Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 1/15 kur. 20-25
  • Kwa Nini Kujilinda na Ibada ya Sanamu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Kujilinda na Ibada ya Sanamu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maana ya Ibada ya Sanamu
  • Maoni ya Yehova juu ya Ibada ya Sanamu
  • Mwaminifu-Mshikamanifu Chini ya Mtihani
  • Sanamu Zashindwa Mahakamani
  • Dhabihu kwa Mashetani
  • Kwa Nini Kujilinda?
  • Je! Utajilinda na Ibada ya Sanamu?
  • Jilinde na Ibada ya Sanamu ya Kila Aina
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Maoni ya Kikristo Juu ya Mifano
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Ikimbieni Ibada ya Sanamu
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 1/15 kur. 20-25

Kwa Nini Kujilinda na Ibada ya Sanamu?

“Watoto wadogo, jilindeni nafsi zenu na sanamu.”—1 YOHANA 5:21.

1. Kwa nini ibada ya Yehova haina ibada ya sanamu?

YEHOVA si sanamu ya chuma, mbao, au jiwe. Hawezi kupewa makao katika hekalu la kidunia. Kwa kuwa yeye ndiye Roho mweza yote, asiyeweza kuonwa na wanadamu, haiwezekani kufanya mfano wa yeye. Kwa hiyo, ni lazima ibada safi ya Yehova iwe bila ibada ya sanamu kabisa.—Kutoka 33:20; Matendo 17:24; 2 Wakorintho 3:17.

2. Ni maswali gani yanayostahili ufikirio wetu?

2 Kwa hiyo, ikiwa wewe ni mwabudu wa Yehova, waweza kwa kufaa kuuliza hivi, ‘Ibada ya sanamu ni nini? Watumishi wa Yehova wameweza kuiepukaje katika wakati uliopita? Na kwa nini kujilinda na ibada ya sanamu?’

Maana ya Ibada ya Sanamu

3, 4. Ibada ya sanamu inaweza kufasiliwaje?

3 Kwa ujumla, ibada ya sanamu huhusisha sherehe au desturi fulani. Ibada ya sanamu ni kutolea sanamu heshima inayozidi, upendo, ibada, au kicho. Na sanamu ni nini? Ni mfano, kiwakilishi cha kitu fulani, au kifananisho kinachopewa ujitoaji. Kwa ukawaida, ibada ya sanamu huelekezwa kwa kitu chenye nguvu nyingi zaidi kihalisi au kinachodhaniwa kuwa na nguvu hizo kinachoaminiwa kuwa na uhai (mtu, mnyama,au shirika). Lakini ibada ya sanamu yaweza pia kuzoewa kwa habari ya vitu visivyo na uhai (kani au kitu cha asili kisicho na uhai).

4 Katika Maandiko, maneno ya Kiebrania yanayorejezea sanamu mara nyingi hukazia hali ya kutofaa kitu, au ni maneno ya kuonyesha dharau. Miongoni mwa hayo ni maneno yanayofasiriwa kuwa “mfano uliochongwa au kuchorwa” (kitu kilichochongwa, kihalisi); “umbo, mfano, au sanamu iliyoyeyushwa” (kitu kilichofinyangwa au kumwagwa); “sanamu yenye kuchukiza”; “sanamu ya ubatili” (utupu, kihalisi); na “sanamu-mavi.” Neno la Kigiriki eiʹdo·lon hufasiriwa kuwa “sanamu.”

5. Kwa nini yaweza kusemwa kwamba mifano yote si sanamu za kuabudiwa?

5 Mifano yote si sanamu za kuabudiwa. Mungu mwenyewe aliwaambia Waisraeli wafanye makerubi wawili wa dhahabu kwa ajili ya sanduku la agano na kutia mapambo ya viwakilishi vya viumbe hivyo vya kiroho kwenye funiko la ndani la nguo za hema za tabenakulo na kwenye pazia lililotenganisha Patakatifu na Patakatifu Zaidi. (Kutoka 25:1, 18; 26:1, 31-33) Makuhani wenye kutumikia rasmi tu ndio walioona viwakilishi hivyo vilivyotumika hasa kuwa ufananisho wa makerubi wa kimbingu. (Linganisha Waebrania 9:24, 25.) Ni wazi kwamba viwakilishi vya makerubi vya tabenakulo havikupasa kupewa heshima inayozidi, kwa kuwa malaika waadilifu wenyewe hawangekubali ibada.—Wakolosai 2:18; Ufunuo 19:10; 22:8, 9.

Maoni ya Yehova juu ya Ibada ya Sanamu

6. Maoni ya Yehova ni nini juu ya ibada ya sanamu?

6 Watumishi wa Yehova hujilinda na ibada ya sanamu kwa sababu yeye hupinga mazoea yote ya ibada ya sanamu. Mungu aliwaamuru Waisraeli wasifanye mifano ya vitu vya kupewa heshima iliyozidi na kuiabudu. Maneno haya yanapatikana miongoni mwa zile Amri Kumi: “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA [Yehova, NW], Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.”—Kutoka 20:4-6.

7. Kwa nini Yehova hupinga ibada ya sanamu yote?

7 Kwa nini Yehova hupinga ibada ya sanamu yote? Hasa ni kwa sababu yeye anatoza ujitoaji wa pekee, kama ilivyoonyeshwa katika Amri Kumi. Isitoshe, alisema hivi kupitia nabii wake Isaya: “Mimi ni BWANA [Yehova, NW]; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.” (Isaya 42:8) Wakati mmoja, ibada ya sanamu iliwatega Waisraeli kwa kadiri ambayo “walitoa wana wao na binti zao kuwa dhabihu kwa mashetani.” (Zaburi 106:36, 37) Waabudu sanamu hawakani tu kwamba Yehova siye Mungu wa kweli bali pia wanatumikia masilahi ya Mpinzani wake mkuu Shetani, pamoja na mashetani.

Mwaminifu-Mshikamanifu Chini ya Mtihani

8. Ni jaribu gani lililowakabili wale Waebrania watatu Shadraka, Meshaki, na Abednego?

8 Uaminifu-mshikamanifu hutufanya pia tujilinde na ibada ya sanamu. Hilo linatolewa kielezi kwa tukio lililorekodiwa kwenye Danieli sura ya 3. Ili kuzindua mfano mkubwa wa dhahabu aliokuwa amesimamisha, mfalme wa Babuloni Nebukadreza aliwakusanya maofisa wa milki yake. Amri yake iliwahusisha Shadraka, Meshaki, na Abednego—Waebrania watatu waliokuwa wakuu wa wilaya za Babuloni. Wote waliokuwako waliamriwa wasujudie mfano huo waliposikia sauti ya ala fulani za muziki. Hilo lilikuwa jaribio la kijimungu halisi cha Babuloni, Shetani, la kuwafanya Waebrania hao watatu wasujudie mfano uliowakilisha milki ya Kibabuloni. Ebu jiwazie ukiwa hapo.

9, 10. (a) Waebrania hao watatu walichukua msimamo gani, nao walithawabishwaje? (b) Mashahidi wa Yehova wanaweza kupata kitia-moyo gani kutokana na mwendo wa Waebrania hao watatu?

9 Tazama! Waebrania hao watatu wanasimama. Wanakumbuka sheria ya Mungu dhidi ya kufanya na kutumikia sanamu au mifano iliyochongwa. Nebukadreza awapa mkataa—wasujudu au wafe! Lakini wakiwa na uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova, wanasema hivi: “Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme. Basi kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”—Danieli 3:16-18.

10 Watumishi hao wa Mungu waaminifu-washikamanifu wanatupwa ndani ya tanuru yenye kupashwa moto sana. Akishangaa kuona watu wanne wakitembea ndani ya tanuru, Nebukadreza awaita Waebrania hao watatu watoke, na wao wanatoka bila dhara. Ndipo mfalme asema hivi kwa mshangao: “Na ahimidiwe Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego; aliyemtuma malaika wake [mtu wa nne katika tanuru], akawaokoa watumishi wake waliomtumaini, wakaligeuza neno la mfalme, na kujitoa miili yao ili wasimtumikie mungu mwingine, wala kumwabudu, ila Mungu wao wenyewe. . . . Hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.” (Danieli 3:28, 29) Kushika uaminifu-maadili kwa Waebrania hao watatu kunaandaa kitia-moyo kwa Mashahidi wa Yehova wa siku ya leo kuwa waaminifu-washikamanifu kwa Mungu, kudumisha kutokuwamo, na kuepuka ibada ya sanamu.—Yohana 17:16.

Sanamu Zashindwa Mahakamani

11. Ni rekodi gani iliyoandikwa na Isaya inayohusu Yehova na vijimungu vya sanamu?

11 Sababu nyingine ya kujilinda na ibada ya sanamu ni kwamba utoaji wa heshima inayozidi kwa sanamu ni jambo lisilofaa kitu. Ingawa baadhi ya sanamu zilizofanywa na watu huenda zikaonekana kuwa na uhai—mara nyingi zikiwa na mdomo, macho, na masikio—haziwezi kusema, kuona, wala kusikia na haziwafanyi wachaji wazo jambo lolote. (Zaburi 135:15-18) Hilo lilionyeshwa katika karne ya nane K.W.K., wakati nabii Isaya aliporekodi, kwa kweli, kesi ya mahakama kati ya Yehova na vijimungu vya sanamu. Katika kesi hiyo watu wa Mungu Israeli walikuwa kwenye upande mmoja, na mataifa ya kilimwengu kwenye upande mwingine.

12. Vijimungu vya mataifa viliwezanaje na mwito wa ushindani uliotolewa na Yehova?

12 Yehova alitolea vijimungu bandia vya mataifa mwito wa ushindani wa kusema “mambo ya zamani,” yaani, kutoa unabii kwa usahihi. Hakuna hata mmoja aliyeweza kufanya hivyo. Akiwageukia watu wake, Yehova alisema hivi: “Ninyi ni mashahidi wangu . . . nami ni Mungu.” Mataifa hayakuweza kuthibitisha kwamba vijimungu vyao vilikuwako kabla ya Yehova au kwamba viliweza kutoa unabii. Lakini Yehova alitabiri uharibifu wa Babuloni na kuachiliwa kwa watu wake waliokuwa mateka. (Isaya 43:8-28) Watu wa Mungu waliokombolewa wangeweza kusema kwamba ‘walikuwa wa Yehova.’ Yeye mwenyewe alisema hivi: “Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho; zaidi yangu mimi hapana Mungu.” Hakukuwa jibu la kukanusha kutoka kwa vijimungu vya sanamu. “Ninyi ni mashahidi wangu,” Yehova akasema tena kuhusu watu wake, akiongeza hivi: “Je! yuko Mungu zaidi yangu mimi? hakika hapana Mwamba.”—Isaya 44:1-8.

13. Ibada ya sanamu inafunua nini juu ya mwabudu sanamu?

13 Sisi pia hujilinda na ibada ya sanamu kwa sababu kushiriki katika hiyo kunaonyesha ukosefu wa hekima. Kwa sehemu ya mti anaochagua, mwabudu sanamu hufanya kijimungu cha kuabudu, na kwa sehemu nyingine anawasha moto ili apike chakula chake. (Isaya 44:9-17) Ni upumbavu kama nini! Mfanyi na mchaji wa vijimungu vya sanamu huona aibu pia kwa sababu ya kutoweza kutoa ushahidi wenye kusadikisha wa kuthibitisha uungu wavyo. Lakini Uungu wa Yehova ni wa hakika, kwani yeye hakutabiri tu kuwekwa huru kwa watu wake kutoka Babuloni bali pia alisababisha jambo hilo litukie. Yerusalemu lilikaliwa na watu tena, miji ya Yuda ikajengwa upya, na “vilindi” vya Babuloni—Mto Frati—vikakauka visiwe chanzo cha ulinzi wa Babuloni. (Isaya 44:18-27) Kama vile Mungu alivyotabiri pia, Koreshi Mwajemi alishinda Babuloni.—Isaya 44:28–45:6.

14. Katika Mahakama ya Juu Zaidi ya Ulimwengu Wote Mzima, ni jambo gani litakalothibitishwa daima?

14 Viabudiwa sanamu vilishindwa katika kesi hiyo ya kisheria kuhusu uungu. Na jambo lililolipata Babuloni kwa hakika litaupata mfano walo wa ki-siku-hizi, Babuloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini bandia. Milki hiyo pamoja na vijimungu vyayo vyote, sherehe za kidini, na vitu vya ibada ya sanamu vitaondolewa milele hivi karibuni. (Ufunuo 17:12–18:8) Ndipo itakapothibitishwa katika Mahakama ya Juu Zaidi ya Ulimwengu Wote Mzima, kwamba Yehova peke yake ndiye Mungu aliye hai na wa kweli na kwamba anatimiza Neno lake la kiunabii.

Dhabihu kwa Mashetani

15. Roho takatifu na baraza linaloongoza la karne ya kwanza lilionyesha nini kuhusu watu wa Yehova na ibada ya sanamu?

15 Watu wa Yehova hujilinda pia na ibada ya sanamu kwa sababu wanaongozwa na roho na tengenezo la Mungu. Baraza linaloongoza la karne ya kwanza la watumishi wa Yehova liliwaambia Wakristo wenzalo hivi: “Kwa maana ilimpendeza Roho Mtakatifu [roho takatifu, NW] na sisi, tusiwatwike mzigo ila hayo yaliyo lazima, yaani, mjiepushe na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na nyama zilizosongolewa, na uasherati. Mkijizuia na hayo, mtafanya vema. Wasalamu.”—Matendo 15:28, 29.

16. Katika maneno yako mwenyewe, ungeelezaje yale ambayo Paulo alisema juu ya vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu?

16 Sababu nyingine ya kujilinda na ibada ya sanamu ni ili kuepuka ushetani. Kuhusiana na Chakula cha Jioni cha Bwana, mtume Paulo aliwaambia Wakristo Wakorintho hivi: “Ikimbieni ibada ya sanamu. . . . Kikombe kile cha baraka tukibarikicho je! si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo? Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja; kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja. Waangalieni hao Waisraeli walivyokuwa kwa jinsi ya mwili; wale wazilao dhabihu, je hawana shirika na madhabahu? Basi niseme nini? ya kwamba kile kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu au ya kwamba sanamu ni kitu? Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani. Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani. Au twamtia Bwana wivu? Je! tuna nguvu zaidi ya yeye?”—1 Wakorintho 10:14-22.

17. Katika karne ya kwanza W.K., Mkristo angeweza kula nyama iliyotolewa dhabihu kwa sanamu chini ya hali zipi, na kwa nini?

17 Sehemu ya mnyama ilitolewa dhabihu kwa sanamu, sehemu iliwaendea makuhani, na mwabudu akapata sehemu kwa ajili ya karamu. Hata hivyo, sehemu ya mnofu huo ungeweza kuuzwa sokoni. Halikuwa jambo lifaalo kwa Mkristo kwenda kwenye hekalu la sanamu kula nyama hata ingawa hakuila ikiwa sehemu ya sherehe, kwani hilo lingewakwaza wengine au lingemvuta ndani ya ibada bandia. (1 Wakorintho 8:1-13; Ufunuo 2:12, 14, 18, 20) Kutoa mnyama kwa sanamu hakukuubadili mnofu, kwa hiyo Mkristo angeweza kununua sehemu yao sokoni. Na pia haikuwa lazima aulize-ulize juu ya chanzo cha nyama aliyopewa nyumbani mwa mtu fulani. Lakini ikiwa mtu alisema “kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka,” asingekila, ili kuepuka kumkwaza yeyote.—1 Wakorintho 10:25-29.

18. Wale ambao wangekula kitu kilichotolewa dhabihu kwa sanamu wangeweza kujihusishaje na mashetani?

18 Mara nyingi ilifikiriwa kwamba baada ya sherehe ya kidhabihu, kijimungu fulani kilikuwa katika nyama hiyo na kiliingia mwilini mwa wale walioila kwenye karamu ya waabudu. Kama vile wale waliokula pamoja walivyofanyiza kifungo kati yao wenyewe, ndivyo wale walioshiriki wanyama wa kidhabihu walivyokuwa na ushirika na madhabahu na kuwa na ushirika pamoja na kile kijimungu shetani kilichowakilishwa na sanamu hiyo. Kupitia ibada ya sanamu hiyo, mashetani waliwazuia watu wasimwabudu Mungu wa pekee wa kweli. (Yeremia 10:1-15) Haishangazi kwamba watu wa Yehova walipaswa waendelee kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu! Uaminifu-mshikamanifu kwa Mungu, kukubali mwongozo wa roho takatifu na tengenezo lake, na azimio la kuepuka uhusiano na ushetani vinathibitika pia kuwa vichocheo vyenye nguvu kujilinda na ibada ya sanamu leo.

Kwa Nini Kujilinda?

19. Ni aina gani ya ibada ya sanamu iliyokuwako katika Efeso la kale?

19 Wakristo hujilinda na ibada ya sanamu kwa bidii-nyendelevu kwa sababu ina namna nyingi, na hata tendo moja la ibada ya sanamu yaweza kuridhiana imani yao. Mtume Yohana aliwaambia waamini wenzake hivi: “Jilindeni nafsi zenu na sanamu.” (1 Yohana 5:21) Shauri hilo lilihitajiwa kwa sababu namna nyingi za ibada ya sanamu ziliwazunguka. Yohana aliandika kutoka Efeso, jiji lililojaa mazoea ya kimzungu na ngano juu ya viabudiwa bandia. Efeso lilikuwa na mojayapo maajabu saba ya ulimwengu—hekalu ya Artemi, mahali pa himaya kwa wahalifu na kitovu cha sherehe zisizo za kiadili. Mwanafalsafa Heraklitus wa Efeso alifananisha kile kijia chenye giza cha kuelekea kwenye madhabahu ya hekalu hiyo na giza la uovu, na aliona maadili ya washiriki wa hekalu hiyo kuwa mabaya zaidi ya yale ya hayawani. Hivyo, Wakristo Waefeso walipaswa wasimame imara dhidi ya ushetani, ukosefu wa adili, na ibada ya sanamu.

20. Kwa nini ilikuwa lazima kuepuka kujihusisha hata kidogo na ibada ya sanamu?

20 Wakristo wanahitaji azimio imara ili waepuke kujihusisha hata kidogo na ibada ya sanamu kwa sababu tendo moja tu la ibada kwa Ibilisi lingeunga mkono hoja yake ya kwamba wanadamu hawangebaki waaminifu kwa Mungu chini ya jaribu. (Ayubu 1:8-12) Alipokuwa akimwonyesha Yesu “milki zote za ulimwengu, na fahari yake,” Shetani alisema hivi: “Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia [na kufanya tendo moja la kuniabudu mimi, NW].” Kukataa kwa Kristo kulitegemeza upande wa Yehova wa suala la enzi kuu ya ulimwengu wote mzima na kukamthibitisha Ibilisi kuwa mwongo.—Mathayo 4:8-11; Mithali 27:11.

21. Kwa habari ya maliki wa Roma, Wakristo waaminifu walikataa kufanya nini?

21 Hata wafuasi wa mapema wa Yesu hawangefanya tendo moja la ibada kwa kuunga mkono upande wa Shetani wa suala hilo. Ingawa waliheshimu ifaavyo “mamlaka iliyo kuu” ya kiserikali, hawangechoma uvumba katika kumhesimu maliki Mroma, hata ikiwa ingewagharimu uhai wao. (Warumi 13:1-7) Kwa habari hiyo Danieli P. Mannix aliandika hivi: “Ni Wakristo wachache sana walioridhiana, ingawa madhabahu yenye kuwaka moto juu yayo iliwekwa uwanjani kwa ajili yao. Jambo tu ambalo mfungwa alihitaji kufanya ni kufukiza kiasi kidogo sana cha uvumba juu ya mwali wa moto naye alipewa Cheti cha Dhabihu na kuachiliwa. Pia alielezwa kwa uangalifu kwamba hakuwa akimwabudu maliki; alikuwa tu akikiri sifa ya kimungu ya maliki akiwa kichwa cha serikali ya Roma. Bado, ni Wakristo wachache sana waliojitwalia nafasi ya kuponyoka.” (Those About to Die, ukurasa 137) Ikiwa ungejaribiwa vivyo hivyo, je, ungepinga ibada ya sanamu yote?

Je! Utajilinda na Ibada ya Sanamu?

22, 23. Kwa nini ujilinde na ibada ya sanamu?

22 Kwa wazi, ni lazima Wakristo wajilinde na namna zote za ibada ya sanamu. Yehova adai ujitoaji wa pekee. Waebrania waaminifu watatu waliandaa kielelezo kizuri katika kukataa kuuabudu ule mfano mkubwa uliosimamishwa na mfalme wa Babuloni Nebukadreza. Katika kesi ya mahakama ya ulimwengu wote mzima iliyorekodiwa na nabii Isaya, Yehova peke yake ndiye aliyeonyeshwa kuwa Mungu wa kweli na aliye hai. Mashahidi wake Wakristo wa mapema walihitaji kuendelea kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu. Waaminifu-washikamanifu wengi miongoni mwao hawakushindwa na mbano wa kufanya hata tendo moja la ibada ya sanamu ambalo lingekuwa kumkana Yehova.

23 Kwa hiyo basi, je, wewe binafsi unajilinda na ibada ya sanamu? Je! unampa Mungu ujitoaji wa pekee? Je! wewe huunga mkono enzi kuu ya Yehova na kumsifu kuwa ndiye Mungu wa kweli na aliye hai? Ikiwa ndivyo, azimio lako lapasa kuwa kuendelea kusimama imara dhidi ya mazoea ya ibada ya sanamu. Lakini ni mambo gani zaidi ya Kimaandiko yanayoweza kukusaidia ujilinde na ibada ya sanamu ya kila aina?

Mawazo Yako Ni Nini?

◻ Ibada ya sanamu ni nini?

◻ Kwa nini Yehova hupinga ibada ya sanamu yote?

◻ Wale Waebrania watatu walichukua msimamo gani kuhusu ibada ya sanamu?

◻ Wale waliokula vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu wangeweza kujihusishaje na mashetani?

◻ Kwa nini tujilinde na ibada ya sanamu?

[Picha katika ukurasa wa 23]

Ingawa uhai wao ulitishwa, Waebrania hao watatu hawangeshiriki katika ibada ya sanamu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki