Kurudia Mambo Makuu ya Kitabu Kulikoamsha Fikira
Mara nyingi wanafunzi ambao ni Mashahidi wa Yehova wanakuwa na nafasi za kushiriki “habari njema” na wengine shuleni. Kwa mfano, katika Spania, wanafunzi katika darasa fulani walipewa mgawo wa kusoma kitabu wakati wa likizo yao ya majira ya baridi na baadaye waje watoe ripoti juu yake darasani.
Shahidi mwenye umri wa miaka 12 aliamua kueleza mambo makuu kutoka kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako, kilichochapwa na Sosaiti. Msichana huyo alipoyarudia mambo makuu wanafunzi wenzake wengi walipendezwa. Na kama matokeo, Shahidi huyo kijana aliwaangushia wenzake vitabu 48 vya Ujana Wako, na funzo la Biblia lenye kufanya maendeleo likatokea kwa jitihada zake.
Kijana mwingine alisikia jambo hili lililoonwa likisimuliwa katika mkutano wa Kikristo. Naye, vilevile, alifurahia kupata matokeo mazuri sana katika kutolea wengine shuleni kitabu icho hicho chenye msingi wa Biblia.