Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w01 7/15 uku. 28
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Kujilinda na Ibada ya Sanamu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Jilinde na Ibada ya Sanamu ya Kila Aina
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Imani Yao Ilishinda Jaribu Kali
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Thamini Uhusiano Wako na Yehova
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
w01 7/15 uku. 28

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Kwenye 1 Petro 4:3, twasoma kwamba wakati mmoja Wakristo fulani walikuwa wakishiriki katika “ibada haramu za sanamu.” Je, si ibada zote za sanamu ni haramu, zimeshutumiwa na kukatazwa na Mungu?

Naam, Mungu huona ibada yote ya sanamu kuwa haramu. Wale wanaotafuta kibali chake hawawezi kushiriki ibada ya sanamu.—1 Wakorintho 5:11; Ufunuo 21:8.

Hata hivyo, inaonekana kwamba mtume Petro alikuwa anarejezea ibada ya sanamu kwa njia nyingine. Hiyo ni kwa sababu, miongoni mwa mataifa mengi ya kale, ibada ya sanamu ilikuwa jambo la kawaida na lisilozuiwa kisheria na wenye mamlaka. Yaani, sheria ya nchi haikukataza ibada hiyo. Hata kuna aina fulani ya ibada ya sanamu ambayo ilikubaliwa na taifa au serikali. Kwa hiyo, wengine walikuwa wakishiriki katika ‘ibada za sanamu bila kizuizi chochote cha kisheria’ kabla ya kuwa Wakristo. (New World Translation, chapa ya 1950) Kwa mfano, huenda unakumbuka kwamba Mfalme Nebukadneza wa Babeli, alisimamisha sanamu ya kuabudiwa ya dhahabu, lakini Shadraka, Meshaki, na Abednego wakakataa kuiabudu.—Danieli 3:1-12.

Kwa upande mwingine, sherehe nyingi za ibada ya sanamu zilitia ndani matendo ambayo yalikuwa kinyume kabisa cha sheria za asili au hisia za maadili zinazotokana na dhamiri iliyorithiwa. (Waroma 2:14, 15) Mtume Paulo aliandika kuhusu mazoea yaliyopotoka ambayo yalikuwa “kinyume cha asili” na “yenye aibu,” mazoea ambayo mara nyingi yalikuwa sehemu ya sherehe za kidini. (Waroma 1:26, 27) Wanaume na wanawake walioshiriki katika ibada haramu ya sanamu hawakuruhusu asili yao ya kupambanua mema na mabaya iwazuie kufanya hivyo. Bila shaka ilifaa kwa wale waliokuwa Wakristo kuacha mazoea hayo mapotovu.

Isitoshe, ibada hizo za sanamu ambazo zilikuwa jambo la kawaida miongoni mwa watu wasio Wayahudi, zilishutumiwa na Yehova Mungu. Hivyo, hazikuwa halali.a—Wakolosai 3:5-7.

[Maelezo ya Chini]

a Andiko la 1 Petro 4:3 katika maandishi ya Kigiriki lamaanisha hivi kihalisi: “Ibada za sanamu zisizo halali.” Maneno hayo yametafsiriwa kwa njia tofauti-tofauti katika Biblia za Kiingereza kwa kutumia semi kama “ibada ya sanamu isiyoruhusiwa,” “ibada ya sanamu iliyokatazwa,” na “ibada za sanamu zilizo kinyume cha sheria.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki