Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 78 uku. 184-uku. 185 fu. 1
  • Yesu Anahubiri Ujumbe wa Ufalme

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Anahubiri Ujumbe wa Ufalme
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • “Habari Njema Lazima Zihubiriwe Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Wale Ambao Wakawa Wanafunzi wa Yesu
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • “Nifuateni, Nami Nitawafanya Kuwa Wavuvi Watu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • “Nendeni Mkafanye Wanafunzi”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 78 uku. 184-uku. 185 fu. 1
Yesu na mwanafunzi wakihubiri

SOMO LA 78

Yesu Anahubiri Ujumbe wa Ufalme

Muda mfupi baada ya ubatizo wake, Yesu alianza kuhubiri: ‘Ufalme wa Mungu umekaribia.’ Wanafunzi walimfuata alipokuwa akisafiri katika eneo la Galilaya na Yudea. Yesu aliporudi katika eneo la nyumbani la Nazareti, alienda kwenye sinagogi, akafungua kitabu cha kukunjwa cha Isaya, na kusoma kwa sauti: ‘Yehova amenipa roho takatifu ili nihubiri habari njema.’ Maneno hayo yalimaanisha nini? Yalimaanisha kwamba ingawa watu walitaka kumwona Yesu akifanya miujiza, sababu kuu ya kupokea roho takatifu ilikuwa ni kuhubiri habari njema. Aliwaambia hivi wasikilizaji wake: ‘Leo unabii huu umetimizwa.’

Kisha Yesu akaenda kwenye Bahari ya Galilaya, ambapo alikutana na wanafunzi wake wanne, ambao walikuwa wavuvi. Yesu akawaambia hivi: ‘Nifuateni, nami nitawafanya muwe wavuvi wa watu.’ Wanafunzi hao walikuwa Petro, Andrea, Yakobo, na Yohana. Mara moja wakaacha biashara yao ya uvuvi na kumfuata. Walienda katika sehemu zote za Galilaya, wakihubiri kuhusu Ufalme wa Yehova. Walihubiri katika masinagogi, sokoni, na barabarani. Umati mkubwa uliwafuata kila mahali walipoenda. Habari kumhusu Yesu zilienea kila mahali, hata kufikia Siria.

Baada ya muda, Yesu aliwapa baadhi ya wafuasi wake nguvu za kuponya watu na kufukuza roho waovu. Wengine waliandamana naye alipokuwa akihubiri kutoka jiji hadi jiji na kutoka kijiji hadi kijiji. Wanawake fulani waaminifu, kutia ndani Maria Magdalene, Yoana, Susana, na wengine walikuwa wakimhudumia Yesu na wafuasi wake.

Baada ya kuwazoeza wanafunzi wake, Yesu aliwatuma wakahubiri. Walipokuwa wakisafiri kotekote katika Galilaya, wengine wengi wakawa wanafunzi na kubatizwa. Watu wengi sana walitaka kuwa wanafunzi hivi kwamba Yesu akawalinganisha na shamba ambalo liko tayari kuvunwa. Alisema hivi: ‘Mwombeni Yehova awatume wafanyakazi wengi zaidi katika mavuno.’ Baadaye alichagua wanafunzi wengine 70 na akawatuma wakiwa wawili-wawili wakahubiri katika maeneo yote kuzunguka Yudea. Waliwafundisha watu wote kuhusu Ufalme. Wanafunzi waliporudi, walikuwa na hamu sana ya kumwambia Yesu kilichotukia. Hakuna kitu ambacho Ibilisi angefanya ili kuzuia kazi ya kuhubiri.

Yesu alihakikisha kwamba wanafunzi wake wangeendelea kufanya kazi hiyo muhimu baada ya yeye kurudi mbinguni. Aliwaambia hivi: ‘Hubirini habari njema duniani pote. Wafundisheni watu Neno la Mungu na kuwabatiza.’

“Ni lazima pia nitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu katika majiji mengine, kwa sababu nilitumwa kufanya hivyo.”​—Luka 4:43

Maswali: Ni kazi gani ambayo Yesu aliwapa wanafunzi wake? Wanafunzi wake walihisije kuhusu kazi yao?

Mathayo 4:17-25; 9:35-38; 28:19, 20; Marko 1:14-20; Luka 4:14-21; 8:1-3; 10:1-22

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki