alipokuwa gerezani, Farao mfalme wa Misri aliota ndoto ambazo hakuna mtu aliyeweza kueleza maana yake. Mtumishi mmoja alimwambia Farao kwamba Yosefu angeweza kumweleza maana ya ndoto zake. Mara moja, Farao akaagiza Yosefu aletwe.

Farao akamwuliza hivi: ‘Unaweza kunieleza maana ya ndoto zangu?’ Yosefu akamwambia Farao hivi: ‘Nchi ya Misri itakuwa na chakula kingi kwa miaka saba, lakini miaka saba itakayofuata kutakuwa na njaa. Chagua mtu mwenye hekima ahifadhi chakula ili watu wako wasife njaa.’ Farao akajibu hivi: ‘Ninakuchagua wewe! Utakuwa mtu wa pili kwa mamlaka nchini Misri!’ Yosefu alijuaje maana ya ndoto za Farao? Yehova alimsaidia Yosefu.

Yosefu anawaagiza watu wahifadhi chakula

Kwa miaka saba iliyofuata, Yosefu alihifadhi chakula. Na kama ambavyo Yosefu alikuwa amesema, kukawa na njaa duniani pote. Watu walitoka maeneo mbalimbali kuja kununua chakula kutoka kwa Yosefu. Yakobo, baba ya Yosefu, alisikia kwamba kuna chakula nchini Misri, kwa hiyo akawatuma wana wake kumi waende huko kununua chakula.

Wana wa Yakobo walienda kwa Yosefu, naye akawatambua mara moja. Lakini wao hawakumtambua Yosefu. Wakamwinamia kama alivyokuwa ameota akiwa mdogo. Yosefu alitaka kujua ikiwa kaka zake bado walikuwa na chuki. Kwa hiyo, akawaambia hivi: ‘Ninyi ni wapelelezi. Mnataka kuchunguza udhaifu wa nchi yetu.’ Wakasema, ‘Hapana! Tulizaliwa kaka 12 nchini Kanaani. Ndugu yetu mmoja amekufa, na yule mdogo zaidi yuko na baba yetu.’ Kisha Yosefu akawaambia hivi: ‘Nileteeni ndugu yenu mdogo, nami nitawaamini.’ Kwa hiyo wakarudi nyumbani kwao.

Chakula kilipoisha, Yakobo aliwatuma tena wana wake waende Misri. Pindi hii, walisafiri pamoja na Benjamini, ndugu yao mdogo. Ili kuwajaribu ndugu zake, Yosefu alificha kikombe cha fedha kwenye mfuko wa Benjamini na kusema kwamba walikuwa wamekiiba. Watumishi wa Yosefu walipopata kikombe hicho kwenye mfuko wa Benjamini, ndugu zake walishtuka. Wakamwomba Yosefu awaadhibu wao badala ya Benjamini.

Sasa Yosefu akatambua kwamba ndugu zake walikuwa wamebadilika. Yosefu akashindwa kujizuia. Akabubujikwa na machozi na kusema hivi: ‘Mimi ni ndugu yenu, Yosefu. Je, baba yangu yuko hai?’ Ndugu zake walishangaa sana. Akawaambia hivi: ‘Msihuzunike kwa sababu ya kile mlichonifanyia. Mungu alinituma huku ili niwaokoe. Sasa harakisheni mwende mkamlete baba yangu.’

Wakarudi nyumbani kumwambia baba yao habari hizo njema, na baadaye wakamleta Misri. Sasa Yosefu na baba yake wakakutana tena baada ya miaka mingi.

Yosefu akimsalimu baba yake, Yakobo

“Msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe makosa yenu.”—Mathayo 6:15

Maswali: Yehova alimsaidiaje Yosefu? Yosefu alionyeshaje kwamba alikuwa amewasamehe kaka zake?

Mwanzo 40:1–45:28; 46:1-7, 26-34; Zaburi 105:17-19; Matendo 7:9-15

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki