Utafutaji wa Ukweli Wathawabishwa
KWA SABABU ya kutotoshelezwa sana akiwa mhubiri wa kawaida katika kanisa la Kipresbiteri, muungwana mmoja wa kiume alianza kutafuta-tafuta kanisa la kweli la Mungu. Aliandika matakwa kumi ambayo alihisi kanisa la kweli limepaswa kuwa nayo. Tayari alikuwa anaelewa kwa usahihi jinsi fundisho la moto wa mateso, kutokufa kwa nafsi, na kadhalika halipatani na maandiko. Kwa muda wa miaka 30 aliongoza utafutaji huu. Alipofikiwa na mmoja wa Mashahidi wa Yehova, alianza kumtupia makombora ya maswali, kama vile: “Kundi dogo ni nani? Ni nani walio wale 144,000 na kondoo wengine?” Alipopata majibu yenye kutosheleza, alikubali kuwa funzo la Biblia. Baada ya miezi mitatu alisema hivi kwa yule Shahidi: “Basi, Ndugu, lililo kanisa la kweli la Mungu ni Mashahidi wa Yehova.” Sasa yeye ni mwenye umri wa miaka 71 na ana furaha kwa kuwa amelipata kanisa la kweli baada ya utafutaji wa miaka 30!