Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 11/15 kur. 4-6
  • Ule Ulimwengu Mpya—Paradiso Iliyopatikana Tena!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ule Ulimwengu Mpya—Paradiso Iliyopatikana Tena!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Paradiso Yapotezwa
  • Paradiso Yarudishwa
  • Ule Ulimwengu Mpya—Tofauti Kweli Kweli!
  • Je! Wewe Utakuwa Kwenye Mambo Hayo?
  • “Tutaonana Paradiso!”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Unaweza Kuwa na Wakati Ujao Wenye Furaha!
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Baada ya Har-Magedoni, Dunia-Paradiso
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • “Utakuwa Pamoja na Mimi katika Paradiso”
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 11/15 kur. 4-6

Ule Ulimwengu Mpya​—Paradiso Iliyopatikana Tena!

MUME na mke waliokuwa wamefunga ndoa karibuni walikuwa na maskani ya kupendeza sana​—bustani kubwa iliyojaa maua, miti, ndege, na wanyama. Ilikuwa Paradiso, zawadi ya ukarimu kutoka kwa Baba yao mwenye upendo! Je! wao “waliishi mustarehe muda wote uliofuata”? Sivyo. Muda si muda, wao walipoteza maskani yao. Lakini kwa nini?

Maskani hiyo ya Paradiso ilipotezwa kwa sababu mume na mke hao hawakuthamini yale ambayo Baba yao alikuwa amewafanyia. Kuongezea ubaya, wao wakawa wasiotii. Ili kujaribu ukamilifu wao, Baba yao alikuwa amewaambia kwamba wangeweza kula tunda la kila mti isipokuwa mmoja, lakini kwa uasi wao wakakosa utii na kuchukua sehemu ya mti huo.​—Mwanzo 2:15-17; 3:6, 7.

Kwa nini kuwe na adhabu kama hiyo kwa jambo ambalo huenda likaonekana kama kwamba lilikuwa uhalifu mdogo? Labda kielezi kimoja kitasaidia kujibu swali hilo. Mwenye duka anaajiri msimamia-kazi aliye na sifa zinazohitajiwa kabisa. Ili kuhakikisha kwamba mwajiriwa huyu mpya anaweza kuitibariwa, mwenyeji huyo anampa funguo lakini anasema kwamba hapaswi kufungua kitoto-meza fulani hata iweje. Mwajiriwa huyo akifanya hivyo, ataondolewa kazini. Anapoachwa peke yake, udadisi unamlemea msimamia-kazi naye anafungua kile kitoto-meza. Mwenyeji anamshika akiwa katika kitendo hicho na kumwondoa kazini.

Paradiso Yapotezwa

Jambo hilo linahusiana jinsi gani na mume na mke wale wachanga? Kwa sababu wao walikula tunda lililokatazwa, Baba yao aliwaondoa katika maskani yao yenye uzuri. Wakiwa nje ya Paradiso ya Edeni, miiba na michongoma ilikabili mume na mke hao waliofunga ndoa, Adamu na Hawa. Badala ya kuwa wakamilifu, sasa walikuwa wasiokamilika. Na badala ya kuishi milele, walianza kufa. Watoto wao walirithi kutokamilika, udhambi, na kifo chao.​—Warumi 5:12.

Mwishowe, “BWANA [Yehova, NW] akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani.” Kwa hiyo, katika siku za Noa, Mungu alitumia Gharika kusafilisha dunia. Je! kulikuwa na waokokaji wowote wa kibinadamu? Wanane tu​—Noa na wanaye watatu pamoja na wake zao wanne. Kwa kujitayarishia ile inayoweza kuitwa safari yao ya kubaharia wakaingie katika ulimwengu tofauti, wao walijipatanisha na maagizo ya Mungu na walikuwa wamejenga safina kubwa sana iliyoweza kuwachukua wao, aina nyingi za wanyama, na vyakula vya kutosha. (Mwanzo 6:5-7, 13-22) Bustani ambayo hapo kwanza ilifurahiwa na Adamu na Hawa ilifutiliwa mbali na Gharika. Hivyo, Paradiso ilipotezwa​—lakini si milele!

Paradiso Yarudishwa

Karne kadhaa baadaye, Mungu alituma duniani Mwana wake mzaliwa wa pekee akomboe aina ya binadamu kutoka kwenye dhambi na kifo. Hiyo ilifanya iwezekane wale wenye kujizoeza imani katika Yesu Kristo wapate uhai wa milele. (Yohana 3:16) Pia Yesu alitabiri kwamba Paradiso ingepatikana tena. Kweli kweli, Yesu alipokuwa akifa juu ya mti wa mateso, yeye alimwambia hivi mhalifu mmoja aliyetundikwa mtini kando yake: “Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.”​—Luka 23:43, ZSB.

Kupatikana tena kwa Paradiso kutafuata ule ambao mara nyingi huitwa mwisho wa ulimwengu, ambao ulitabiriwa na Yesu wakati wanafunzi wake walipouliza: “Ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” Katika kujibu, Yesu alielekeza kwenye vita, upungufu wa vyakula, matetemeko ya dunia, magonjwa ya kipuku, ukosefu wenye kuongezeka wa kutii sheria, na kampeni ya ulimwenguni pote ya kuhubiri Ufalme. Mambo hayo na mengineyo yaliyo sehemu ya ishara yamekuwa ithibati yenye kuonekana tangu 1914. (Mathayo 24:3-14, NW) Hizo ni dalili za kuashiria mwisho wa mfumo huu na kurudishwa kwa Paradiso juu ya dunia hii.

Katika unabii ule ule, Yesu alisema hivi pia: “Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu; nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni. Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia.” (Mathayo 24:32-35) Manabii mengine ya Biblia yanaonyesha pia kwamba kupatikana tena au kurudishwa kwa Paradiso ku karibu sana, kwamba ulimwengu mpya uko kwenye upeo wa macho. Lakini huo utakuwaje?

Ule Ulimwengu Mpya—Tofauti Kweli Kweli!

Nafasi ya serikali za siku iliyopo itachukuliwa na Ufalme wa Mungu. (Danieli 2:44) Kutakuwako haki na amani ya kudumu kwa ajili ya wote katika ule ulimwengu mpya chini ya utawala wa Ufalme mikononi mwa Yesu Kristo, “Mwana-Mfalme wa Amani.” (Isaya 9:6, 7, NW) Kwa kuwa yeye ataharibu waovu na elementi zisizotii sheria ambazo zinalemea aina ya binadamu sasa, wale “wasio na lawama” ambao ni wapenda-amani ndio peke yao watabaki. (Mithali 2:21, 22; Ufunuo 19:11-21; 16:14-16) Ndiyo, waokokaji watakuwa watu wasikivu, wapenda-amani. Hicho kitakuwa kitulizo kama nini!

Ubaguzi wa rangi ya ngozi na wa namna nyinginezo utatoweka katika ule ulimwengu mpya. Kwa uhakika, umati mkubwa sana wa watu umekwisha tayari kutoka mbali katika kushinda mambo hayo. Wao ni akina nani? Mashahidi wa Yehova. Na kwa nini wao ni tofauti sana? Kwa sababu wanajifunza Biblia kwa bidii-endelevu, wanaitumia katika maisha, na wana upendo miongoni mwao wenyewe. (Yohana 13:34, 35; Matendo 10:34, 35) Sasa hesabu ya Mashahidi ni mamilioni ulimwenguni pote, lakini Biblia inatabiri kwamba mwishowe waabudu wa kidunia wa Yehova watakuwa “hesabu kubwa sana, isiyowezekana kuhesabu, ya watu kutoka kila taifa, rangi ya ngozi, kabila na lugha.”​—Ufunuo 7:9, The Jerusalem Bible.

Vita haitachukua tena uhai wa wanadamu. Mabilioni ya pesa hayatatumiwa tena kuhusiana na silaha za nyukilia, silaha nyinginezo, na kani za kijeshi. Mapinduzi makubwa, mapambano kati ya watu wa rangi mbalimbali, na aina nyinginezo zote za jeuri hazitakuwako. (Isaya 2:4) Mazoezi ya kijeshi na kuandikisha wanajeshi wapya yatakoma, kwa maana hayatahitajiwa kabisa. Itakuwa siku yenye furaha wee wakati Mungu avikomeshapo vita!​—Zaburi 46:8, 9.

Amani ya kweli itakuwako kwa wingi. “Bado kitambo kidogo,” akasema mtunga zaburi, “asiye haki [aliye mwovu, NW] hatakuwapo . . . Bali wenye upole watairithi nchi, watajifurahisha kwa wingi wa amani.”​—Zaburi 37:10, 11.

Upungufu wa vyakula utaondoka kuwe na utele. Katika mahali pengi, sasa wakulima wadogo walio maskini wanang’ang’ana na miiba na michongoma, udongo usio na rutuba, majangwa yenye kuwajongelea, ukavu, na mavamio ya nzige wateketezaji. Yote hayo yatapindushwa. (Isaya 35:1, 6, 7) Tokeo liwe nini? Ongezeko kubwa sana katika uzaaji! (Zaburi 72:16) Akikomesha upungufu wa vyakula na vinywaji, Yehova ataandaa “karamu ya vinono”!—Isaya 25:6.

Kazi ya kuthawabisha itafurahiwa na wote. Itaridhisha kama nini kujenga maskani, kupanda mitunda, na kutunza bustani! Na lo, ni furaha gani kuketi katika uvuli wa mtini wako mwenyewe na kula matunda yao matamu!​—Mika 4:4.

Makao ya nyumba za hali bora kabisa yataandaliwa kwa kila mmoja. Leo, mamilioni wanaishi katika mitaa ya kimaskini sana au katika miji ya vibanda vichafu-vichafu. Ni maisha ya kukosa furaha kama nini! Mathalani, katika Afrika mamilioni ya wakaaji wanaacha sehemu za mashambani, lakini mara nyingi wanalazimika kuishi katika maskani za matope au udongo ulioezekwa mabati, hali mbaya za kiafya, na ufaragha kidogo. Hata hivyo, katika ule ulimwengu mpya watu watajenga nyumba nzuri sana na kuzikaa.​—Isaya 65:21, 22.

Afya kamilifu itasitawi sana badala ya ugonjwa na maradhi kama UKIMWI wenye kufisha. Mnabii aliyevuviwa alitabiri kwamba hakuna mmoja atasema: “Mimi mgonjwa.” Waaidha, katika ule ulimwengu mpya ulio karibu, “macho ya vipofu yatafumbuliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa. Ndipo mtu aliye kilema ataruka-ruka kama kulungu, na ulimi wake aliye bubu utaimba.”​—Isaya 33:24; 35:5, 6.

Kifo, machozi, na sebule za kutayarishia maziko zitatoweka. (Ufunuo 21:4) Lakini namna gani juu ya mabilioni ambao tayari ni wafu? Alipokuwa mwanadamu duniani, Yesu alifufua watu kadhaa. Mathalani, wakati mmoja alikutana na msafara wa maziko ukiandama jeneza la kijana mwanamume aliyekuwa amekufa kitambo kidogo katika jiji la Naini. Baada ya neno la kufariji mama yule mfiwa, aliye mjane, Yesu alisema: “Kijana, nakuambia, Inuka”! Naye akainuka! (Luka 7:11-17) Katika pindi nyingine, Yesu alitoa uhakikishio huu: “Saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini [makaburi ya ukumbusho, NW] . . . watatoka.” (Yohana 5:28, 29) Kwa kuwa Mungu aliumba kwintilioni za nyota na madude mengine ya kimbingu na huyaita “kwa majina,” kwa uhakika ufufuo wa mabilioni ya wafu wa kibinadamu hautakuwa tatizo lolote.​—Isaya 40:26.

Je! Wewe Utakuwa Kwenye Mambo Hayo?

Hapo awali Yehova Mungu alikusudia aina ya binadamu isife kamwe bali ifurahie milele vitu vyema alivyoandaa kwa upendo. Kwa hiyo ebu wazia baraka za uhai katika ulimwengu mpya wenye jamaa zilizo na furaha! Fikiria watoto wakiweza kucheza kwa usalama pamoja na wanyama ambao sasa ni hatari sana. (Isaya 11:6-9) Fikiria baraka za amani, makao ya nyumba njema, kazi ya kuthawabisha, chakula tele. Ndiyo, na ufikirie kuishi milele katika paradiso ya kidunia.

Je! wewe unaweza kuwako? Ndiyo, ukitwaa maarifa sahihi juu ya Neno la Mungu na kutenda kulingana nayo. Mashahidi wa Yehova wako tayari kukusaidia wewe ujenge imani katika makusudi ya Mungu yasiyoshindwa. Wewe unaweza kuwa na uhakika kwamba karibuni Paradiso itapatikana tena, kwa maana ulimwengu mpya u karibu sana!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki