Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 2/1 uku. 24
  • ‘Kuvuna’ Katika Venezuela

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kuvuna’ Katika Venezuela
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Habari Zinazolingana
  • “Tumehubiri Eneo Letu Mara Nyingi Sana!”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Wanahitajiwa kwa Haraka—Wafanya Kazi Zaidi wa Mavuno!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Mashamba Ni Meupe kwa Ajili ya Kuvunwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Iweni Wavunaji Wenye Furaha!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 2/1 uku. 24

Wapiga Mbiu ya Ufalme Waripoti

‘Kuvuna’ Katika Venezuela

Katika pindi moja Yesu aliilinganisha kazi ya kuhubiri na mavuno ya kila mwaka. (Mathayo 9:36-38) Bwana wa mavuno ni Yehova Mungu, na mavuno kwa kweli ni mengi tufeni pote. Hii inatia ndani eneo lisilofanyiwa kazi kwa ukawaida katika Venezuela.

Ofisi ya tawi ya Watch Tower Society ya Venezuela yaripoti lililotokea wakati kikundi cha Mashahidi walipolifanyia kazi eneo la Sabana Grande, Jimbo la Guárico. Mashahidi hao waeleza hivi: “Nyumba ambayo tungeishi ilikuwa mahali pazuri pa kufanyia mikutano, kwa hiyo mara moja tulianza kualika watu kwenye mikutano huko. Watu hawakuwa wamejua juu ya Mashahidi wa Yehova. Ingawa kulikuwako na vikundi vinne vya kievanjeli mjini, watu walikuwa na tamaa ya kujifunza kutokana na Biblia.

“Tulifanya kazi kwa muda wa saa tatu kipindi cha asubuhi na saa tatu kipindi cha alasiri, tukienda nyumba kwa nyumba na kualika watu kwenye mkutano usiku ufuatao. Hatukuwa na viti, kwa hiyo tuliwaalika waje na viti vyao. Wakati ulipofika wa mkutano kuanza, watu walianza kuja, kila mmoja akibeba kiti. Mkutano ulipokwisha, tuliwaambia tungependa kuandika majina ya wale waliotamani kuwa na funzo la Biblia la nyumbani bila malipo. Wahudhuriaji wote 29 walitaka majina yao yawe katika orodha.

“Tulipokuwa tukifunga mlango baada ya mgeni wa mwisho kuondoka, tuligundua watu watatu waliokuwa wamesimama kwenye kona ya nyumba. Karibu saa tatu hivi, tulikuwa tayari kula walipobisha mlangoni. Waliuliza maswali kama vile: ‘Ni kuhubiri gani huku mnakofanya katika mji huu? Ni kwa sababu gani mlikuwa na mkutano usiku huu?’

“Tuliuliza ikiwa tulikuwa tumevunja sheria yoyote. Walijibu la na wakasema walikuwa mapasta wa makanisa matatu ya kievanjeli ya mji huo. Walikuwa wameudhika kwa sababu makanisa yao yalikuwa matupu jioni hiyo. Tuliwakaribisha ndani na kuwaeleza juu ya kazi yetu. Tuliwaangushia pia vichapo kadhaa na tukawaomba warudi Alhamisi ifuatayo.

“Alhamisi iliyofuata mapasta walirudi tena na watu 22 wengine waliotaka kusikia tuliyokuwa tunasema. Mapasta walifikiria kwamba, tukiwa wanawake, hatungeweza kuwafikia katika mazungumzo. Ingawa hivyo, kulingana na maoni yetu mkutano huo ulifanikiwa. Mwishoni tulieleza kwamba tulikuwa tunafanya orodha ya wale waliotaka kujifunza mengi kutokana na Biblia. Waandamani kadha wa mapasta walitaka majina yao yatiwe katika orodha hiyo, na wengine hata walisema walitaka kwenda nasi katika kazi ya kuhubiri!

“Tulieleza kwamba wangehitaji maarifa zaidi ya Biblia na mazoezi zaidi kabla ya kujiunga nasi katika kazi ya kuhubiri. Kila siku watu walikuwa wakija kwenye nyumba, wakituomba tuwaeleze juu ya Biblia. Wakati mwingine, tulipokuwa tukiongea mpaka usiku sana, ilitulazimu tuwaombe waende nyumbani. Hatimaye tulipokuwa tuondoke kwenye eneo hilo, walihuzunika sana na wakatuambia kwamba tukirudi wataenda nasi katika kazi ya kuhubiri. Waliahidi kwamba kufikia wakati huo watakuwa wamefanya maendeleo yanayohitajiwa.”

Mashahidi walipoliacha eneo hilo, kulikuwa watu 40 waliotaka kujifunza Biblia. Majina ya watu hao wenye kupendezwa yalipelekwa kwa kundi lililokuwa karibu zaidi, ambalo ni kilometa 50 hivi. Hatimaye, Mashahidi kadha kutoka mji mwingine walihamia katika mji huo, na kikundi chenye bidii cha wahubiri wa habari njema kimeanzishwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki