Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 6/1 uku. 10
  • Wenye Umoja Katika Kutangaza Neno la Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wenye Umoja Katika Kutangaza Neno la Yehova
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Umoja wa Tendo
  • Namna ya Kufanya Mambo ya Kitheokrasi
  • Kufurahia—Wakati Huo na Sasa
  • Kuangalia Mbele
  • Tengenezo la Mungu Linaloonekana
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Mnara wa Mlinzi Unaanza Kuchapwa Wakati Mmoja na Kiingereza Katika Lugha Nyingi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • “Tumefikia Kauli Moja”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Familia ya Yehova Hufurahia Muungano Wenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 6/1 uku. 10

Wenye Umoja Katika Kutangaza Neno la Yehova

“Mwe miongoni mwenu na maoni ya akili yale yale aliyokuwa nayo Kristo Yesu, ili kwa kupatana pamoja kwa kinywa kimoja mweze kumtukuza Mungu na Baba ya Bwana yetu Yesu Kristo.”​—WARUMI 15:5, 6, New World Translation.

1. (a) Mpango wa Yehova wa kufanya watu wake wawe na umoja ni nini? (b) Maandiko yanaonyesha nini kuhusu utaratibu wa kufanywa kuwa na umoja?

YEHOVA amewakusanya mashahidi wake katika umoja wa duniani pote wenye thamani. Hilo ni kupatana na mpango wa nyumba wa Mungu ambao mtume Paulo anaeleza kwenye Waefeso 1:10, NW: “Usimamizi katika utimilifu wa nyakati zilizowekwa, yaani, kuvikusanya tena vitu vyote pamoja katika Kristo, vitu vilivyomo mbinguni na vitu vilivyomo duniani.” Wale wa “kundi dogo” la Wakristo wapakwa mafuta watakaoenda mbinguni ndio wa kwanza kukusanywa na baadaye wale wa “mkutano mkubwa . . . wa kila taifa” wanaotazamia kuokoka waingie katika ‘dunia mpya’ yenye uadilifu ya ahadi ya Mungu.​—Luka 12:32; Ufunuo 7:3, 4, 9, 13-17; 21:1, 5.

2. Ni nini linalowezesha Mashahidi wa Yehova waseme “kwa kupatana pamoja”?

2 “Kwa kupatana pamoja”​—ndivyo mashahidi wa Yehova hao wanavyozungumza juu ya ujumbe wake wa Ufalme. Ni kwa sababu gani wanaweza kufanya hivyo? Ni kwa sababu, kote kote katika dunia yetu, wanaonyesha “maoni ya akili yale yale aliyokuwa nayo Kristo Yesu” alipokuwa angali duniani. Yeye hakuwa sehemu ya ulimwengu huu wenye kiburi. Badala yake, yeye alijinyenyekeza kufanya mapenzi ya Mungu na kusitawisha umoja mchangamfu, wa upendo kati ya wanafunzi wake. Huo ulikuwa ndio mwanzo wa kuunganishwa kwa kidunia kulikotofautisha Wakristo wa kweli katika karne zilizofuata.​—Wafilipi 2:5-8; Yohana 13:34, 35; 17:14.

3. (a) Kuna tofauti gani kubwa inayoonekana duniani leo? (b) Maandiko yanasaidiaje katika kuitambua jamii ya duniani pote ya Wakristo wa kweli?

3 Umoja huo wa tengenezo umefikia kiwango kilicho bora zaidi wakati wa hizi “siku za mwisho,” tofauti sana na migawanyiko inayoupata mfumo wa mambo wa Shetani, ambamo chuki na uvunjaji wa sheria vimeenea sana. (2 Timotheo 3:1-5, 13; Mathayo 24:3, 12) Hakujapata tena katika historia ya kibinadamu kuwa duniani pote, katika nchi 203, tengenezo ambalo lina upatano wa imani, kusudi na utendaji. Jamii hii ya duniani pote ya wanafunzi wa Yesu yaweza kutambuliwa kwa tunda inalozaa.​—Yohana 15:8; Waebrania 13:15; Wagalatia 5:22, 23.

Umoja wa Tendo

4. (a) Ni mabishano gani yaliyotokea katika kundi la karne ya kwanza? (b) Kulingana na Matendo 15:1-6, ni tendo gani la kitheokrasi lililoanzishwa?

4 Tunaonyeshwa umoja wa tendo katika tengenezo la Yehova kwenye Matendo sura ya 15. Ebu wazia ukiona mkusanyiko wa mashahidi wa Yehova waliokomaa​—wale mitume 12, wanaume wazee wengine wa kundi la Yerusalemu na Paulo na Barnaba, wazee kutoka kundi la Antiokia. Katika Antiokia, na pia katika Yerusalemu, waongofu fulani kati ya Wayahudi wanasisitiza kwamba watu wa mataifa ni lazima watahiriwe na ni lazima waishike Torati ya Musa ili waokolewe. Kwa hiyo mitume na wanaume wazee “wakakusanyika wapate kulifikiri neno hilo.”​—Matendo 15:1-6.

5-7. (a) Kulikuwako “kubishana sana” katika maana gani? (b) Ni ushuhuda gani uliotolewa? (c) Maandiko yalitumiwaje ili kuthibitisha jambo hilo? (d) Ni upambanuzi gani wa ukomavu aliofanya Yakobo, ukaelekeza kwenye uamuzi gani wa mwisho? (e) Ni tendo la namna gani lililofuata?

5 Tatizo hilo linazungumzwa vilivyo, wanaume hao waliojitoa wakieleza juu ya mambo yanayofaa na yasiyofaa ya jambo hilo. Hawajatangulia kukata kauli. Wana nia ya kuchunguza jambo hilo pande zote. Kuna “kubishana sana,” (NW) lakini kwa wazi wanadumisha utaratibu mzuri na kusikiliza kwa heshima maoni ya mmoja na mwenzake. Mtume Petro anashuhudia uhakika wa kwamba Mungu amewapa roho takatifu watu wa mataifa wasiotahiriwa. Kwa hakika huo ukiwa ni ushuhuda wenye nguvu kwamba tohara ya mwili si takwa tena kwa wale wanaookolewa. Barnaba na Paulo wanaunga mkono ushuhuda huo, wakisimulia mambo mengi mazuri ajabu ambayo Mungu ametimiza kupitia huduma yao kwa mataifa.​—Matendo 15:7-12.

6 Kisha, Yakobo anatumia maneno ya Maandiko ili kuunga mkono hoja ambayo ndiyo kwanza tu imetoka kutolewa. Anaeleza kwamba Amosi 9:11, 12 ni andiko linaloelekeza kwenye kurudishwa kwa kibali ya kimungu chini ya Daudi Mkuu Zaidi, Yesu Kristo, na kuhusu Yehova kuonyesha fadhili zisizostahilika kwa “mataifa yote ambao jina [lake] limetajwa kwao.” Yakobo haoni sababu ya kuwataabisha waongofu kutoka mataifa kwa kusisitiza kwamba watahiriwe na kushika amri zote zilizomo katika Torati ya Musa. Lakini, kuna mambo machache ya lazima: Ni lazima wajiepushe na ibada ya sanamu, kutotumia damu katika njia yo yote na kutokosa adili za ngono.​—Matendo 15:13-21.

7 Baraza linaloongoza katika Yerusalemu linafikia uamuzi wa kauli moja. Linawatuma wajumbe mpaka kwenye kundi la Antiokia wakiwa na barua inayomalizika kwa kitia-moyo hiki: “Ikiwa kwa uangalifu mnajiepusha ninyi wenyewe na vitu hivyo, mtafanikiwa. Afya njema kwenu!”​—Matendo 15:22-29, NW.

Namna ya Kufanya Mambo ya Kitheokrasi

8. (a) Baraza Linaloongoza la kisasa linaongozwaje kufanya maamuzi? (b) Ni baadhi ya mambo gani ambayo yameelezwa wazi hivi karibuni?

8 Katika nyakati za kisasa, Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, linalowakilisha “mtumwa mwaminifu mwenye akili” wa Bwana duniani, linafuata kielelezo icho hicho cha mitume. (Mathayo 24:45-47) Kwa hiyo, ujuzi wa Kikristo, uongozi kutoka Biblia, na miongozo ya roho ya Yehova yanaelekeza kikundi hicho cha Mashahidi wapakwa mafuta wafikie kauli za kitheokrasi kuhusu mambo ya kuhangaikiwa sana na kundi. Kwa mfano, katika miaka ya karibuni Baraza Linaloongoza limefuata namna ya kufanya mambo ya kitheokrasi kwa kufafanua mambo kama vile maoni ya Biblia kuhusu “wahudumu” (maminista), dhamiri tuliyopewa na Mungu, kuchukua silaha hatari, na kadiri ambayo sehemu za unabii wa Isaya zinahusu Paradiso ya duniani ya wakati ujao.​—Linganisha Yohana 14:26; 1 Wakorintho 2:10.

9. Ni namna gani ya kufanya mambo ambayo wazee wanapaswa kufuata katika kushughulikia matatizo leo?

9 Namna ya kufanya mambo ya Matendo sura ya 15 ni lazima pia ifuatwe na wazee wa kundi katika kushughulikia matatizo leo. Kwanza, tatizo na mambo ya uhakika yanayohusika yanapasa kuelezwa. Kisha, mashahidi wenye kutegemeka watoe ushuhuda wenye mambo ya uhakika, ulio wazi, unaohusu jambo hilo. Maandiko yatafutwe ili kuona maoni ya Yehova, na kutumia pia msaada unaopatikana katika vichapo vya Sosaiti yetu. Kwa njia ya sala mfanye kazi kufikia uamuzi wa kauli moja, kwa kupatana na fundisho la Neno la Yehova, uamuzi utakaofaidi kundi.​—Isaya 48:17; 1 Wakorintho 14:33.

Kufurahia—Wakati Huo na Sasa

10. (a) Kama ilivyokuwa katika kundi la karne ya kwanza maamuzi ya kitheokrasi yanapasa yawe na matokeo gani kwetu leo? (b) Matukio ya kisasa yameongozaje kwenye kutiwa nguvu na kuongezwa kwa watu wa Mungu?

10 Waliposikia uamuzi wa baraza linaloongoza, washiriki wa kundi katika Antiokia ‘walifurahi kwa ajili ya kitia moyo hicho.’ (NW) Vivyo hivyo leo, Mashahidi wa Yehova wanafurahi kujua maamuzi ya kitengenezo na mafafanuzi ya mafundisho yanayoendeleza afya ya kiroho ya watu wa Mungu na kusogeza mbele kazi ya Yehova. (Linganisha Tito 2:1.) Lakini si lazima tena Baraza Linaloongoza liandike barua za maagizo kwa mkono na kuzieneza kupitia wajumbe wenye kusafiri kwa miguu. Njia za kisasa za uchukuzi na vifaa vya uchapaji katika matawi ya Sosaiti yetu zaidi ya 30 duniani pote yamefanya iwezekane kupeleka “habari njema za neno la Yehova” (NW), kwa mamilioni ya watu wa Mungu kwa wakati mfupi sana. Jambo hilo linafanywa hasa kupitia gazeti Mnara wa Mlinzi. Kwa hiyo, makundi ulimwenguni pote yanaendelea ‘kutiwa nguvu katika imani na hesabu yao kuongezeka kila siku.’​—Matendo 15:30-16:5.

11. Yehova ametumiaje Mnara wa Mlinzi kutimiza Isaya 30:18-21?

11 Wale ambao wamesoma Mnara wa Mlinzi kwa miaka mingi wamefurahia kuona mwenezo walo wenye kuongezeka. Katika miaka 105 ya uchapishaji, mwenezo huo ulipanuka kutoka nakala 6,000 katika Kiingereza mara moja kwa mwezi ukawa nakala 11,150,000 katika lugha 102, chapa zote kubwa-kubwa zikiwa mara mbili kwa mwezi. Hakika, Mnara wa Mlinzi umetumiwa kwa njia kubwa na Mfundishaji Mkuu wetu, Yehova Mungu, katika utimizo wa ahadi: “Heri wote wamngojao. . . . Masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.”​—Isaya 30:18-21.

12. (a) Ni kwa nini tuna sababu zaidi ya kufurahi? (b) Mpango huo mpya unapasa kutufaidije?

12 Sasa kuna sababu zaidi ya kufurahi. Kuanzia na kuendelea katika mwaka wa 1985, Mnara wa Mlinzi linachapishwa mambo yale yale katika wakati ule ule, katika lugha 23!a Chapa zote hizo zina umbo lile lile la jalada. Zina mfululizo ule ule wa makala za utangulizi na makala zile zile za kujifunza. Jambo hilo linawezesha programu ya ‘ulishwaji’ wa mambo yale yale ambayo itawafanya watu wa Yehova wawe na umoja katika kukua kiroho mpaka ‘tuufikie umoja wa imani.’ Linapasa litusukume hata zaidi, ili ‘kwa kupatana pamoja kwa kinywa kimoja tuweze kumtukuza Mungu na Baba ya Bwana yetu Yesu Kristo.’​—Waefeso 4:13; Warumi 15:6.

13. (a) Programu hiyo ni kubwa kadiri gani? (b) Kwa hiyo andiko la 1 Wakorintho 1:10 laweza kutumiwaje?

13 Gazeti hili linapokuwa mkononi mwako kwenye funzo la kundi la kila juma la Mnara wa Mlinzi, je, haikusisimui kujua kwamba sehemu kubwa ya ndugu zako ulimwenguni pote watakuwa kwa umoja wakila chakula kile kile cha kiroho siku ile ile? Ndiyo, jambo hilo litakuwa hivyo katika Amerika yote ya Kaskazini na Kusini, sehemu kubwa ya Ulaya, katika Japani na katika sehemu nyingi za Afrika ya upande wa kusini! Inakadiriwa kwamba tayari asilimia zaidi ya 90 ya wale wanaohudhuria funzo la Mnara wa Mlinzi duniani pote​—watu 2,500,000 hivi kila juma​—sasa wanashiriki mpango huu wa ‘ulishwaji’ wa wakati ule ule. Pamoja hao, ‘wanafanywa wenye umoja ifaavyo katika akili ile ile na katika namna ile ile ya kuwaza.’ (1 Wakorintho 1:10, NW) Kwa kadiri hali zinavyoruhusu, lugha nyingine zitaongezwa.

14. Jamaa zitafaidikaje?

14 Kufikia wakati huo, kwa sababu ya tofauti za lugha, washiriki wa jamaa moja huenda wakawa walikuwa wameachana miezi mingi katika kujifunza makala fulani za Mnara wa Mlinzi. Lakini sasa wanaweza kuwa wenye umoja katika jambo hilo. Katika jamaa zinazozungumza lugha mbalimbali, wazazi watakuwa wenye utayari zaidi kutimiza agizo la Waefeso 6:4 na 2 Timotheo 3:14, 15.

15. (a) Katika huduma yetu ya peupe, sasa tunaweza kufanyaje kwa kupatana na Isaya 52:8, 9? (b) Ni jambo gani lililofanywa liwezekane mapema 1985, na kwa ajili ya wakati ujao?

15 Fikiria, pia, huduma yetu ya peupe pamoja na magazeti. Katika njia hiyo ya ziada, wahubiri wa Ufalme duniani pote sasa wanaweza ‘kupaza kwa umoja sauti zao pamoja’ wanapotolea watu wote wa ulimwengu ujumbe unaofanana wakati ule ule. (Isaya 52:8, 9) Katika kutoa ushuhuda wa barabarani katika maeneo ya watu wanaozungumza lugha mbalimbali, wahubiri wanaweza kuonyesha magazeti yenye kichwa kile kile cha jalada katika lugha mbili au zaidi. Ebu fikiria hilo! Wakati wa sehemu ya mapema ya mwaka wa 1985, wahubiri wa Ufalme duniani pote walikuwa wakitoa ushahidi wenye kuamsha, wa umoja kuhusu Har–Magedoni! Kwa wakati wake, huenda Yehova akaelekeza watu wake wafanye matangazo mengine yenye nguvu ya umoja ulimwenguni pote wanapotumikia ‘kando ya mmoja na mwenzake kwa ajili ya imani ya habari njema.’ (Wafilipi 1:27, NW) Uchapishaji wa wakati ule ule wa Mnara wa Mlinzi katika lugha nyingi utafanya iwezekane kufanya matangazo hayo.​—Linganisha Danieli 11:44.

Kuangalia Mbele

16. (a) Mnara wa Mlinzi unatuambia nini kuhusu utendaji wa magazeti kwenye kurasa 8, 9, na 21? (b) Ni kwa nini watu wanahitaji magazeti yetu leo?

16 Wakati wa mwaka wa 1984, Mashahidi wa Yehova waligawanya sana magazeti-menzi Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Utendaji huo umebarikiwa sana na Yehova, kama inavyoonyeshwa na takwimu zilizochapishwa kwenye kurasa 8, 9 na 21 katika gazeti hili. Ulimwenguni pote, ugawaji wa magazeti yetu wakati wa mwaka 1984 uliongezeka kwa asilimia 11.1 kufikia jumla kuu ya 287,358,064, nayo maandikisho ya magazeti yakaongezeka kwa asilimia 3.2 kufikia 1,812,221. Hakuna shaka kwamba watu wengi zaidi na zaidi wanataka kujua ni kwa nini mataifa yana huzuni nyingi, “wasijue njia ya kutokea.” (Luka 21:25, 26, NW) Wazazi wanataka watoto wao wawe na wakati ujao wenye furaha​—jambo bora zaidi ya dunia iliyoteketezwa na vita ya nyukilia. Magazeti yetu yanatoa tumaini lililo hai!—Mathayo 12:18, 21; Warumi 15:4.

17. Magazeti yetu yatatusaidiaje tumpinge Ibilisi?

17 Basi, namna gani juu ya mwaka wa 1985? Ujumbe uliomo katika Mnara wa Mlinzi na Amkeni! unakuwa wenye kutaja mambo wazi zaidi na zaidi. Hilo ni jambo la kutazamiwa wakati siku za mwisho za ulimwengu wa Shetani zinapomalizika. (Ufunuo 12:12) Usikosee! Ibilisi angependa kutuvunja moyo tusishiriki kwa ukawaida katika utumishi wa Yehova. Ndiyo, Shetani angependa kututenganisha na baraza la watu wa Mungu na utendaji walo, na hivyo atumeze. (1 Petro 5:8) Lakini tunaweza kumpinga kwa kukutana kwa ukawaida ili kutwaa maarifa sahihi, na kwa kutumia maarifa hayo yaliyoongezeka kumtumikia Yehova.​—Waefeso 6:11, 14-16; Wakolosai 1:9-11.

18. (a) Daraka lako ni kubwa kadiri gani ukiwa mhubiri wa Ufalme? (b) Tunaweza kutumiaje shauri la Warumi 12:10-11 na 15:5, 6?

18 Je! wewe ni mhubiri wa Ufalme? Ikiwa ndivyo, una cheo kikubwa katika sosaiti ya kitheokrasi ya kisasa. Ukiwa Mkristo aliye wakfu, huenda ukawa na madaraka mengine kundini. Hata hivyo, ili uishi kwa kupatana na jina la Yehova, ni lazima uwe mhudumu (minista) mwenye bidii shambani. Tukiwa wenye umoja katika upendo wa kidugu na tukiwa na shauku nyororo kwa mmoja na mwenzake, sisi sote na tuendelee kuwaka kwa ile roho ‘tunapomtumikia Yehova.’ (Warumi 12:10, 11) Hata tupatwe na mikazo gani kutoka kwa Shetani na ulimwengu wake, ni lazima tuendelee tukiwa mwili mmoja, ndiyo, ‘kwa upatano mmoja na kwa kinywa kimoja,’ kumtukuza Yehova kwa kujulisha makusudi yake ya Ufalme.

19. (a) Tunaweza kushindanaje kwa kufanikiwa na mateso na matatizo mengine? (b) Andiko la Sefania 3:8, 9 linatupa shauri gani?

19 Wengi wetu tunalazimika kushindana na mateso au maeneo yasiyoitikia kuhubiri kwetu. Lakini, na tuendelee kuonyesha maoni yale yale ya akili aliyokuwa nayo Kristo Yesu. (Yohana 16:33; 1 Petro 4:1, 2) Tukiwa mwili wenye umoja na tuonyeshe uhodari wa kweli​—nguvu za kiroho za kindani zinazovumilia na zisizoshindwa na mkazo. (Zaburi 27:14; Wafilipi 1:14) Na tusilegeze mikono kamwe katika kutafuta wenye mfano wa kondoo. Na tuendelee ‘kumtazamia’ Yehova na siku yake ya kutoza hesabu, tukimtumikia bega kwa bega tunapoliitia jina lake na kusema “lugha safi” ya ukweli.​—Sefania 3:8, 9.

20. (a) Tunaweza kupataje furaha ya kweli? (b) Andiko la Isaya 11:6-9 limeona utimizo gani wa kutokeza?

20 Kwa umoja, wote wanaomtukuza Mungu ‘wavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.’ (Waefeso 4:24) Jambo hilo linatokeza furaha ya kweli. Linaonyeshwa katika Isaya 11:6-9, andiko ambalo linasimulia paradiso ya kiroho iliyopo sasa kati ya watu wa Yehova waliorudishwa. Ni amani na upatano kama nini! Lo! hakuna pupa, hakuna tabia-tabia za nyutu zenye kuumiza! Ukiwa umalizio wa masimulizi hayo ya paradiso, tunaona maneno haya: “Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa na kumjua [Yehova], kama vile maji yanavyoifunika bahari.” ‘Mlima mtakatifu’ wa Yehova wa ibada ya umoja umeimarishwa leo katika dunia yote. Kwa nini? Kwa sababu Yehova amewasukuma mashahidi wake walitukuze jina lake ‘kwa upatano mmoja na kwa kinywa kimoja.’ Kwa hiyo “dunia,” shamba la kiroho la watu Wake, limejazwa na ‘kumjua Yehova.’

21. Ni kwa nini tunapaswa kuyaeneza magazeti yetu kwa kadiri kubwa iwezekanayo?

21 Sisi, katika nguvu ambazo Yehova anatoa, na tugawanye Mnara wa Mlinzi na gazeti-jenzi lake Amkeni! kwa kadiri kubwa iwezekanayo. Na tufanye hivyo tukiwa na tumaini kwamba miisho yote ya dunia na jamaa za mataifa yote, zikiwakilishwa, ‘zitamrejea Yehova.’​—Zaburi 22:27; Ufunuo 15:4.

[Maelezo ya Chini]

a Lugha hizo ni: Afrikaans, Danish, Dutch, English, Finnish, French, German, Italian, Japanese, Norwegian, Portuguese, Spanish, Swedish, na Thai; lugha za Kiafrika: Sepedi, Sesotho, Tsonga, Tswana, Venda, Xhosa, na Zulu; na lugha mbili katika nchi ambazo kazi ya Mashahidi wa Yehova imezuiwa.

Maswali ya Kurudia​—

◻ Kundi la karne ya kwanza lilikuwa likitendaje?

◻ Ni faida gani zinazopasa kutokana na uchapishaji wa wakati ule ule wa Mnara wa Mlinzi?

◻ Ni jitihada gani nzuri ya kutoa magazeti iliyofanywa mwaka 1984?

◻ Tunaweza kufanikiwaje kiroho, hata nyakati za jaribu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki