Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 1/15 kur. 22-23
  • Je! Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Habari Zinazolingana
  • Kikubali Cheo Kikuu Cha Kristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Daraka Bora Mno la Kristo Yesu Katika Makusudi ya Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Haraka Inayokupasa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Je! Wakumbuka?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 1/15 kur. 22-23

Je! Wakumbuka?

Umesoma matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi kwa uangalifu? Ikiwa ndivyo, bila shaka utayakumbuka mambo haya:

● Kwa kuchagua Yehova awe Mungu wake na Israeli wawe watu wake, Ruthu Mmoabi alithawabishwaje sana?

Ruthu alipendelewa sana akawa kiungo katika nasaba iliyomtokeza Mfalme Daudi na kumalizika na Yesu Kristo.​—⁠M7/15/78 uku. 17.

● Ni akina nani ‘waliohamishwa wakaingizwa katika ufalme wa Mwana wa pendo lake Mungu,’ na kuanzia wakati gani na kuendelea? ​—⁠Kol. 1:13.

Wanafunzi waaminifu wa Yesu Kristo, Waisraeli wa kiroho, walikuja chini ya utawala wake kuanzia na Pentekoste ya mwaka 33 W.K. M9/1/78 uku. 8.

● “Utimilifu wote” wakaa katika Yesu Kristo katika maana gani?​—⁠Kol. 1:19.

Yesu Kristo anacho cheo kilicho kikuu zaidi katika kundi la Kikristo kwa habari ya cheo na mamlaka. Vilevile ana “utimilifu” wote wa yale yanayohitajiwa na Wakristo kwa uongozi na mafundisho. Mfano wake ni mkamilifu na mafundisho yake pia, bila kukosa cho chote ambacho lazima kiongezewe filosofia na mapokeo ya kibinadamu. Ilikuwa kulingana na mapenzi ya Yehova Mungu kwamba utimilifu wote ukae katika Mwana wake.​—⁠M9/15/78 kur. 7, 8.

● Kuna ushuhuda gani wa historia unaoonyesha kwamba kwa kweli Yesu Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu?

Zaidi ya wanafunzi Wakristo 500 walimwona Mwana wa Mungu aliyefufuliwa. (1 Kor. 15:6) Wale waliokuwa na uhakika kabisa kwamba Yesu Kristo alikuwa amefufuliwa kutoka kwa wafu waliutangaza ukweli huu bila kuogopa hata ingawa kufanya hivyo kulihatarisha maisha zao. Hawangeweza kuonyesha imani ya namna hiyo ikiwa hilo lilikuwa jambo la kuwazia tu. Jaribio lo lote la kudanganya lingaliweza kufunuliwa wakati huo, kwa kuwa adui za Wakristo walikuwa wamejikaza sana wawavunjie heshima na kukomesha utendaji wao. M11/15/78 kur. 4, 5.

● Kwa sababu gani Yehova Mungu akachagua kusema kupitia kwa mwaguzi Balaamu?

Kwa wazi Yehova alikusudia kuonyesha kwamba hakuna silaha yo yote inayoweza kufaulu ikitumiwa juu ya watu wake. Wamoabi na Wamidiani walikuwa wamefahamu kwamba uwezo wa kijeshi haungeshinda Israeli. Wakiamini kwamba Balaamu angeweza kuwalaani Waisraeli kwa matokeo, walimwona mwaguzi huyu kuwa silaha yao yenye nguvu kupita zote. Walakini, wakati Balaamu alipolazimishwa kuwabariki Israeli, ijapokuwa haikuwa kulingana na mapenzi yake, ilionekana wazi kwamba kupigana nao hakungefaulu.​—⁠M11/15/78 uku. 8.

● Kuna ushuhuda gani unaoonyesha kwamba jina la Mungu (YHWH), ambalo mara nyingi linaandikwa Yehova, lilionekana katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo?

Ushuhuda ulio mkubwa zaidi unatokana na vipande vya hati za maandishi ya kale ya tafsiri ya Septuagint Version ya Kigiriki iliyo tafsiri ya kwanza ya Kigiriki ya Maandiko ya Kiebrania. Katika hati zilizo kamili zaidi za tafsiri hii zenye tarehe za kuanzia na karne ya nne W.K., maneno ya Kigiriki ya “Mungu” na “Bwana” yametiwa mahali pa jina la Mungu. Walakini, katika vipande vilivyo vya kale zaidi, jina la Mungu linaonekana likiwa katika herufi za Kiebrania. Kwa kuwa jina la Mungu linapatikana katika nakala za Septuagint zilizopatikana katika karne ya kwanza, ni jambo la akili kuamua kwamba lazima waandikaji wa Biblia Wakristo wawe walitumia jina hilo walipokuwa wakitumia mafungu ya maneno kutoka katika Maandiko ya Kiebrania yaliyokuwa na jina hilo. Mwishowe wakati jina hilo lilipoondolewa katika nakala za Septuagint, ni wazi kwamba vilevile liliondolewa katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.​—⁠M10/1/78 kur. 7-12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki