Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 6/1 kur. 26-27
  • Kufurahi Pamoja na Darasa la 82 la Gileadi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufurahi Pamoja na Darasa la 82 la Gileadi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Habari Zinazolingana
  • Wamisionari Zaidi kwa Ajili ya Mavuno ya Duniani Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kuhitimu kwa Darasa la Gileadi la 83 Pindi ya Kisikukuu Kweli Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Makao Mapya kwa Ajili ya Shule ya Umisionari ya Gileadi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Mfurahieni Yehova na Kushangilia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 6/1 kur. 26-27

Kufurahi Pamoja na Darasa la 82 la Gileadi

“SISI SI Wakristo wa hali nzuri ya hewa. Tunafurahi tu kuwa hapa.” Mwenyekiti alifungua mkutano wa pekee wa siku nzima kwa maneno hayo katika Jumba la Kusanyiko la New Jersey la Mashahidi wa Yehova Jumapili, siku ya kwanza ya Machi. Nje, kulikuwa na mvua nzito. Ndani, ilikuwa siku ya kuhitimu kwa wanafunzi 24 wa darasa la 82 la Gileadi. Akiangalia nyuso zenye furaha za wanafunzi, mwenyekiti Theodore Jaracz wa Baraza Linaloongoza aliendelea kusema: “Ni wazi kwamba wao wana shauku na furaha kuhusu matarajio yao. Kwa kuwa Biblia inasema ‘furahini pamoja na watu wanaofurahi,’ nina uhakika kwamba sisi sote tunahisi ivyo hivyo.” Makofi yaliyopokea maelezo hayo yalitoa ushuhuda kwamba watu wote 4,557 waliohudhuria walikubaliana nayo.

Msemaji wa kwanza kwenye programu alikuwa John Barr, ambaye pia ni mshiriki wa Baraza Linaloongoza. Akitumia sana maneno kutoka Zaburi 104, Ndugu Barr alionyesha kwamba Yehova hakuumba kila kitu tu, chenye uhai na kisicho na uhai, bali pia aliumba mahali pa kila kiumbe kukaa. Akaendelea kusema: “Sasa, mnapoenda kwenye mgawo wenu, fikirini hivi: ‘Yehova ameniweka hapa.’ Msisahau hilo kamwe.”

Aliyefuata kuzungumza alikuwa mshiriki wa halmashauri ya Mashamba ya Mnara wa Mlinzi, John Stuefloten. Yeye aliwakumbusha wanafunzi: “Mithali inatuambia sisi: ‘Mwelimishe mwenye hekima, naye atazidi kuwa na hekima.’” (Mithali 9:9) Kwa miezi mitano, wanafunzi walikuwa wamepewa chakula kinono cha kiroho. Bila shaka, katika siku hii ya kuhitimu walihisi kuwa wameshiba. “Lakini,” msemaji akasema, “mmeanza sasa hivi!” Yeye aliwatia moyo wanafunzi waendelee kukua katika hekima na rehema ili waweze kuwasaidia wengine katika njia nzuri.​—Mithali 3:27.

George Gangas wa Baraza Linaloongoza alifuata akiwa na maneno yaliyochaguliwa vizuri juu ya furaha. Yeye aliwakumbusha wahitimu kwamba wao wanamtumikia “Mungu mwenye furaha” na akatangaza: “Ninyi mtapata furaha katika migawo yenu katika nchi za kigeni.” Kwa sababu gani? “Kwa sababu Yehova anawapeleka ninyi ili mwokoe watu kutoka utumwani.”

George Couch wa halmashauri ya makao ya Betheli ya Brooklyn alizungumza juu ya hangaiko. Yeye alikiri kwamba hangaiko halikuwa jambo geni kwa wanafunzi hao. Miito ya ushindani ya kuja Gileadi, kuishi katika Betheli ya Brooklyn, na kuhubiri katika Mji wa New York, yote hayo yalisababisha hangaiko fulani. Sasa wanafunzi walikuwa na wasiwasi kuhusu migawo yao ya umisionari. Lakini hangaiko la kiasi si adui. “Hangaiko linaweza kusaidia kutuchochea tujitahidi kwa uwezo wetu wote,” akaeleza Ndugu Couch, naye akawatia moyo wanafunzi wamtumaini Yehova na kujitahidi kwa uwezo wao wote katika migawo yao.

Aliyefuata jukwaani alikuwa mwalimu wa shule Jack Redford. Yeye alionya dhidi ya kuchambua-chambua bila haki. Akitaja mifano ya Kibiblia ya hukumu za haraka-haraka zilizosababisha matatizo baadaye, yeye aliyatumia maneno ya Yesu: “Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi.” (Mathayo 7:1) Darasa la 82 lilimwakilisha Mungu wa upendo. Wanafunzi hao walikuwa wakipelekwa kwenye migawo yao ili kuonyesha hisia-mwenzi, wala si kuchambua-chambua.

Mwalimu wa Gileadi Ulysses Glass aliyatumia maneno haya ya mithali ya Biblia: “Si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani.” (Mhubiri 9:11) Matokeo ya jambo sikuzote hayategemei uwezo mbalimbali tuliozaliwa nao. Katika kazi ya misionari, jambo linalosaidia zaidi ni imani na kuwa na nia ya kukubali mwito wa ushindani. Ndugu Glass alilisifu darasa la 82 kwa kuwa imara, wenye kutegemeka, na wenye uthabiti wa kutenda bila ugeugeu. Sifa kama hizo zitawasaidia sana.

Msemaji wa mwisho asubuhi hiyo, msimamizi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Frederick Franz, alitangaza kwamba kuhitimu kwa darasa la 82 kulishuhudia imani ya wale walioianzisha shule huko nyuma wakati hali zilipokuwa mbaya katika siku za Vita ya Ulimwengu ya Pili. Yeye alisema juu ya jina Gileadi, akieleza kwamba katika Biblia neno hilo linamaanisha “Rundo la Ushuhuda.” (Linganisha Mwanzo 31:43-53, NW.) Wamisionari wa Gileadi wanaoendelea kwa uaminifu katika migawo yao wanatumikia kama rundo la ushuhuda. Wao ni ushuhuda ulio hai kwa ajili ya ukweli.

Ndipo wanafunzi walipopokea shahada zao, na asubuhi hiyo ikamaliziwa kwa kusoma barua ya shukrani kutoka darasa la 82. Wanafunzi waliandika kwamba ‘baraka ya Yehova ndiyo inayotajirisha.’ Kwa sababu ya hayo, wao walisema, “Yehova ametufanya sisi tuhisi kama watu 24 walio matajiri kupita wote duniani!”​—Mithali 10:22, NW.

Alasiri, baada ya Funzo la Mnara wa Mlinzi lililofupishwa, wanafunzi walionyesha programu yenye kupendeza sana. Ilimalizia kwa maneno ya uthamini wenye kutoka moyoni kwa wazazi wao, ambao kwa kutokuonyesha ubinafsi na kwa kutoa utegemezo waliwaruhusu watoto wao waondoke wakawe wamisionari.

Programu ya wanafunzi ilifuatwa na utoaji wa mchezo wa kuigiza wa wakati wake, na baada ya huo mwenyekiti, Theodore Jaracz, akatoa maelezo fulani ya mwisho. Nao ulikuwa mshangao ulioje ambao Sosaiti ilikuwa imeweka akiba kwa ajili ya dakika hizo za kumalizia! Msemaji alitangaza kwamba karibuni Sosaiti itafungua shule mpya, Shule ya Mazoezi ya Kihuduma, kwanza kwa ajili ya mazoezi ya wazee waseja na watumishi wa huduma walio waseja. Wote walitega sikio sana wakati Ndugu Jaracz alitangaza mojapo la matakwa ya kuhudhuria shule mpya hiyo: Nia ya “kutumikia mahali po pote ambapo pana uhitaji katika shamba la ulimwenguni pote.”

Makofi ya shauku yalipokea habari hizo kuhusu shule mpya hiyo. (Habari zaidi kuihusu zimetolewa katika makala inayofuata.) Ndipo programu ilipomalizika kwa wimbo na sala ya kumshukuru Yehova. Ndipo kila mtu akaenda nje kwenye jioni yenye mawingu-mawingu katika mji huo wa New Jersey. Bado kulikuwa na mvua kidogo angani, lakini ni wachache waliojali. Mioyo yote ilikuwa ingali ikifurahi pamoja na darasa lenye kuhitimu la 82 la Gileadi.

[Picha katika ukurasa wa 26]

Wahitimu wa Darasa la 82 la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi

Katika orodha iliyopo chini, mistari imepewa namba kuanzia mbele mpaka nyuma, na majina yameorodheshwa kuanzia kushoto mpaka kulia katika kila mstari.

(1) Gish, L.; Evans, E.; Dean, S.; Hanson, R.; Suomalainen, A.; DuBose, D.

(2) Wallenberg, P.; Wallenberg, M.; Bauer, O.; Suomalainen, H.; Taylor, B.; DiStefano, G.

(3) Scott, K.; Evans, M.; Taylor, A., Jr.; Lindby, J.; Hanson, C.; Holmkvist, M.

(4) Sampson, T.; Gish. T.; Ball, D.; DuBose, J.; Dean, T.; Scott, D.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki