“Nitachukua Machapisho Yenu Ikiwa Utachukua Yangu”
Maneno hayo husemwa na baadhi ya wenye nyumba. Kwa kuwa hatubadilishani machapisho yetu ya kujifunzia Biblia na machapisho ya dini za uwongo, tunawezaje kujibu kwa busara? (Rom. 1:25) Tunaweza kusema: “Asante sana. Chapisho hili linasema nini kuhusu suluhisho la matatizo ya wanadamu? [Mruhusu ajibu. Akikuomba usome chapisho lake ili upate jibu, unaweza kumkumbusha kwamba hukumpa chapisho kabla ya kumweleza habari iliyo katika chapisho hilo. Kisha usome au unukuu andiko la Mathayo 6:9, 10.] Yesu alisema kwamba Ufalme wa Mungu utafanya mapenzi ya Mungu yatendeke duniani kote. Kwa hiyo, chapisho pekee la kidini ambalo mimi husoma huzungumzia hasa Ufalme wa Mungu. Je, ninaweza kukuonyesha katika Biblia mambo fulani hususa ambayo Ufalme wa Mungu utatimiza?”