Dhambi
Dhambi ni nini, na kwa nini inatuathiri sisi sote?
Biblia inatuhakikishiaje kwamba tunaweza kushinda mielekeo yetu ya dhambi?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
2Sa 11:2-5, 14, 15, 26, 27; 12:1-13 —Mfalme Daudi anatenda dhambi nzito sana, anapata nidhamu kali, na anajitahidi sana kurekebisha njia zake
Ro 7:15-24—Mtume Paulo, ambaye ni mfano bora wa mtu mwenye imani yenye nguvu na anayemtumikia Mungu kwa bidii, anaeleza jinsi anavyopambana na mwelekeo wake mwenyewe wa dhambi
Kutojua na kupotoshwa kumewaongozaje watu wengi kwenye dhambi?
Mdo 3:17; 17:29, 30; 1Ti 1:13; 1Pe 1:14
Tazama pia Hes 15:27-29
Kwa nini zoea la kufanya dhambi kimakusudi ni jambo zito sana?
Ebr 10:26, 27; 1Yo 3:4, 8, 9
Tazama pia Hes 15:30; Ro 1:28-32; 1Ti 5:20
Huenda Shetani akatumia nini ili kuwashawishi watumishi wa Mungu watende dhambi?
Met 1:10, 11, 15; Mt 5:28; Yak 1:14, 15
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 3:1-6—Akizungumza kupitia nyoka, Shetani anamjaribu Hawa kwa kuchochea tamaa mbaya ya ubinafsi na kudhoofisha uhakika wake katika Yehova
Met 7:6-10, 21-23—Mfalme Sulemani anaeleza jinsi mwanamume kijana asiye na busara anavyoshawishiwa na mwanamke mwenye maadili mapotovu
Tunawezaje kupinga vishawishi vya Shetani?
Efe 4:27; 6:10-18; Yak 4:7, 8
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Met 5:1-14—Kama baba anavyozungumza na mwana wake, Mfalme Sulemani anatoa ushauri ulioongozwa na roho kuhusu kwa nini na kwa njia gani tunaweza kuepuka kishawishi cha kufanya uasherati
Mt 4:1-11—Yesu anatuwekea kielelezo kikamilifu cha kupinga vishawishi vya Shetani vyenye ujanja kwa kutegemea Neno la Mungu
Baadhi ya mifano ya dhambi nzito ambazo Mkristo anapaswa kuepuka
Tazama “Mazoea Yasiyofaa”
Kuungama dhambi
Kwa nini hatupaswi kujaribu kuficha dhambi zetu?
Tunapaswa kuungama dhambi zetu zote kwa nani?
Ni nani anayetenda kama “msaidizi” kwa kututetea mbele za Yehova?
Je, mtenda dhambi anaweza kuonyesha toba kupitia matendo yake?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Kut 22:1-12—Chini ya Sheria ya Musa, mwizi anapaswa kuwalipa wale aliowaibia
Lu 19:8, 9—Zakayo, mkuu wa wakusanya kodi, anaonyesha toba kwa kubadili njia zake na kwa kuwarudishia pesa wale aliowadhulumu
Tazama pia “Toba”
Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika na msamaha wa Yehova?
Tazama “Kusamehe”
Yehova ameandaa mpango gani unaotoa msaada na kulilinda kutaniko mtu anapofanya dhambi nzito?
Tazama pia Mdo 20:28; Gal 6:1
Dhambi nzito inaweza kuwaathirije wengine katika familia au kutanikoni?
Tazama pia Kum 29:18
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Yos 7:1-13, 20-26—Akani anawaletea msiba Waisraeli wote kwa kufanya dhambi nzito na kujaribu kuificha
Yon 1:1-16—Kwa sababu anamwasi Yehova, nabii Yona anahatarisha uhai wa watu walio katika meli pamoja naye
1Ko 5:1-7—Mtume Paulo anafunua kisa cha dhambi nzito huko Korintho, inayolidhuru kutaniko lote
Kwa nini woga wa kutiwa nidhamu haupaswi kamwe kutuzuia kutafuta msaada wa wazee?
Kwa nini tunapaswa kukubali msamaha wa Mungu badala ya kuendelea kuhuzunika kwa sababu ya makosa tuliyofanya wakati uliopita?
Tazama “Kusamehe”
Ikiwa tunajua kwamba mtu fulani amefanya dhambi nzito, kwa nini tunapaswa kuhakikisha kwamba mtenda dhambi anaenda kuwajulisha wazee wa kutaniko?
Simulizi la Biblia linalohusika:
Kum 13:6-9; 21:18-20—Sheria ya Musa inamtaka mtu atoe ripoti ya dhambi nzito iliyofanywa hata na mtu wa familia au mpendwa wake