Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 4/15 kur. 22-23
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Kaa Salama Ukiwa Sehemu ya Tengenezo la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Tengenezo la Yehova Lenye Kusonga Mbele
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Msifu Yehova Pamoja na Watu Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Yehova Analiongoza Tengenezo Lake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 4/15 kur. 22-23

Maswali kutoka kwa Wasomaji

● kwa kuwa neno “tengenezo” halipatikani katika Biblia, hata katika zile lugha za kwanza kabisa, tuna haki gani ya kusema kwamba Mungu ana tengenezo au kusema habari za tengenezo la Mungu?

Neno la kisasa la Kiebrania kwa “tengenezo” ni jina ir·gunʹ. Limetolewa kwenye neno la Kiebrania la kitendo, e·ragʹ, nalo lina maana ya “kupanga katika mstari,” na vilevile “kufuata.” Kwa hiyo, tengenezo ni mpango wa mambo. (Kama mfano wa jambo hilo, mtu akitaka anaweza kuangalia kitabu “Mambo Mawili Yasiyobadilika Asiyoweza Mungu Kusema Uongo,” sura ya 17, fungu la 28, katika chapa ya Kiebrania.)

Lugha ya Waebrania ina neno jingine linalolingana na “tengenezo,” yaani, histadruthʹ. Neno hilo linategemea neno linalopatikana katika Maandiko ya Kiebrania ya kwanza kabisa. Herufi za msingi au zilizo za maana zaidi katika neno histadruthʹ ni s na d na r. Konsonanti (heruf bubu) hizo tatu ndizo zimetumiwa kulifanyiza neno Kiebrania la kitendo, sadarʹ, nalo hasa lina maana ya “kupanga kwa utaratibu,” na kwa njia hiyo kufanyiza mpango fulani. Namna ya mtungo wa neno la kitendo (au kiarifa) sadar ndiyo inayokuwa msingi wa kutokea kwa jina histadruth’, ambalo maana yake ni “tengenezo.”

Ingawa hatulioni neno hilo katika Maandiko ya Kiebrania yaliyoongozwa na Mungu, tunaliona jina (noun) la Kiebrania linalohusiana nalo katika Ayubu 10:22, yaani, seder. Hapo jina hilo limetumiwa kwa namna ya wingi, nalo herufi zalo zimeendelezwa kuwa s’darimʹ. Tafsiri ya Biblia inayoitwa English Revised Version inaitafsiri Ayubu 10:22 kama ifuatavyo: “Nchi ya giza tititi, kama giza lenyewe; Nchi ya kivuli cha kifo, isiyo na utaratibu [s’darim’] wo wote, Na ambako nuru iko kama giza.” (Pia, Authorized Version; Young’s Literal Translation.) Hapo New World Translation inasema hivi: “Kwenye ile nchi ya ufichani kama giza nene, ya kivuli chenye giza jingi sana na ukosefu wa utaratibu [lo s’darim’], ambako hakuangazi mwangaza sawasawa na vile giza nene lisivyoangaza.” (Pia, The Emphasised Bible ya Rotherham.) Ukosefu wa utaratibu hapa ungekuwa na maana ya ukosefu wa mipango, hali ya mambo kuwa shaghala-baghala.

Mpaka leo hii Wayahudi wanalitumia neno seder. “Seder” ni sehemu ya Mishnah ya Kiyahudi (mafundisho ya mila za Wayahudi). Chini ya neno “Mishna,” Cyclopedia ya M’Clintock na Strong inasema: “Mishna imegawanywa sehemu sita (. . . , Sedarim, mipango), ambazo zina habari 62 mbalimbali . . . na sura 514 . . . Nazo sura zimegawanywa visehemu-sehemu ambavyo kila kimoja kina namba yacho.”

Kwa hiyo katika Biblia ya Kiebrania ya kwanza kabisa neno la kusema “utaratibu” au “mpango” linapatikana bila shaka. Akikazia uhitaji wa kuwa na utaratibu na mpango katika kundi la Kikristo, mtume Paulo aliwaandikia hivi Wakristo katika Korintho: “Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu. Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu [tafsiri za Kiebrania zinatumia maneno s‘darim’ n’khonim’].” (1 Wakorintho 14:33, 40) Shauri hilo lililotolewa na mtume katika karne ya kwanza lina mkazo ule ule hata leo kuhusiana na makundi yote ya mashahidi Wakristo wa Yehova. Mtume Paulo aliandika kwa kutumia Kigiriki kilichosemwa na watu wengi siku hizo, na neno la Kigiriki kwa “tengenezo” (au “organization” kwa Kiingereza) ni or·ganʹo·sis. Asili ya neno hilo ni er’gon, neno lililo na maana ya “kazi” linalopatikana mara nyingi katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

Kwa kuwa yote hayo yamezungumzwa kwa kuyalinganisha na Maandiko, mtu akijaribu kutoa ubishi wa kwamba Mungu hana tengenezo kwa sababu maneno ya kwanza kabisa yanayomaanisha “tengenezo” katika lugha za kale hayaonekani katika Maandiko ya Kiebrania na ya Kigiriki, mtu huyo anajaribu kuliepa jambo lililo wazi na la kweli. Katika kila jambo Mungu anaonyesha kwamba ana uwezo wa kusimamia mambo kwa njia ya kitengenezo. Ingekuwaje kama yeye asingesimamia viumbe wake watiifu kwa namna ya kitengenezo? Tengenezo shirika la watu wenye akili wanaokusanywa pamoja na kufanyiwa mipango ili wafanye kazi pamoja kwa amani na upatano ili wote watimize kusudi moja, yaani, kusudi la yule mwenye kuwasimamia kwa namna ya kitengenezo.

Kupatana na jambo hilo Mungu anaitwa mara nyingi ‘Yehova wa majeshi.’ Jeshi ni kundi la askari waliopangwa kitengenezo. Kwa hiyo, kwa kuunga mkono ile kweli ya kwamba Mungu ana tengenezo, tunasoma maneno yafuatayo yanayolitia moyo tengenezo lake: “Mhimidini [Yehova], enyi malaika zake, ninyi mlio hodari, mtendao neno lake, mkiisikiliza sauti ya neno lake. Mhimidini [Yehova] enyi majeshi yake yote, ninyi watumishi wake mfanyao mapenzi yake. Mhimidini [Yehova], enyi matendo yake yote mahali pote pa milki yake.’ (Zaburi 103:20-22) Yehova alikuwa na tengenezo la viumbe vya kimbinguni vya kiroho muda mrefu kabla hajaiumba dunia yetu na kumweka mwanadamu juu yayo.

Mungu anatumia semi za mifano katika hali mbalimbali kumaanisha tengenezo lake. Kisa cha kwanza cha kufanya hivyo kimo katika Mwanzo 3:15. Hapo Mungu analiita tengenezo lake la kiroho la huko mbinguni kuwa “mwanamke’ mwenye kupingana na “yule nyoka,” hayo yakiwa ni maneno ya mfano ya kumtaja Shetani Ibilisi. (Linganisha Mwanzo 3:14; Ufunuo 12:9.) Mwasi huyo mwenye kumpinga Mungu amemwiga Mungu akajifanyizia tengenezo linalopinga tengenezo la Mungu, kumpinga “mwanamke” wa Mungu wa usemi wa mfano.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki