Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 6/1 kur. 21-23
  • Makao Mapya kwa Ajili ya Shule ya Umisionari ya Gileadi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Makao Mapya kwa Ajili ya Shule ya Umisionari ya Gileadi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Gileadi Yahama Brooklyn
  • Darasa la 86 Lahitimu
  • Shule ya Gileadi—Ina Umri wa Miaka 50 na Yaendelea Kufanikiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Wamisionari Zaidi kwa Ajili ya Mavuno ya Duniani Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Shule ya Gileadi Yatuma Darasa Layo la 100
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Darasa la 84 la Gileadi Laishi Kulingana na Matarajio!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 6/1 kur. 21-23

Makao Mapya kwa Ajili ya Shule ya Umisionari ya Gileadi

KATIKA FEBRUARI 1, 1943, Nathan H. Knorr, msimamizi wa hapo kwanza wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti, alitolea darasa la kwanza la shule mpya hotuba ya kufungua. Aliwaeleza wale wanafunzi mia moja kwamba “si kusudi la [shule] hii kuwatayarisha nyinyi muwe wahudumu walioagizwa rasmi. Tayari nyinyi ni wahudumu na mmekuwa watendaji katika huduma kwa miaka mingi. . . . Mtaala wa funzo . . . ni kwa kusudi pekee la kuwatayarisha muwe wahudumu wenye uwezo zaidi. Kufikia leo hii Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi huendelea kuzoeza wahudumu kwa ajili ya kazi ya misionari katika nchi za kigeni.

Huko nyuma katika 1943, Shule ya Gileadi ilikuwa katika jimbo la Finger Lakes la Mkoa wa New York. Gileadi ikabaki huko kwa miaka 17. Kisha, katika 1961, ikapelekwa Brooklyn. Kwa kusudi gani? Sikuzote mtaala wa mafunzo ya Gileadi umekusudiwa utimize mahitaji ya tengenezo. Uhitaji wa kusitawisha na kupanga vizuri zaidi kitengenezo vifaa vya tawi kotekote duniani ulitaka wanafunzi wapewe maagizo mengi zaidi na washiriki wa wafanya kazi wa makao makuu ya Mashahidi wa Yehova, yaliyoko Brooklyn. Kwa hiyo kwa miaka kadhaa, mkazo ulitiwa juu ya kuzoeza wafanya kazi wa matawi. Baada ya hapo, lengo likawa tena juu ya kazi ya misionari.

Kwa miaka 27 iliyofuata, toka 1961 mpaka 1988, wanafunzi wa Shule ya Gileadi walifurahia pendeleo la kuishi na kujifunza mle mle miongoni mwa wafanya kazi wa makao makuu katika Brooklyn. Humo wanafunzi walinufaika na ushirika wa karibu wa washiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova na wahudumu wengine wenye ujuzi. Kungekuwa na njia gani bora zaidi ya kujifunza jinsi tawi la Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi linavyoendeshwa? Wanafunzi walinufaika si na mazoezi darasani tu bali pia kwa kutazama wafanya kazi wa makao makuu wakifanya kazi kila siku.

Shule ya Gileadi imekuwa na matokeo gani juu ya kazi ya kimataifa ya kuhubiri? Waratibu 74 kati ya 93 wa halmashauri za tawi wanaotumika kuendeleza kazi ikiwa imepangwa kitengenezo ulimwenguni pote, ni wahitimu wa Shule ya Gileadi. Jambo hilo linatoa sifa kwa yale mazoezi bora waliyopokea wanaume hawa kwa ajili ya kushughulikia daraka zito la kuchunga watu wa Mungu leo. Pia waangalizi wanaosafiri wasiohesabika wanaotumikia sasa mahitaji ya tengenezo ni wahitimu wa Shule ya Gileadi. Ndiyo, programu ya mazoezi kwenye Shule ya Gileadi imeenda sambamba na mahitaji ya tengenezo.

Gileadi Yahama Brooklyn

Hata hivyo, kwa mara nyingine tena, uamuzi ulifanywa kuhamisha Shule ya Gileadi. Hivyo katika vuli ya 1988, malori manne yenye kujaa fanicha na vifaa vya ofisi yaliwasili kwenye makao ya tatu ya Gileadi​—Mashamba ya Mnara wa Mlinzi, yaliyoko Wallkill, New York. Katika muda wa miezi miwili tu, watengenezaji vifaa kwenye Mashamba ya Mnara wa Mlinzi walitayarisha madarasa mazuri, maktaba moja, na ofisi za shule hiyo. Baadhi yao walifanya kazi mchana na usiku ili kutayarisha vifaa vya shule bila kuchelewa ili darasa lililokuwa likifuata lianze mazoezi yalo.

Katika Oktoba 17, 1988, darasa la 86 la Gileadi likaanza. Bila kukosa jambo lolote, shule hiyo iliendelea na kusudi layo la ‘kuzoeza wanaume na wanawake wawe wahudumu wenye uwezo zaidi.’ Katika mazingira yayo yenye kupendeza kwenye Mashamba ya Mnara wa Mlinzi, baadhi ya mambo yenye kuvutia ya shule ya kwanza kabisa katika jimbo la Finger Lakes yalirudishwa.

Darasa la 86 Lahitimu

Katika Machi 5, 1989, wafanya kazi wote wa makao makuu ya Mnara wa Mlinzi katika Brooklyn na Mashamba ya Mnara wa Mlinzi walikusanyika pamoja kwenye Jumba la Kusanyiko la Jiji la Jersey kushiriki programu ya kuhitimu kwa darasa la 86. Daniel Sydlik, mshiriki wa Baraza Linaloongoza, alifungua programu kwa sala. Karl Klein wa Baraza Linaloongoza alitumika akiwa mwenyekiti. Katika utangulizi wake, alionyesha tofauti iliyoko kati ya wamisionari wa nchi za kigeni wa Jumuiya ya Wakristo na wale wa Mashahidi wa Yehova. Lo, wamisionari waliozoezwa Gileadi wamefanikiwa kama nini katika kufundisha ukweli wa Neno la Mungu katika nchi kama Japani, ambako sasa kuna Mashahidi zaidi ya 131,000 wanaoshiriki utumishi wa shambani wakiwa watendaji!

Donald Krebs akitumia kichwa “Acheni Kazi Nzuri Ziwe Kitambulisho Chenu,” alieleza lile daraka lenye kuleta badiliko ambalo wamisionari wa Gileadi wamekuwa nalo katika ongezeko la ulimwenguni pote la tengenezo la Yehova. “Kazi zenu nzuri katika shamba la umisionari mkiwa walimu wa Neno la Mungu zitakuwa . . . sifa yenu ya kuwapambanua. Twawatia moyo mfanye kazi kwa bidii. Yehova atabariki sana jitihada zenu.”

George Gangas, mshiriki wa Baraza Linaloongoza, alitoa hotuba motomoto juu ya kichwa “Biblia Ndicho Kitabu Bora Zaidi Chini ya Jua.” Aliwashauri wahitimu hivi: “Msisahau kujifunza Biblia. Biblia imejaa vito vya kiroho . . . ambavyo hung’aa na kumetameta. Mtu anayevithamini hutaka kuvitazama tena na tena na kufurahia sifa zavyo zenye kumetameta.”

Kichwa cha Richard Eldred kilikuwa “Nyinyi Mnaweza Kufanyiza Tofauti.” Wamisionari wapya wanapogusa maisha za watu wengine, wanaweza kufanyiza tofauti nzuri. Wanaume na wanawake wa nyakati za kale kama vile Daudi, Nehemia, Debora, na Abigaili walikuwa na uvutano mzuri juu ya wengine kwa kuwajali sana, wakidumisha imani yenye ujasiri, na kuonyesha mwelekeo wa upole na wa kiroho.

“Hesabuni Baraka Zenu” ndiyo maneno Lyman Swingle, mshiriki wa Baraza Linaloongoza, aliyosema kwa darasa hilo lenye kuhitimu. Baada ya kusimulia baraka chache ambazo darasa hilo limekuwa nazo, kama vile kuweza kutumia miezi mitano wakikaza fikira kwenye funzo la Biblia, aliwatia moyo hivi: “Mwisho ukaribiapo, huenda mkaona mwendo ukiwa wa haraka zaidi, huenda njia ikawa ngumu zaidi, kijia kikainuka zaidi. Lakini hakikisheni kwamba hamchoki kamwe, kwamba hamwachi kamwe, kwamba hamshindwi kamwe.”

Mmoja wa wakufunzi, Jack Redford, alisitawisha kichwa “Msiache Nguvu Yenu Iwe Udhaifu.” Kikitegemea shauri la Sulemani, “Usiwe na haki [uadilifu, NW ] kupita kiasi,” yeye alitoa onyo juu ya kutegemea sana majaliwa ya kibinafsi badala ya kumwegemea Yehova. (Mhubiri 7:16, 17) “Sifa nzuri zikitumiwa kupita kiasi zaweza kuwa mtego.” Kielezi, mtu ambaye nguvu yake ni sheria na utengamano huenda akatumia sifa hiyo kwa njia ya kupita kiasi kwa kuwa mkali mno. Hivyo, alitolea darasa shauri hili: “Yatupasa sisi sote kujua udhaifu wetu, lakini yatupasa pia kujua nguvu zetu. Muwe waadilifu lakini si wenye kujihesabu wenyewe kuwa waadilifu. Mwegemeeni Yehova. Mfanyeni Yehova kuwa nguvu yenu.”

Ulysses Glass, aliye mkufunzi na mwandikishi wa shule, alifafanua maneno ya Yesu, “Jitieni nira yangu.” (Mathayo 11:29, 30) Hapa Yesu alikuwa akiwaalika wanafunzi wake ‘wajitie chini ya nira yake’ pamoja naye. Yeye hakutaka kuwawekelea mzigo wenye kulemea. Alikuwa sana-sana akifikiria mahitaji ya wengine. Alionyesha unyenyekevu. Hakupiga wanafunzi wake kwa maneno makali. Yesu alisema, “Mjifunze kwangu.” Lazima misionari awe na nia ya Kristo. Msemaji huyu alisifu darasa kwa sababu ya roho yao ya kutoa na akawatia moyo waendelee kuonyesha roho iyo hiyo katika migawo yao ya nchi za kigeni.

Kipindi cha asubuhi kilipokuwa kikikaribia kufungwa, mshiriki wa Baraza Linaloongoza Carey Barber alitoa hotuba motomoto juu ya kichwa “Mavuno Ni Umalizio wa Mfumo wa Mambo.” Alivuta uangalifu kwenye utimizo wa ki-siku-hizi wa kielezi cha Yesu cha ngano na magugu. (Mathayo, sura 13, NW) Kwanza, wapakwa-mafuta wa Kristo wanakusanywa. Kisha, hasa tangu mwaka 1935, kondoo wengine wamejiunga wakiwa ‘wamevunwa.’ Shule ya Gileadi imetimiza kazi nzuri ajabu katika kusaidia kuvuna wanafunzi wa Kristo.

Baada ya wahitimu kupewa diploma zao, mmoja wao alisoma barua yenye uchangamfu iliyoeleza hisia zao juu ya mazoezi na uangalifu waliopokea kutoka kwa wakufunzi na jamaa ya Betheli. Kwa sehemu, barua hiyo ilisema hivi: “Sisi tumevutiwa na jinsi nyinyi mmependezwa nasi tukiwa mmoja mmoja, licha ya kupendezwa nasi tukiwa darasa la Gileadi, na huo ni mwendo unaostahiki kuigwa. Tunaachana tukiwa na hisia zenye kuchanganyika​—tukiwa na huzuni kuondoka kwa sababu hamtakuwapo pamoja nasi lakini tukiwa na furaha na kusisimukia mgawo wetu mpya.”

Kwa ajili ya programu ya alasiri, wahitimu walishiriki Funzo la Mnara wa Mlinzi lililoongozwa na Ralph Walls. Kisha darasa likaigiza baadhi ya mambo makuu ya maono waliyopata katika huduma ya shambani wakati wa kukaa kwao katika Mashamba ya Mnara wa Mlinzi. Halmashauri ya Ufundishaji ya Baraza Linaloongoza ilitoa programu ya viigizo vya kuchekesha yenye kichwa: “Ustahifu kwa Mamlaka Huendeleza Umoja” pamoja na wonyesho wa slaidi ukionyesha shangwe ambazo wamisionari wameshiriki katika mabara mengi kwa muda wa miaka mingi iliyopita. Programu ilifikia ukomo kwa sala yenye kujaa hisiamoyo iliyotolewa na Frederick Franz, msimamizi wa Shule ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi mwenye umri wa miaka 95.

Kwa itikio lao lenye idili kwa programu hiyo, wahudhuriaji walionyesha kwamba wanawaunga mkono hao waliotazamiwa kuwa wamisionari na wakaithamini kwa programu. Hakuna shaka kwamba wale wahitimu 24 wa darasa la 86 la Gileadi wameazimia kumfanya Yehova kuwa nguvu yao waendapo kwenye migawo yao yenye pendeleo katika shamba la umisionari.

[Sanduku katika ukurasa wa 21]

MUHTASARI KUHUSU WANAFUNZI

Hesabu ya wenzi wa ndoa: 12

Hesabu ya wanafunzi: 24

Hesabu ya nchi watokako wanafunzi: 6

Hesabu ya nchi walikogawiwa: 12

Wastani wa umri: 32.3

Wastani wa miaka katika ukweli: 14.1

Wastani wa miaka katika huduma ya wakati wote: 9.1

[Picha katika ukurasa wa 23]

Kuhitimu kwa darasa la 86 la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi

Katika orodha iliyopo chini, mistari imepewa namba kuanzia mbele mpaka nyuma, na majina yameorodheshwa kuanzia kushoto mpaka kulia katika kila mstari.

(1) Parrott, R.; Imig, E.; Benig, G.; Bengtsson, E.; Baart, W.; Ihander, K. (2) Lewis, J.; Hilario, L.; Lindmark, A.; Antoncich, G.; Agurs, C. (3) Bengtsson, R.; Parrott, J.; Benig, J.; Imig, J.; Baart, A.; Rissell, S. (4) Rissell, M.; Lewis, L.; Antoncich, M.; Hilario, R.; Agurs, H.; Lindmark, L.; Ihander, J.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki