Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 2/1 kur. 66-68
  • Shauri—Utafaidika Nalo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Shauri—Utafaidika Nalo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “HATUA YA KWANZA KUELEKEA KUPATA MSAMAHA”
  • WAKATI SHERIA HAIKUVUNJWA
  • KIZUIZI CHA KUFAIDIKA NA SHAURI
  • Sikiliza Shauri, Kubali Nidhamu
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Usipinge Shauri la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Je! Sikuzote Wewe Unapata Maana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • ‘Sikiliza Maneno ya Wenye Hekima’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 2/1 kur. 66-68

Shauri​—Utafaidika Nalo?

“TWAJIKAA sisi sote pia katika mambo mengi.” (Yak. 3:2) Bila shaka utakubaliana na kweli hiyo ya Maandiko. Wanadamu wote wanahitaji shauri la kuondoa makosa. Lakini watu wengi wanaitikiaje shauri? Je! wanafaidika nalo? Wewe wafaidika nalo?

Labda umeona maelekeo ya wengi ya kuwekea wengine lawama la makosa. Hili si jambo jipya, kama tuwezavyo kuona namna wanadamu wawili wa kwanza, Adamu na Hawa, walivyoitikia wakati Mungu alipouliza juu ya kula tunda fulani bila kutii. Twasoma hivi:

“Adamu akasema, Huyo mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda ya mti huo, nikala. [Yehova] Mungu akamwambia mwanamke, Nini hili ulilolifanya? Mwanamke akasema, Nyoka alinidanganya, nikala.”​—Mwa. 3:12, 13.

Kwa kuweka kosa juu ya “huyo mwanamke uliyenipa [wewe] awe pamoja nami,” Adamu hata alimaanisha kwamba Mungu alikuwa na kosa. Jitihada hizi za kujitetea hazikuleta faida kwa maana Mungu alifukuza Adamu na Hawa katika Bustani ya Edeni na mwishowe walikufa katika utimizo wa hukumu ya Mungu. (Mwa. 2:16, 17; 3:23, 24; 5:5) Mwishowe Yehova alisema: “Mimi sitamhesabia haki yeye aliye mwovu.” (Kut. 23:7) Kujaribu kufanya mwendo mbaya uonekane wenye haki ni bure kwa Mungu.

“HATUA YA KWANZA KUELEKEA KUPATA MSAMAHA”

Kwa upande mwingine, faida kubwa zinatokana na nia ya kutii shauri na kutengeneza mwendo mbaya. Ebu mfikirie Daudi, aliyevunja vibaya sheria ya Mungu. Daudi hakuzini na Bath-sheba tu, mke wa mwanamume mwingine, bali alitaka pia kufunika ufisadi wake kwa kufanya mpango mume wa Bath-sheba afe vitani. (2 Sam. 11:1-27) Kwa sababu hii, Mungu alimkemea vikali Daudi kupitia kwa nabii Nathani, akitabiria nyumba yake mabaya. Lakini Biblia yaendelea kusimulia hivi: “Daudi akamwambia Nathani, Nimemfanyia [Yehova] dhambi. Nathani akamwambia Daudi, [Yehova] naye ameiondoa dhambi yako; hutakufa.”​—2 Sam. 12:1-13.

Wakati uliofuata Daudi aliandika juu ya tukio hili: “Nalikujulisha dhambi yangu, wala sikuuficha upotovu wangu. Nalisema, Nitayakiri maasi yangu kwa [Yehova], nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.” Maelezo haya yanatolewa katika The Soncino Books of the Bible: “Yeye hakuwa akimpasha Mungu habari Aliyejua jambo alilokuwa ametenda; kwa kukiri kwake Yeye alijikiri mwenyewe. Hilo ndilo kusudi la kuungama na hatua ya kwanza kuelekea kupata msamaha. . . . Mwenye dhambi alipokwisha kutimiza upande wake, Mungu alikuwa tayari kutimiza upande Wake kama Mwenye Kusamehe.” Lo! namna Daudi alivyofaidika sana kwa kutii karipio’ Je! wewe pia wafaidika na karipio?

WAKATI SHERIA HAIKUVUNJWA

Namna gani ikiwa unapokea shauri juu ya tendo lisilovunja sheria? Je! ulione jambo hilo kama ‘si shughuli ya mtu bali ni yako mwenyewe’? Kwa habari ya jambo hilo, mtume Paulo aliandika haya:

“Kila kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri. . . . Na mtu [mpagani] asiyeamini akiwaalika [chakulani], nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri.

“Lakini mtu akiwaambia, Kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka, msile kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri. Nasema, dhamiri, lakini si yako, bali ya yule mwingine.” 1 Kor. 10:25-29.

Je! ulifahamu kanuni ya msingi iliyomo katika shauri hilo? Yampasa kila Mkristo aziheshimu dhamiri za wengine. Kitabu Word Pictures in the New Testament kinaeleza hivi:

“Paulo anajiweka kwa kufaa mahali pa ndugu aliye na nguvu anayetazamiwa kufikiria dhamiri ya ndugu aliye dhaifu anayeona kipande cha nyama kuwa jambo kubwa. Ni kupunguzwa kwa uhuru wa mtu kwa faida ya ndugu aliye dhaifu. Watu wawili wanatofautiana. Sababu moja tu ni upendo unaojenga ([1 Kor.] 8:2 na sura yote ya 13).”

Je! unaweza kufaidika na shauri kama hilo leo? Ni kweli, labda chakula hakitatokeza mashaka ya dhamiri mahali pako. Lakini labda mambo mengine yatatokeza. Kwa mfano: Kujipamba; mitindo ya mavazi; namna ya tafrija. Kama mtu angekushauri kwamba uchaguzi wako wa mambo hayo ulisumbua dhamiri ya Mkristo mwenzako, je! ungefaidika na shauri hilo ‘upunguze uhuru wako mwenyewe’ kwa sababu ya upendo?

KIZUIZI CHA KUFAIDIKA NA SHAURI

Wewe waitikiaje wakati mtu fulani anapokuonyesha makosa ambayo umefanya au anakupa wazo la kutengeneza jambo fulani la maisha yako? Namna gani ikiwa mtu anayekushauri ni mchanga au ni mwenye ujuzi kidogo kuliko wewe, au ni mdogo katika cheo mahali pako pa kazi? Je! unaudhika mara hiyo hata unazuiwa usifaidike na shauri jema? Sababu ya haya ni nini?

Ni maelekeo ya tabia ya kibinadamu yanayozungumzwa katika Warumi 12:3, ZSB: “Ninamwambia kila mutu wa kwenu, asiwaze kujisifu kupita ilivyomupasa kuwaza.” Sababu ni kiburi, ambacho ni kujisifu kusikofaa au kujiona mkubwa kushinda wengine. Unaweza kushinda kizuizi hiki cha kiburi namna gani?

Jambo la kwanza ni kuikubali kweli iliyoandikwa katika Warumi 3:23: “Wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.” Je! wasadiki hilo? Labda utajibu kwa haraka Ndiyo, lakini je! maisha yako yanaonyesha kwamba ndivyo unavyomaanisha? Kama unatoa wazo la kwamba ‘wewe hufanyi makosa sikuzote,’ kwa kukataa shauri jema, basi maisha yako yanaonyesha vingine.

Ebu fikiria matokeo yenye hatari ya kukataa kwa kiburi shauri la kukuonya makosa! Kwanza, kuna upweke, kwa maana ni nani anayetamani kushirikiana na mtu asiyekubali makosa yake? Zaidi ya hilo, Muumba anatangaza hivi: “Majivuno na kiburi . . . ninakichukia.” (Mez. 8:13 (Mit.), ZSB) Roho ya kiburi inaharibu uhusiano wa mtu na Yehova. Kwa hiyo, haiwezi kuleta faida nzuri. “Majivuno yanatangulia uharibifu, na roho ya kiburi inatangulia kuanguka.”​—Mez. 16:18, ZSB.

Kwa upande mwingine, “maonyo ya mafundisho ni njia ya uzima.” (Mez. 6:23, ZSB) Mtu anayeitikia shauri anatunza uhusiano mzuri na wengine, zaidi ya wote, anatunza uhusiano mzuri na Muumba. Mtu wa namna hiyo hapotezwi na upumbavu. Yeye hafaidiki na mawazo ya wengine tu, bali naye anamwonyesha mwenzake faida za maoni makuu. Kweli shauri ni lenye kufaidi. Ulizo ni: Je! wewe utafaidika nalo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki