Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 12/1 kur. 4-6
  • Weka Akiba Sasa Katika Wakati Ujao Salama

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Weka Akiba Sasa Katika Wakati Ujao Salama
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kupima Akiba Yako
  • “Weka Akiba” Sasa!
  • Usalama Wako Ni Nini?—Ni Nyumba Yako?—Pesa Zako Banki? —Au Ni Kazi Yako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Unamtegemea Mungu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • ‘Tukiwa Hatuna Kitu Lakini Tukiwa na Vitu Vyote’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Kwa Nini Utimize Ahadi Zako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 12/1 kur. 4-6

Weka Akiba Sasa Katika Wakati Ujao Salama

KWA kutaja mambo waziwazi, kuna machache sana unayoweza kufanya ili ulinde raslimali zako. Ni kweli kwamba kutumia fedha zako kwa busara zaidi na kukopa mara chache sana huenda kukapunguza mkazo fulani. Lakini mambo mengi yenye kuupata uchumi hayako katika uwezo wa mkono wako kuyaongoza. Hata hivyo, kuna jambo unaloweza kufanya, ili kulinda amani yako ya akili na hali njema yako. Biblia inasema: “Hekima ni ulinzi, kama vile fedha ilivyo ulinzi; na ubora wa maarifa ni ya kwamba hekima humhifadhi yeye aliye nayo.”​—Mhubiri 7:12.

Hekima hiyo ni zaidi ya masomo ya kilimwengu. “Kwa kuwa [Yehova] huwapa watu hekima; kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.” (Mithali 2:6) Unaweza kupata hekima hiyo kwa kuweka raslimali katika funzo la Biblia. Jambo hilo linakuwaje “ulinzi”? Kwanza, maarifa ya Biblia yanakupa maoni mapya juu ya taabu ya kiuchumi ya wakati huu. Unapata kuthamini kwamba tunaishi katika ambazo Biblia inaita “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1-4) Mwishowe, mfumo huu wenye kuvuruga na wenye mchafuko utafagiliwa mbali katika siku ya hukumu ya Mungu. (2 Petro 3:12, 13) Na kama Mithali 11:4 inavyoonya, “Mali hazifaidii kitu siku ya ghadhabu.”

Unapopata kujua na kuthamini mambo hayo, unaepushwa na mengi ya mahangaiko yanayoletwa na kufuatia mambo ya kimwili yasiyofaa kitu. Hauna harakati za kuhifadhi vitu vya kimwili ulivyo navyo sasa, ukijua mali zinapita mbio-mbio. Wala huvunjiki moyo endapo huwezi kujipatia vitu vya raha vya hivi majuzi. “Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu; ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo.”​—1 Timotheo 6:7, 8.

Hata wale ambao wana “usalama” wa kifedha wanaweza kufaidika na hekima ya kimungu. Mtume Paulo aliendelea kusema hivi katika 1 Timotheo 6:17, 18: “Walio matajiri wa ulimwengu wa sasa uwaagize wasijivune, wala wasiutumainie utajiri usio yakini, bali wamtumaini Mungu atupaye vitu vyote kwa wingi ili tuvitumie kwa furaha. Watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema.” Hata katika siku za Biblia mali zilikuwa ‘zisizo yakini’ (zisizotegemeka). Kwa hiyo Wakristo walio matajiri walipaswa kutambua kwamba usalama wo wote unaowaziwa unaletwa na fedha ulikuwa udanganyifu tu. Walipaswa ‘kumtumaini Mungu.’

Hata hivyo, hiyo haikumaanisha kwamba maisha yangepasa yawe kujikalia tu, kuketi bila kufanya lo lote tukingojea “mwisho” uje. Walipaswa ‘kutenda mema, wawe matajiri kwa kutenda mema.’ Bila shaka hilo lilimaanisha kutumia wakati mwingi na nguvu. Na leo wengi wanaposikia kazi ikitajwa wanakimbia. Lakini namna gani wewe? Je! wewe una nia ya kufuata mwendo wa Biblia? ‘Sina hakika,’ lingeweza kuwa jibu la wengi. Inaelekea, kwanza ungependa kujua jinsi kufanya hivyo kungeweza kukufaidi wewe. Ni mambo gani yanayohusika? Je! kweli kweli wakati na jitihada yote inayohitajiwa inastahili? Ebu tutumie kanuni fulani za msingi za kuweka akiba ili tukusaidie kupata majibu yaliyo wazi.

Kupima Akiba Yako

Mambo yanayoweza kuleta hasara, mkopo anaoweza kupewa mtu, mataraja ya wakati ujao, na pia faida, ni mambo ambayo mfanyi-biashara mwenye busara atachunguza kabla ya kutia alivyo navyo katika mpango fulani. Hilo lingehusikaje juu ya kama unataka ‘kumtumaini Mungu’?

Kwanza, fikiria mkopo mzuri unamaanisha nini. Kwa msingi unadokeza kwamba mtu anatumainika, kwa kutegemea utendaji wa wakati uliopita. Kwa kuwaza kwa njia hiyo, mfumo wa kiuchumi uliopo wakati huu ungepewa mkopo ulio mdogo zaidi. Zaidi ya hayo, unaweza kuwatumaini kwa kadiri gani viongozi wa kidini na wa kisiasa?

Kwa upande mwingine, Mungu angekadiriwaje inapokuwa ni kutegemeka? Mwamuzi Yoshua alikuwa ametumia maisha yake yote akimtumikia Mungu. Miaka mingi ya kupiga guu kupitia jangwa kavu, kupigana na kuhukumu taifa lenye kichwa kigumu, yote hayo hayakudhoofisha tumaini lake kwa Mungu. Yeye alisema hivi kwa uhakika: “Angalieni, mimi leo ninakwenda njia ile waendayo watu wote wa ulimwengu; nanyi nyote mnajua mioyoni mwenu, na [nafsini] mwenu, ya kuwa halikuwapungukia ninyi hata neno moja katika mambo hayo mema yote aliyoyanena [Yehova], Mungu wenu, katika habari zenu; yote yametimia kwenu, hapana neno lo lote mlilopungukiwa.” (Yoshua 23:14) Yehova amesitawisha kumbukumbu la kuwa mwenye utumainifu ambao unapita sana ule wa tengenezo lo lote la kibinadamu. Kuweka akiba katika ahadi anayotegemeza kuna msingi imara kabisa.

Namna gani mambo yanayoweza kuleta hasara? Kwa kawaida sheria ni kwamba, ‘Kwa kadiri ambavyo akiba inaweza kuleta faida kubwa, ndivyo uwezekano wa wa kupata hasara unavyokuwa mkubwa.’ Sababu moja unajitia katika uwezekano kupata hasara kubwa unapotumaini tengenezo la kibinadamu ni kwamba mwanadamu mwenyewe ana uwezo wenye kipimo, uwezo wa kutangulia kuona ya mbele wenye kipimo na uzima wenye kipimo. Kwa kufaa Biblia inaonya hivi kwa upole: “Msiwatumainie wakuu, wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake. Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, siku hiyo mawazo yake yapotea.” (Zaburi 146:3, 4) Wale wanaotumaini ahadi za Mungu, hata hivyo, hawaelekei kamwe kupata hasara hizo. Akiwa Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote, Yehova ana uwezo usio na kipimo! Hakuna mtu anayeweza kuharibu kusudi lake. Wala hata kifo chenyewe hakiwezi kumzuia mtu asipate “faida” kutokana na “akiba” yake ya utumishi wa uaminifu, kwa maana Yehova anaahidi kufufua watumishi wake waaminifu ikiwa lazima.​—Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15.

Namna gani mataraja ya wakati ujao na “faida,” za kuchagua kumtumaini Mungu? Mtengeneza-sayari hii anaona huko mbele jambo lililo bora zaidi kwa dunia kuliko kupunguka kukubwa sana kwa thamani ya fedha, uchafuzi wa mazingira ulioenea sana, jeuri isiyozuilika na mashindano ya kuunda silaha yenye kwenda kasi. Yeye ameahidi, mahali pake, “kuwaharibu hao waiharibuo nchi.” (Ufunuo 11:18) Vita na silaha ‘zitakomeshwa.’ (Zaburi 46:9) Hakuna ye yote atakayefanya wakaaji waadilifu wa dunia kuwa na “hofu,” kwa maana vitisho vya jeuri na kifo vitakuwa mambo ya wakati uliopita. (Mika 4:4) Je! mtu anaweza kuwa na taraja zuri zaidi ya hilo kwa wakati ujao?

“Weka Akiba” Sasa!

Hata hivyo, kumbuka kwamba ni lazima ufanye kazi kwa bidii ili upokee baraka hizo. Itakugharimu wakati na jitihada. Lakini je, wakati ujao salama haustahilishi hilo? Kwa mfano, katika mfano wake mmoja Yesu alisema juu ya “mfanya biashara” mwenye kutaka kuweka akiba ya lulu nzuri. “Alipoona lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza alivyo navyo vyote, akainunua.” (Mathayo 13:45, 46) Mtu anayethamini ahadi ya Mungu ya Ufalme wa uadilifu atatenda kama mtu huyo katika mfano huo. Atauweka kwanza maishani mwake. Kwa ajili ya huo mtu anastahili kujinyima hivyo.​—Mathayo 6:33.

Kwa hiyo wewe utaweka akiba katika nini? Je! wewe utakuwa kama Waisraeli wa kale ambao walifuatia bure vitu vya kimwili badala ya faida za ibada ya Mungu? Wao walifanya kazi kwa bidii sana ili wawe na nyumba zao za anasa zenye mapambo. Hata hivyo, nabii Hagai aliwafananisha na mtu ‘anayepata mshahara na kuutia katika mfuko uliotoboka-toboka.’ (Hagai 1:4-6) Ebu wazia huzuni kubwa ya kugundua kwamba fedha zako ulizozichuma kwa bidii zimepotea kupitia mfuko wa pesa wenye kuvuja! Vitu vya kimwili leo hali moja na hiyo si hakika na vinapita mbio-mbio.

Kwa hiyo tunawasihi wote washike ahadi za Mungu na kumtumaini kabisa. Kwa kuendelea kujifunza Biblia kwa bidii na kwa kufuata mashauri yayo ya hekima huenda ukapata baraka bora zaidi, kutia uzima wa milele katika dunia iliyo paradiso! Hizo ndizo faida zinazopatikana kwa kuweka akiba sasa katika wakati ujao ulio salama ambao Mungu anaahidi katika Neno lake.​—Waefeso 3:20, 21.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Baada ya maisha ya utumishi wa utumainifu, Yoshua angewesa kusema hivi juu ya ahadi za Yehova: ‘Hapana neno lo lote lililopungukiwa’

[Picha katika ukurasa wa 6]

Kufuatia mali na kama ‘kupata mshahara na kuutia katika mfuko uliotoboka-toboka’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki