Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 8/1 uku. 11
  • Ufahamu Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufahamu Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Moyo Wenye Furaha Unaponya’
  • ‘Ulimwengu Unahitaji Masihi’
  • Roho Zisizoonekana—Je! Zinatusaidia? Au Zinatuumiza?
    Roho Zisizoonekana—Je! Zinatusaidia? au Zinatuumiza?
  • Kuwasiliana na Ulimwengu wa Roho—Kunaonwaje na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Mbona Wengi Wanapendezwa na Uwasiliani-roho?
    Amkeni!—2000
  • Kwa Nini Uepuke Kuwasiliana na Pepo?
    Amkeni!—2008
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 8/1 uku. 11

Ufahamu Katika Habari

‘Moyo Wenye Furaha Unaponya’

● “Inaonekana kuna ukweli mwingi katika imani ya kwamba kadiri ulivyo na furaha ndivyo unavyoishi muda mrefu zaidi,” lilisema gazeti “The Wall Street Journal.” Lilitaja uchunguzi uliofanywa na wanafunzi waliohitimu wa chuo kikuu ambao maisha yao yalichunguzwa kwa muda wa miaka 32. Ilipatikana kwamba mahangaiko ya wakati wote, kushuka moyo na matatizo ya maono ya ndani yaliongeza hatari ya kuzeeka mapema, kutojiweza kwa mwili na kifo kinacholetwa na maradhi ya mwili. Kwa upande mwingine, ilipatikana kwamba afya nzuri ya akili ilizuia kuzeeka, kutojiweza kwa mwili na hesabu za vifo. Katika kikundi “bora” cha wanaume, 57 kati ya 59 walikuwa wangali na afya nzuri sana kufikia umri wa miaka 53. Kata hivyo katika kikundi “kibaya” ni 30 tu kati ya 48 waliokuwa wangali katika afya nzuri, wale wengine wakiwa wamekufa au wakiwa wamekuwa wagonjwa wakati wote.

Zamani sana, Biblia ilisema hivi: “Moyo wenye furaha unafanya mema katika kuponya, walakini roho iliyopigwa hufanya mifupa ikauke.” (Mit. 17:22, NW) Vivyo hivyo: “Moyo wa furaha huchangamsha uso.” (Mit. 15:13) Wengi wamepata kwamba, kwa kugeukia Biblia na kujifunza juu ya Mungu na kusudi lake la kusimamisha taratibu mpya yenye haki duniani, wamepunguza mahangaiko yao kwa kadiri kubwa. Vilevile, kwa kufanya mapenzi ya Mungu wanakuja chini ya uongozi wa roho yake takatifu yenye nguvu inayoleta “upendo, furaha, amani, . . . upole, kujiweza,”‏ yote hayo yakiwa yanasaidia kutokeza “moyo wenye furaha.”—Gal. 5:22, 23, NW.

‘Ulimwengu Unahitaji Masihi’

● Habari kutoka Roma inataja maneno haya rais na mwanzilishi wa “Klabu (Chama) cha Roma” kinachojulikana sana (ambacho ni kikundi cha mataifa yote cha watu wenye elimu nyingi) aliomba “masihi” auokoe ulimwengu kutoka kwa msukosuko wake wa sasa wa kijamii na kiuchumi. Ripoti hiyo ilisema hivi: “Aurelio Peccei, ambaye ameona kila namna ya maisha kwa miaka 72, anasema kwamba ulimwengu unahitaji sana masihi. Rais huyo na mwanzilishi wa Klabu cha Roma anasema kuwa kiongozi mwenye uwezo wa kuvuta watu—wa kisayansi, kisiasa au kidini —ndiye angekuwa wokovu pekee wa ulimwengu kutokana na misukosuko ya kijamii na kiuchumi inayoelekea kuharibu ustaarabu. Kiongozi huyo angepaswa kuachana na faida za taifa na za mataifa yote pamoja na mambo ya kisiasa na ya kiuchumi ili aongoze wanadamu kutoka kwa mabaya yanayowapata, akasema Peccei.”

Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote amejua uhitaji huo kwa muda mrefu. Yeye ameahidi mtawala huyo mwenye uwezo wa “kuachana na faida za taifa na za mataifa yote.” Hiyo inaonyeshwa na unabii juu ya mfalme wa Kimasihi katika Danieli 7:14: “Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie.”‏

Yesu Kristo aliyefukuzwa kwa hakika ndiye mfalme wa Kimasihi aliyeahidiwa na kutolewa na Mungu awe “kiongozi na jemadari kwa kabila za watu.” (Isa. 55:4) Yeye atakuwa mtawala wa namna gani? Nabii wa Yehova anamsimulia kuwa mwenye “roho ya hekima na ya ufahamu, roho ya kushauri na ya ukuu, roho ya maarifa na ya kumwogopa Yehova,”‏ ili ahukumu kwa haki na kuunganisha wanadamu katika amani.—Isa. 11:1-9, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki