Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 12/1 uku. 23
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Habari Zinazolingana
  • “Usitikiswe Upesi Katika Sababu Yako”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • “Nitachukua Machapisho Yenu Ikiwa Utachukua Yangu”
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Mashahidi wa Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Je, Wapaswa Kuchunguza Dini Nyingine?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 12/1 uku. 23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

■ kwa sababu gani Mashahidi wa Yehova hukataa kubadilishana vifaa vyao vya kujifunza Biblia na vitabu vya kidini vya watu wanaokutana nao?

Mashahidi wa Yehova wanatekeleza huduma yao ya peupe kwa kutii maagizo ya kimungu. Yesu alisema kwamba wakati wa huu “umalizio wa mfumo wa mambo,” “habari njema za ufalme [lazima] zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:3, 14, NW) Kwa hoyo Mashahidi hawaendi kwenye milango ya watu wakitafuta ukweli au nuru ya maarifa. Mahali pake, tayari wamekwisha kutumia saa zisizohesabika wakijifunza ukweli kutoka Neno la Mungu na, wakiwa wamekwisha kutwaa “habari njema,” kwa kutii wanatoka wakazishiriki na wengine.

Watu wengi wanaoamini kwamba ‘kuna wema katika dini zote’ huenda wakawa na maoni ya kwamba huko ni kuwaza kwa kijuu-juu. (Tofautisha na maoni ya Yesu yanayosemwa katika Mathayo 7:13, 14, 21-23.) Wanafalsafa Wagiriki katika Athene wa kale walikuwa na nia ya “kukubali yote” na walifurahia “kutoa habari na kusikiliza habari za jambo jipya.” (Matendo 17:18-21) Lakini mtume Paulo alipokuja mbele yao, hakuja kubadilishana faIsafa au mawazo na wao. Aliitumia pindi hiyo kutangaza aliyojua ni ukweli, wawe walimwona anawaza kijuu-juu tu au la. Ingawa wengine wa Waathene hao walimfanyia dhihaka, hesabu fulani waliitikia wakawa waamini.​—Matendo 17:32-34; 2 Wakorintho 6:14-18.

Bila shaka Paulo alitambua mafundisho fulani ya Kigiriki, na alitumia maarifa hayo kutoa ushuhuda wenye matokeo sana. (Matendo 17:28) Hali moja na hiyo, Mashahidi wa Yehova wanajua imani za wengine. Wamekwisha kupata maarifa ya kutosha ya msingi juu ya mafundisho ya imani za dini zilizo za kawaida katika eneo lao. Mafundisho hayo yamekwisha kuzungumzwa katika kitabu What Has Religion Done for Mankind? na pia makala nyingi katika Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Habari za namna hiyo juu ya dini mbalimbali zinatolewa kwa maoni ya kwamba zinatofautiana na mafundisho sahihi ya Biblia.

Neno la Mungu linaonya Wakristo kwamba “Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.” (2 Wakorintho 11:14, 15) Kwa kufaulu sana Shetani alionekana kama “malaika wa nuru” hata akaweza kudanganya mwanadamu mkamilifu, Hawa. (1 Timotheo 2:14) Kwa hiyo ungekuwa upumbavu, na pia kupoteza wakati wenye thamani kwa Mashahidi wa Yehova kukubali na kujiweka katika hatari ya kuambukizwa na vitabu vya dini ya uongo ambavyo vimekusudiwa vidanganye. Hawana nia ya kuanguka katika mwendo wenye kusikitisha wa Wayahudi, ambao Paulo alisema ‘walibadilishana ukweli wa Mungu na uongo.’​—Warumi 1:25, NW.

Zaidi ya hayo, vingine vya vitabu vya kidini ambavyo huenda watu wakawasihi Mashahidi wa Yehova wasome vimeandikwa na, au ndani yake mna mawazo, ya watu ambao wameikana imani. Wakristo wa kweli wanaamriwa wawakatae waasi-imani hao. (2 Yohana 9-11; Tito 3:10, 11) Basi, kwa kufaa, Mnara wa Mlinzi wa Novemba 15, 1983, ulishauri hivi:

“Katika karne ya kwanza, Himenayo na Fileto waligeuka wakawa waasi-imani na kujaribu kupindua imani ya wengine. Kiwango cha Mungu kilisema: ‘Jiepushe na semi hizo zisizo na faida yo yote zinazochafua kilicho kitakatifu.’ (2 Timotheo 2:16-19, NW) Wakristo wenye kushika kiwango hicho wasingalipendezwa na kuwasikiliza waasi-imani hao, wala wasingalipendezwa na kujipatia maandishi yo yote yenye sumu ambayo watu hao wangaliweza kugawa ‘kwa ajili ya mapato ya aibu.’ Mbona wauchangie uovu wao pesa kwa kununua vitabu vyao? (Tito 1:11) Sisi Wakristo washikamanifu na tushike viwango vya Mungu, tulishe akili zetu mambo yaliyo ya kweli na ya uadilifu, tuufuate kwa ushikamanifu na kuthamini kipitio kilichotumiwa kutufunza kweli ya Biblia hapo kwanza.​—Linganisha 1 Timotheo 4:16.​—Ukurasa 15.

Kwa hiyo, kwa sababu ya hekima na kuheshimu shauri la Mungu, Mashahidi wa Yehova hawazoei kubadilishana vifaa vya kujifunza Biblia vyenye thamani ambavyo ndani yake mna ukweli wa Kimaandiko na kuchukua vitabu vya kidini vinavyoeneza kosa au mawazo ya kuasi-imani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki