“Usitikiswe Upesi Katika Sababu Yako”
“Tunawaomba ninyi msitikiswe upesi katika sababu yenu wala kutiwa wasiwasi kupitia usemi ulioongozwa kwa roho au kupitia ujumbe wa maneno au kupitia barua fulani kama kwamba imetoka kwetu.”—2 WATHESALONIKE 2:1, 2, Biblia ya New World Translation.
1. Ni mambo gani ya kupendeza tunayokumbuka tukiufikiria wakati ambao tulijifunza ukweli mara ya kwanza?
TUNAKUMBUKA mambo mengi ya kupendeza wakati sisi Wakristo tunapoufikiria wakati tulipojifunza kwanza ukweli wa Neno la Mungu. Kufanya hivyo kulifurahisha sana, kulifaa, kuliridhisha. Mioyo yetu ilifurikwa na uthamini wakati tulipojifunza juu ya Yehova na sifa zake zilizotukuka, kutia na upendo wake mwingi na rehema! Tulifurahi sana tulipoanza kushirikiana na waamini wenzetu wenye kuonyesha upendo wa kweli wa Kikristo kisha wakawa wanaishi kulingana na kanuni za Biblia.
2. Sisi watumishi wa Yehova tuna mataraja gani, nasi tunajikuta katika hali gani ya kiroho?
2 Jinsi tulivyoshukuru kujifunza kwamba karibuni Yehova ataondoa maumivu, huzuni, na hata kifo. (Ufunuo 21:3, 4) Wazia, kuishi milele katika paradiso duniani, ukiwa afya nzuri kabisa na furaha kamili! Hayo yalikuwa mambo mazuri sana hata karibu yawe kama ndoto, sivyo? Lakini yalikuwa kweli. Yalitegemezwa na Neno la Mungu. Yalisisimua! Bila shaka tulihisi kama wanafunzi wakati Yesu alipowatokea baada ya ufufuo wake. Waliambiana: “Je! mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko?” (Luka 24:32) Ndiyo, tulipojifunza ukweli na kuweka wakfu maisha zetu kwa Yehova, tulijikuta katika paradiso ya kiroho. Ni baraflka iliyoje!
3. Ibilisi na wapinzani wengine wanatafutaje kutuzuia tusizipate faida za paradiso ya kiroho ya Yehova?
3 Lakini kuwa katika paradiso ya kiroho ya Yehova si jambo tunaloweza kulichukua vivi hivi tu. Tuliingia katika paradiso hiyo kwa kujitolea wenyewe; tunaweza kutoka nje (au kuondolewa nje) tukikosa kuamini au tukivunja kwa makusudi sheria za uadilifu za Yehova. Bila shaka, hilo halitatokea tukiutunza ukiwa wenye nguvu ‘upendo tuliokuwa nao kwanza,’ tukiendelea kuthamini maandalizi yote ya Yehova ya kutuweka wenye nguvu kiroho. (Ufunuo 2:4) Lakini Ibilisi na wapinzani wengine wa ibada ya kweli ni mafundi wa udanganyifu. Hatupaswi kusahau kamwe kwamba wanakaa tayari daima ili wayunje ukamilifu wetu wakiweza. Progaganda zao zimekusudiwa zidhoofishe imani yetu, zipoze upendo wetu kwa Mungu, zipande mashaka akilini mwetu—ndiyo, zimekusudiwa zifanye paradiso ya kiroho ionekane si paradiso hata kidogo.
4. Matokeo yanaweza kuwa nini tukiruhusu imani yetu idhoofike na kuachilia mashaka mazito yasitawi?
4 Kwa usemi wa kimithali, tunaweza kufika kwenye hatua ambayo tunaona ni jambo gumu, labda hata lisilowezekana, kuona msitu wa miti ile mingine ya paradiso kwa sababu ya kutazama sana miti isiyokamilika ya kibinadamu iliyomo ndani ya paradiso hiyo sasa. Msisimuko tuliokuwa nao tulipojifunza ukweli wa Neno la Mungu, pia lile tumaini bora sana tulilolipata, hata upendo tuliokuza kuelekea Mungu na ndugu zetu za kiroho, na bidii tuliyokuwa nayo kwa ajili ya utumishi wa Yehova, unaweza kufifia. Ikiwa hatua kubwa hazichukuliwi ili kuondoa uharibifu huo wa kiroho, karibuni matakwa ya Mungu yenye upendo yanaonekana kuwa ya uonevu. Huenda chakula chenye kuleta afya kutoka kwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili” kikaonekana kuwa kitu cha kudharaulika, na udugu wa watumishi wenye upendo wa Yehova huenda ukaonekana kuwa nyumba y a maadui. Halafu uradhi peke yake, ambao umepotoka, ungekuja wakati mtu huyo anapoanza kuwapiga watumwa wenzake kwa kutumia uchongezi na mambo ambayo si ya kweli kabisa.—Mathayo 24:48-51.
5. Hasara ya mtu inaweza kulinganikaje na walichokipoteza Adamu na Hawa kwa kufukuzwa katika Paradiso ya Edeni?
5 Ndiyo, zaidi ya kuweza kupoteza faida za paradiso ya kiroho sasa lakini, jambo zito zaidi, ni kwamba tungeweza pia kupoteza tumaini la kuishi milele katika Paradiso ya kidunia. Na tunaweza kuuacha mwendo kwa sababu ile ile ambayo Adamu na Hawa walipoteza Paradiso ya Edeni. Walikuwa na kila kitu walichohitaji ili wawe na furaha kamili na wangaliweza kuishi milele. Lakini hali ya kujitegemea—ambayo kwa kweli ilikuwa fundisho tofauti—ikawa ya maana kwao kuliko utii kwa Yehova na zile baraka za Edeni. Hawa alidanganywa. Ingawa Adamu hakudanganywa, aliruhusu uvutano wa hali, kutia na maongozi makubwa ya mke wake, yamtendeshe dhambi yeye pia. Basi, waliondolewa katika Paradiso, wakaishi maisha yenye masikitiko mpaka kufa kwao. Waliiipotezea wenyewe taraja la uzima wa milele na wakaletea wazao wao urithi wa dhambi na kifo (Mwanzo 3:1-7, 14-19, 24; 1 Timotheo 2:14; Warumi 5:12) Ilikuwa bei ya kuhuzunisha kama nini ya kulipia ule uliosemekana kuwa ni uhuru wao ati!
6. (a) Paulo alionyesha hangaikio gani kuhusu watu fulani katika kundi la Korintho? (b) Alionyeshaje hangaikio ilo hilo katika habari alizoliandikia kundi katika Thesalonike?
6 Mtume Paulo alijieleza kuwa mwenye hangaiko hili: “Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.” (2 Wakorintho 11:3) Paulo aliuona uhitaji mkubwa wa kuandika juu ya mafundisho fulani yenye kosa yaliyokuwa yakienea katika siku zake. Katika barua ya pili aliyoliandikia kundi katika Thesalonike, yeye alisema: “Tunawaomba ninyi msitikiswe upesi katika sababu yenu wala kutiwa wasiwasi kupitia usemi ulioongozwa kwa roho au kupitia ujumbe wa maneno au kupitia barua fulani kama kwamba kutoka kwetu, ya kwamba siku ya Yehova imefika. Mtu ye yote asiwashawishi kwa njia yo yote.”—2 Wathesalonike 2:1-3, NW.
Usifanye Shughuli Zo Zote na Waasi-Imani
7. (a) Ni maulizo gani yanayotokea ikiwa vitabu vya waasi-imani vimepokewa katika sanduku la posta? (b) Kwa habari ya kujilinda na mavutano ya waasi-imani, sababu gani ni hatari mtu kujiona mwenye uhakika kupita kiasi?
7 Sasa, utafanya nini ukikabiliwa na fundisho la uasi-imani—mawazo ya ujanja—lenye kudai kwamba mambo unayoamini ukiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova siyo ukweli? Kwa mfano, utafanya nini ukipokea barua au kitabu fulani, ukifungue, na mara moja uone kwamba kimetoka kwa mwasi-imani? Je! utafiti utakufanva ukisome, ili uone tu anayosema? Huenda hata ukawaza hivi: ‘Haitanidhuru; mimi ni mwenye nguvu mno katika ukweli. Zaidi ya hilo, ikiwa sisi ndio wenye ukweli, hatuna cha kuogopa. Ukweli utabaki umesimama ujapotiwa katika jaribu.’ Kwa kufikiri hivyo, wengine wamelisha akili zao mawazo ya waasi-imani kisha wakaanza kudadisi-dadisi na kuwa na mashaka mazito. (Linganisha Yakobo 1:5-8.) Kwa hiyo likumbuke onyo kwenye 1 Wakorintho 10:12: “Anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.”
8. Ni usaidizi gani unaohitajiwa na wengine ambao wamelemewa na mashaka?
8 Kwa kupewa msaada wenye upendo na ndugu wanaojali, wengine wenye mashaka yaliyopandwa na waasi-imani wamepata nafuu baada ya kipindi cha maumivu na uchungu mwingi wa kiroho. Lakini maumivu hayo yangaliweza kuepukwa. Kwenye Mithali 11:9 (NW) tunaambiwa hivi: “Kwa kinywa chake mtu aliye mwasi-imani analeta mtu mwenzake kwenye uharibifu, lakini kwa maarifa waadilifu wanaokolewa.” Yuda aliwaambia Wakristo wenzake waendelee “kuonyesha rehema wengine wenye mashaka; waokoeni kwa kuwanyakua kutoka motoni.” (Yuda 22, 23) Paulo alimshauri mwangalizi Timotheo awafundishe “kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli; wapate tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambao hao wametegwa naye, hata kuyafanya mapenzi yake.”—2 Timotheo 2:25, 26.
9. Ni matokeo gani yenye msiba yanayowapata wale wanaoiacha ibada ya kweli?
9 Msiba wenye kusikitisha ni kwamba wengine wameingia katika giza tititi, hata wakarudia mafundisho ya Jumuiya ya Wakristo. Mtume Petro aliandika juu ya wengine waliotembea katika ukweli lakini wakageuka kando. Alisema: “Kwa hakika. ikiwa wanajitia tena katika mambo yenyewe hayo nao wanashindwa baada ya kuyaepuka mambo ya unajisi ya ulimwengu kwa maarifa sahihi ya Bwana Mwokozi Yesu Kristo, hali za mwisho zimekuwa mbaya zaidi kwao kuliko za kwanza.” Petro alisema wanafanana na mbwa anayerudia matapiko yake na nguruwe aliyesafishwa anayerudi kugaa-gaa matopeni.—2 Petro 2:20-22.
10. (d) Yehova anasema nini juu ya kuwasikiliza waasi-imani? (b) Kusoma vitabu vya waasi-imani kungekuwa sawa na kufanya nini?
10 Wakati mwanadamu mwenzetu anapotuambia, ‘Usifanye hivi’ au, ‘Usiyasikilize hayo,’ huenda tukashawishwa kupuuza shauri lake. Lakini kumbuka kwamba katika kisa hiki ni Yehova anayetuambia katika Neno lake jambo la kufanya. Naye anasema nini juu ya waasi-imani? ‘Waepukeni’ (Warumi 16:17, 18); “msichangamane” nao (1 Wakorintho 5:11); na ‘msiwakaribishe nyumbani mwenu, wala kuwapa salamu’ (2 Yohana 9, 10). Hayo ni maneno yenye mkazo, ni mielekezo iliyo wazi. Iwapo, kwa utafiti, tunasoma vitabu vya mwasi-imani anayejulikana, je, hiyo haingekuwa sawa na kumkaribisha adui huyo wa ibada ya kweli ndani ya nyumba yetu aketi pamoja nasi na kutusimulia mawazo yake ya uasi-imani?
11, 12. (a) Ni mfano gani unaotolewa kutusaidia tufahamu kwamba hatuwezi kusoma vitabu vya waasi-imani na bado tusiwe na hatia? (b) Jambo hilo linaweza kutumiwaje kuhusu jinsi Yehova anavyohangaikia watu wake?
11 Tuonyeshe hilo kwa mfano huu: Tuseme kwamba mwanao tineja angepokea katika sanduku la posta kichapo fulani kinachoonyesha ngono chafu. Wewe ungefanya nini? Ikiwa angekuwa na maelekeo ya kukisoma kwa utafiti, je, wewe ungesema: “Ndiyo, ni sawa mwanangu, soma tu. Hutapatwa na madhara. Tangu utoto tumekufundisha kwamba ukosefu wa adili ni mbaya. Isitoshe, unahitaji kujua yanayoendelea ulimwenguni ili ujue kweli kweli kwamba ni mbaya’? Je! wewe ungetoa sababu hizo? Bila shaka sivyo! Badala yake, kwa uhakika ungemwonyesha hatari za kusoma vitabu vyenye kuonyesha uchafu wa ngono na kutaka viharibiwe. Kwa sababu gani? Kwa sababu hata mtu awe na nguvu jinsi gani katika ukweli, akilisha akili yake mawazo yaliyopotoka yanayopatikana katika vitabu hivyo, yatadhuru akili na moyo wake. Tamaa mbaya yenye kusalia iliyopa-ndwa nyuma ya moyo hatimaye inaweza kutokeza tamaa mbaya ya ngono. Matokeo yangekuwa nini? Yakobo anasema kwamba tamaa mbaya inapositawi, inazaa dhambi, na dhambi inaongoza kwenye kifo. (Yakobo 1:15) Kwa hiyo mbona uanzishe mfululizo huo wa mambo?
12 Basi, ikiwa tungefanya uamuzi huo wa moja kwa moja kulinda watoto wetu na mambo hayo ya uchafu wa ngono, je, tusitazamie Baba yetu wa kimbingu mwenye upendo atulinde sisi vivyo hivyo kutokana na uasherati wa kiroho, kutia na uasi-imani? Yeye anasema, Jiepushe mbali nao!
13. Tunaweza kufanya nini ikiwa tunapokuwa katika kazi ya kuhubiri maulizo yenye mashtaka yanatokezwa kwa kutegemea mambo yaliyosemwa au kuandikwa na waasi-imani?
13 Lakini iweje iwapo kwamba tunapokuwa tukihubiri habari njema watu wanatokeza maulizo au vipingamizi vinavyofanana na vile vinavyotokezwa na wapinzani? Bila shaka, ikiwa mtu hana moyo mweupe na anataka tu kufanva ubishi, kwa kawaida inakuwa vizuri zaidi kujitafadhalisha ili tuondoke na kwenda mlango ule mwingine. Lakini ikiwa mtu anauliza kwa moyo mweupe juu ya madai fulani ya waasi-imani, ni jambo gani linaloweza kufanywa? Kwanza tunaweza kuuliza ni iambo gani hasa limetokeza hangaiko hilo. Huenda ikawa ni jambo moja au mawili tu. Halafu tunaweza kushikamana na hayo na kujibu kwa Maandiko, kwa vichapo vya Sosaiti, na kwa yale tunayojua kuwa ni ukweli juu ya habari hiyo. Hatupaswi kukata maneno kwamba ni lazima tusome kitabu fulani au gazeti ambalo limejaa uchongezi na kweli ambazo ni kweli nusu ili tukanushe madai na mafundisho ya uwongo ya wapinzani.
Kumtumaini Yehova kwa Uhakika
14. Baba yetu wa kimbingu anatuonyesha hangaikio gani lenye upendo, na kwa sababu gani tunaweza kumtumaini yeye kabisa?
14 Tunaposonga mbele, tukijenga imani na kuendelea kujishughulisha katika utumishi wa Ufalme, tunaweza kumtumaini Yehova kwa uhakika, tukijua kwamba yeye akiwa ndiye Baba yetu wa kimbingu mwenye upendo, anatutaka tupate faida zilizo kubwa zaidi. Mungu anatufundisha; anatuonya. Anafanya hivyo kupitia Neno lake na kwa mwelekezo ulio wazi unaoandaliwa na tengenezo lake linaloonekana. Kama tungeomba mzazi mwenye upendo atupe mkate na samaki, yeye hangetupa jiwe au nyoka. Naye Mungu hatatupumbaza wala kutudanganva, (Mathayo 7:7-11) Hata hivyo, Mungu hatatukinga ili kwamba tusipatwe kabisa na vishawishi au hata kunenewa mambo ya udanganyifu na propaganda za kiibilisi. Yeye anasema hivi juu yake mwenyewe: “Mimi ni [Yehova], Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.” (Isaya 48:17) Ndiyo, Yehova ‘anatufundisha ili tupate faida.’ Anatuambia tuendelee kujitenga na waasi-imani na fundisho lao, na kufanya hivyo kunatulinda sisi wenyewe. Kunamaanisha uzima wetu.
15. Ni maonyo gani ambayo mtume Paulo alitoa juu ya wengine ambao wangejaribu kuwavuta wanafunzi wawafuate wao?
15 Mtume Paulo aliwaonya hivi wazee wenzake Wakristo: “Katika ninyi wenyewe watainuka watu, wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao.” (Matendo 20:30) Tukiendelea kusikiliza hoja za ujanja na sababu zinazoonekana kama kwamba ni za kweli, “mapotovu” yanaweza kusikika kama kwamba yamenyooka. Kwa kadiri Hawa alivyoendelea kutazama tunda lililokatazwa na kusikiliza sababu zilizopotoka za Ibilisi, ndivyo alivyoendelea kusadikishwa alikuwa akisema kweli. Paulo alionya hivi: “Angalieni mtu asiwafanye mateka kwa elimu yake ya bure na madanganyo matupu kwa jinsi ya mapokeo ya wanadamu, kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya ulimwengu, wala si kwa jinsi ya Kristo.” (Wakolosai 2:8) Mtume alionyesha pia kwamba “kwa maneno laini na ya kujipendekeza [waasi-imani] waidanganya mioyo ya watu wanyofu.” (Warumi 16:17, 18; linganisha 2 Wakorintho 11:13-15.) Bila shaka, uhakika wa kwamba wachache wanavutwa na propaganda hiyo haumaanishi kwamba ni lazima tuwafuate. Hata hivyo, tunahitaji kuendelea kukaa chonjo.
16. Ni kutumiwa kwa maonyo gani ya Kimaandiko kutatusaidia tushinde jitihada za Shetani za kudanganya watu na kuwaongoza watoke katika ibada ya kweli?
16 Mbinu za Ibilisi hazijabadilika tangu Edeni. Yeye anatumia mashaka ya ujanja na kuvutia tamaa ya kujipendeza binafsi. Petro aliandika hivi: “Pia walimu wa uwongo [watakuwa] miongoni mwenu ninyi. Watu wenyewe hao wataingiza kisiri-siri madhehebu zenye kuharibu . . . Vilevile, kwa tamaa watawatumieni ninyi kwa faida yao kwa kutumia maneno ya bandia.” (2 Petro 2:1-3, NW) Kitu bandia kimekusudiwa kionekane au kisikike kuwa ni cha kweli. Kwenye 2 Timotheo 2:14-19 (NW), Paulo alikazia sha mambo lakini akaonya juu ya uhitaji wa kuepuka waasi-imani, ambao ‘maneno yao matupu yanachafua kilicho kitakatifu,’ kwa rnaana, kama alivyosema yeye, ,“neno lao litaenea kama donda-ndugu.”
17, 18. (a) Fundisho la uasi-imani linafananaje na donda-ndugu? (b) Mtume Petro anatoa onyo gani juu ya wale wanaojaribu kutuondoa katika ibada ya kweli? (c) Ni maulizo gani yatakayojibiwa katika funzo linalofuata?
17 Huo ni ufanani unaofaa kweli kweli! Kama donda-ndugu, mawazo ya uasi-imani yanafanana kabisa na kifo cha kiroho chenye kuenea haraka. Na kwa kuwa washiriki wa kundi ni kama mwili mmoja, kuna hatari ya kwamba huenda wengine wakaambukiwa. Ikiwa mwenye kueneza mafundisho ya uasi-imani hawezi kurudishwa awe na afya ya kiroho kwa kupakwa zeri ya Neno la Mungu wa upendo lakini kwa uthabiti, njia iliyobaki ya kulinda viungo vingine vya mwili ni kukikata kiungo hicho kisiwe sehemu ya mwili (kutenga na ushirika). (Linganisha Tito 1:10, 11.) Usiambukiwe na donda ndugu lenye kufisha la aina ya kiroho! Endelea kuwa na afya nzuri ya kiroho kwa kuepuka kuchafuliwa na mawazo ya uasi-imani. Tii shauri timamu lililo kwenye 2 Petro 3:17, 18: “Basi, wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu, mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu. Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo.”
18 Lakini tunaweza kujilindaje na uasi, imani? Tunaweza kudumishaje mioyo yetu katika kutokupokea fikira za uasi-imani? Maulizo hayo yatafikiriwa katika makala inayofuata.
Je! Unakumbuka?
◻ Huenda tukapotezaje faida za paradiso ya kiroho ya Yehova?
◻ Kwa sababu gani kusoma vichapo vya uasi-imani kunafanana na kusoma vitabu vya ngono chafu?
◻ Tunaweza kufanya nini tukiulizwa habari za madai fulani yaliyotolewa na waasi-imani?
◻ Kwa sababu gani mafundisho ya uasi-imani ni kama donda-ndugu?
[Picha katika ukurasa wa 12]
Wewe unatumia hekima ya kuharibu vitabu vya uasi-imani?