Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 4/1 kur. 166-168
  • Mifano ya Kupamba au ya Ibada ya Sanamu—Jambo Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mifano ya Kupamba au ya Ibada ya Sanamu—Jambo Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Kujilinda na Ibada ya Sanamu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Je, Tumwabudu Mungu Kupitia Sanamu?
    Amkeni!—2008
  • Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawatumii Sanamu Katika Ibada?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Maoni ya Kikristo Juu ya Mifano
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 4/1 kur. 166-168

Mifano ya Kupamba au ya Ibada ya Sanamu​—Jambo Gani?

WATU wanaotaka ukubali wa kimungu wana lazima ya kujua kama mifano fulani ni ya ibada ya sanamu au ya kupamba tu. Yeye asiyeweza kufahamu kile ambacho ni sanamu, angekuwa na ugumu kutii amri za Biblia: “Ikimbieni ibada ya sanamu.” “Jilindeni nafsi zenu na sanamu.” (1 Kor. 10:14; 1 Yohana 5:21) Hili lingekuwa jambo lenye msiba kwa mtu anayetiwa ndani. Sababu gani? Kwa kuwa waabudu sanamu wanatajwa waziwazi kati ya wale ambao hawataurithi ufalme wa Mungu.​—1 Kor. 6:9, 10.

Ni nini, basi, kinachofanya kitu kiwe mfano wa ibada? Je! sanamu, picha, au kitu kingine kama hicho, ni mfano wa ibada kwa sababu kiumbe au kitu kinachofananishwa wakati fulani kilikuwa chombo cha ibada? Je! kitu fulani kinaweza kuwa sanamu ya ibada katika sehemu moja ya ulimwengu lakini kiwe chenye makusudi ya kurembesha au kupamba katika sehemu nyingine ya ulimwengu? Ni nini kinachopaswa kumwongoza Mkristo katika kuamua kama ataharibu vitu fulani kwa sababu vinashirikiana na ibada ya sanamu?

Maandiko Matakatifu yanafunua wazi kwamba si picha zote, sanamu na mifano mingine ambavyo ni sanamu za ibada. Kama kitu ni sanamu ya ibada au hapana inategemea zaidi juu ya namna kinavyoonwa. Hii inaweza kufananishwa na mifano ya kale ya mafahali au ng’ombe dume.

Katika behewa la hekalu lililojengwa na Sulemani ilikuwapo “bahari ya kusubu.” Chombo hiki kikubwa kilikalia mafahali wa mfano kumi na wawili. Mifano hii hivyo ilikuwa na makusudi yote ya faida na ya kupamba. Lakini haikuabudiwa wakati wo wote. Wakitegemeza chombo ambacho kwa kawaida kilikuwa na karibu galani 11,600 za maji, mafahali hao walikuwa mfano unaofaa wa nguvu au uwezo. (1 Fal. 7:26) Walikazia fikira kwenye kweli inayotangazwa katika Zaburi 62:11: “Nguvu zina Mungu.”

Kwa upande mwingine, ndama wa dhahabu waliosimamishwa na Mfalme Yeroboamu katika Dani na Betheli walikuwa sanamu za ibada. Walipata ibada katika Ufalme wa Kaskazini wa Israeli. Hata ingawa dai lilifanywa kwamba ndama hao wa dhahabu walimwakilisha Yehova, hii haikufanya ibada iliyotiwa ndani na kutolewa kwao ikubalike. (1 Fal. 12:28; 14:7-9) Alitangaza Yehova kupitia kwa nabii wake Isaya: “Mimi ni [Yehova]; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.” (Isa. 42:8) Kwa kutengeneza ndama wa dhahabu (kwa wazi mafahali wachanga) na kuwatumia katika ibada, Waisraeli walijifanya wenyewe wenye hatia ya kugeuza utukufu wa Mungu kwa kitu kilichomwakilisha vibaya. Namna lilivyokuwa jambo la matusi kwa Mwenye Enzi Yote wa ulimwengu wote kuwakilishwa na fahali, “mla majani”!​—Zab. 106:20.

Uhakika wa kwamba fahali alikuwa chombo cha ibada katika Ufalme wa Kaskazini wa Israeli haukuwafanya mafahali katika hekalu la Sulemani sanamu za ibada. Vivyo hivyo, uhakika wa kwamba viumbe mbalimbali, mimea na jua, nyota, na mwezi​—vyote sehemu ya kazi za Mungu za uumbaji​—vimekuwa na bado vinapewa kicho huo wenyewe haungevifanya viwe havikubaliki kwa kurembesha au kupamba. Vitu vingi ambavyo wakati fulani viliabudiwa na watu wa kale vimepoteza maana yake ya ibada ya sanamu na kwa kawaida vinachukuliwa kama vya kurembesha tu.

Lakini, Mkristo ni lazima awe mwangalifu kwamba haanzi kuona chombo cho chote ambavyo hakiko. Jambo hili lilielezwa vizuri na mtumishi mwaminifu wa Yehova Ayubu: “Kama nililitazama jua lilipoangaza, au mwezi ukiendelea katika kung’aa; na moyo wangu umeshawishwa kwa siri, na midomo yangu imeubusu mkono wangu; hilo nalo lingekuwa uovu wa kuadhibiwa na waamuzi; kwani ningemwambia uongo Mungu aliye juu.”​—Ayubu 31:26-28.

Kwa hiyo, kama Mkristo aliona kwamba kuwako kwa picha fulani au chombo kungeweza kuchochea maoni yanayokamatana na ibada kwa sababu ya kushirikishwa kwake kale na ibada ya sanamu, angetaka kukiharibu. Hii ingetia ndani mapambo ya mtu mwenyewe, vitu vilivyofanyizwa kwa vito na dhahabu au vingine vya namna hiyo. Na, bila shaka, hangetaka kuweka vitu ambavyo kwa sasa vinadhaniwa kuwa na maana takatifu au ambavyo kwa wazi vimekusudiwa kutumiwa katika kawaida za ibada za dini ya uongo. Ingekuwa hivyo hata kama vitu vinavyotiliwa shaka havikuwa tena na maana ya kidini kwake. Kama Wakristo katika Efeso wa kale, angeharibu vitu vinavyoshirikishwa na ibada ya uongo, viwe vilikuwa vimegharimu kadiri gani ya fedha, ili kwamba mtu mwingine asivitumie kwa njia mbaya.​—Matendo 19:19.

Inampasa Mkristo vile vile akumbuke kwamba ni lazima afikirie dhamiri za wengine. Ijapokuwa yeye mwenyewe huenda akawa hana maoni yo yote ya ibada kuelekea picha fulani au chombo, wengine, kwa sababu ya hali zao za kidini, huenda wakayaona mambo kwa njia tofauti. Kwamba hili huenda hata likawa kweli kati ya Wakristo inatiwa mkazo na shauri la mtume Paulo lililoongozwa na roho ya Mungu: “Toeni hukumu hii, mtu asitie kitu cha kumkwaza ndugu au cha kumwangusha. Najua, tena nimehakikishwa sana katika Bwana Yesu, ya kuwa hakuna kitu kilicho najisi kwa asili yake; lakini kwake yeye akionaye kitu kuwa najisi, kwake huyo kitu kile ni najisi.”​—Rum. 14:13, 14.

Kwa hiyo mtu anayetaka ukubali wa Mungu anafanya vizuri kuchunguza picha na vyombo katika nyumba yake ili kuona kama inampasa afanye mageuzi fulani. Huenda akajiuliza mwenyewe: Je! watu katika mtaa ninaoishi wangechukua picha fulani na vyombo nilivyo navyo kama vyenye maana zaidi ya mapambo? Je! watu hawa wanashikamanisha vyombo hivyo na maana fulani yao ya kidini, wakivichukua kama vitakatifu au vya kuleta bahati nzuri? Je! picha fulani au vyombo katika nyumba yangu vingewaletea wengine mafikira ya kwamba mimi ninapatana na taratibu za dini ya uongo au mazoea? Je! vitu fulani nilivyo navyo vinawakilisha mafundisho ya Biblia vibaya? Ikiwa jibu kwa lo lote la maulizo haya ni “Ndiyo,” mwendo wa hekima ungekuwa ni kuondoa nyumbani mwa mtu kitu cho chote kinachoweza kumkwaza mtu mwenyewe au wengine.

Kwa kweli, hakuna lazima ya kupita kadiri juu ya jambo hili. Hata vitabu vya maarifa yote (encyclopedias) na kamusi vina mifano ya miungu ya uongo na ya kidini. Lakini mtu kuwa na vitabu kama hivyo vya kuangalia haiwapi wengine mafikira ya kwamba anakubaliana na mawazo ya uongo. Biblia yenye picha za kidini na mifano inaweza kuonwa kwa maana ile ile, yaani, kama kumbukumbu.

Inapaswa ikumbukwe, hata hivyo, kwamba matokeo ambayo picha na mifano mingine inakuwa nayo juu ya watu yanatofautiana sana. Hakuna anayeweza kuwawekea sheria. Kwa hiyo ikiwa mtu anaona kwamba hawezi kutazama picha bila kujisikia kuvutwa na dini ya uongo, angekuwa akitenda kwa busara ikiwa angeiharibu. Po pote panapokuwa na shaka la kweli, ni vizuri zaidi kila mara kuchagua mwendo utakaomwacha mtu akiwa na dhamiri safi mbele za Mungu.

Hivyo inakuwa wazi kwamba kila mtu anayetaka ukubali wa Mungu anapaswa kulifikiria jambo hili kwa uzito, ili ahakikishe kwamba anafahamu yanayompendeza Mungu. Mara nyuma ya kufanya hivyo, anaweza kusafisha nyumba yake kwa njia ya kidini. Kama matokeo hakuna cho chote alicho nacho kitamzuia asitoe ibada ya pekee kwa Muumba wake, Yehova Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki