Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 31 uku. 78
  • Yoshua na Wagibeoni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yoshua na Wagibeoni
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Wagibeoni Wenye Hekima
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Jua Linasimama Tu
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • “Yehova Mungu Wetu Ndiye Sisi Tutatumikia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Yoshua na Akusaidie Wewe Umtumikie Yehova kwa Uhodari!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 31 uku. 78
Wagibeoni walimwendea Yoshua na jeshi lake wakiwa wamevalia mavazi yaliyochakaa

SOMO LA 31

Yoshua na Wagibeoni

Habari kuhusu kuanguka kwa Yeriko zilienea katika mataifa mengine ya Kanaani. Wafalme wao wakaamua kuungana ili wapigane na Waisraeli. Lakini Wagibeoni wakaamua kufanya jambo tofauti. Wakiwa wamevalia mavazi yaliyochakaa wakamwendea Yoshua na kusema hivi: ‘Tumetoka nchi ya mbali sana. Tumesikia kumhusu Yehova na yote aliyowafanyia mlipokuwa Misri na Moabu. Tunaomba mtuahidi kwamba hamtatushambulia, nasi tutakuwa watumishi wenu.’

Yoshua aliwaamini na akawaahidi kwamba hatawashambulia. Siku tatu baadaye, akagundua kwamba hawakuwa wametoka nchi ya mbali. Walikuwa wakaaji wa nchi ya Kanaani. Yoshua akawauliza Wagibeoni hivi: ‘Kwa nini mlitudanganya?’ Wakamjibu: ‘Tuliogopa! Tunajua kwamba Yehova Mungu wenu anawapigania. Tafadhali msituue.’ Yoshua akatimiza ahadi yake na kuwaacha waendelee kuishi.

Baada ya muda mfupi, wafalme watano Wakanaani na majeshi yao wakatishia kuwashambulia Wagibeoni. Yoshua na jeshi lake wakatembea usiku mzima ili kuwaokoa Wagibeoni. Vita vikaanza mapema asubuhi siku iliyofuata. Wakanaani wakaanza kukimbia kuelekea pande zote. Kila mahali walipokimbilia Yehova aliangusha mvua ya mawe makubwa juu yao. Kisha Yoshua akamwomba Yehova alifanye jua lisimame tuli. Kwa nini Yoshua amwombe Yehova afanye hivyo wakati jua halikuwahi kusimama tuli kabla ya hapo? Kwa sababu Yoshua alimwamini Yehova. Jua halikutua kwa siku nzima hadi Waisraeli walipowashinda wafalme Wakanaani na majeshi yao.

Yoshua anatazama juu mbinguni na kumwomba Yehova afanye jua lisimame tuli

“‘Ndiyo’ yenu imaanishe ndiyo, na ‘Siyo’ yenu, siyo, kwa maana linalozidi hayo linatoka kwa yule mwovu.”​—Mathayo 5:37

Maswali: Wagibeoni walifanya nini ili kujilinda? Yehova aliwasaidiaje Waisraeli?

Yoshua 9:1–10:15

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki