Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 5/1 uku. 21
  • Thawabu kwa Uaminifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Thawabu kwa Uaminifu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Habari Zinazolingana
  • “Mungu Hana Upendeleo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Upendo Wafanya Jamaa Ziwe na Umoja
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Mke Anayependwa Sana
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • “Neno la Mungu Likaenea”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 5/1 uku. 21

Ripoti ya Watangazaji Ufalme

Thawabu kwa Uaminifu

ILIKUWA katika Italia kwamba, miaka 15 iliyopita, Bi. B​—, aliyekuwa wakati huo na umri wa miaka 15, alipata kuujua ukweli. Hata hivyo, yeye hakufanya maendeleo, kwa hiyo akaolewa na mtu asiye mwamini. Ingawaje, mbegu za ukweli zilibaki moyoni mwake na karibu mwaka mmoja uliopita yeye alikubali funzo la Biblia pamoja na mmoja wa Mashahidi wa Yehova na akaanza kuhudhuria mikutano. Mume wake alikuwa akipinga vikali na akatisha kumwondosha nyumbani. Mume huyo alikuwa akimpiga sana sana hata mwanamke huyo akahitaji matibabu. Jioni moja mume huyo aliingia kwa nguvu nyingi ndani ya Jumba la Ufalme wakati wa mkutano mmoja, akampiga ndugu mmoja, akakivunja kioo mlangoni, na kupiga kelele kwa hasira nyingi.

Mwanamke yule aliporudi nyumbani, alipata kwamba mumeye alikuwa amemfungia nje. Bila kupoteza ushujaa wake, akaenda kwenye kituo cha Carabinieri (polisi) kuwajulisha lililokuwa limetukia na ndipo akaenda kulala kwenye nyumba ya shangazi mmoja. Baada ya siku mbili mume wake akamruhusu aje nyumbani.

Mume yule anajulikana sana mjini. Alianza kuwalaani Mashahidi wa Yehova peupe, akisema kwamba wao walikuwa wameharibu jamaa yake. Katika shughuli hiyo ya kupinga Mashahidi, aliungwa mkono na viongozi wa kidini. Padri mmoja alifanya mpango ili vibandiko viandikwe maneno haya: “MASHAHIDI WA YEHOVA: Msiisumbue amani ya jamaa hii. ASANTENI!” na akaagiza vibandiko hivyo viwekwe juu ya milango mjini. Kila mtu alikuwa akiongea juu ya Mashahidi wa Yehova na kuwafanya wawe ndiyo sehemu kuu ya dhihaka na madharau yao. Ijapokuwa hivyo, akina ndu-gu walifanya ushujaa wakasonga mbele katika huduma yao wakiwa na juhudi nyingi zaidi kuliko hapo kwanza. Jamaa zilizo nyingi hazikutaka vibandiko vile milangoni pao. “Wavulana fulani, waliotumwa na padri, walipewa lira 100 kwa kuvibandika milangoni,” ikaripotiwa.

Wakati huo, Bw. B​——​akamjulisha mke wake kwamba angepaswa kuondoka nyumbani, maadamu yeye alikuwa tayari amechukua hatua za mtengano wa kisheria. Lakini mambo yalikuwa yakianza kubadilika katika mji huo. Kituo cha redio cha mahali hapo kilitangaza programu moja, na mweleza-habari akaeleza kisa kile kuwa “mbinu isiyopendeza, ya kukosa adabu.” Wakati wa programu, ndugu zetu walieleza kwamba jamaa nyingi zilibandikiwa vibandiko vile bila kupenda. Jambo hilo lilithibitishwa na uhakika wa kwamba vilibandikwa wakati wa usiku hata juu ya milango fulani ya Mashahidi wa Yehova na za jamaa zilizokuwa zikikaribisha ziara zao. Mweleza-habari yule wa redio aliwasifu Mashahidi wa Yehova na kusema kwamba wao ni watu “wenye uungwana mwingi sana, na wao wanajiendesha kwa fadhili nyingi kabisa.”

Mwishowe, wakati ukaja wa mume na mke yule kuonekana mbele ya hakimu ili kuanzisha mtengano wa kisheria ambao mume aliuomba. Hakimu alimsifu Bi. B​— kwa tamaa yake ya kutokutaka kutengana, na walipokuwa wakingojea hatua za kisheria, yeye akampa mwanamke yule ulinzi wa watoto. Wangeweza kuendelea kuishi katika nyumba yao, na mume wake angepaswa kumpa lira 250,000 kwa mwezi. Mume alikinza jambo hilo, akisema: “Nyumba ni mali ya mama yangu, na mke wangu hawezi kukaa humo.” Hakimu akajibu: “Wewe unataka kuwa mume na bwana-mkubwa, mke wako analazimika sikuzote kusema ndiyo, na kwa safari moja yeye alisema hapana, hivyo ukauvuruga-vuruga mji wote. Kama mke angalikuwa si mwaminifu kwako, ningaliweza kufahamu, lakini kwa sababu anafuata imani moja badala ya nyingine, hiyo si taabu yako.”

Bi. ​——​ sasa anamtumikia Yehova kwa furaha. (Mathayo 5:10) Watu wa mji huo wamebadili mwelekeo wao, na mazungumzo mazuri ajabu ya Kibiblia yanatukia. Watu wanakubali kwamba si Mashahidi wa Yehova wanaosumbua amani ya kijamaa. Ikiwa kungali kuna vibandiko juu ya milango, havina maana yo yote tena.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki