Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 2/1 uku. 30
  • Tumbaku na Makasisi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumbaku na Makasisi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Kuongozwa na Dhamiri Katika Kufanya Mema kwa Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Mungu atahisije nikitumia tumbaku?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Tumbako na Uchunguzi wa Kama Yafaa Kutumiwa
    Amkeni!—1990
  • Maadili ya Tumbaku?
    Amkeni!—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 2/1 uku. 30

Tumbaku na Makasisi

MIAKA 115 iliyopita, daktari mmoja wa tiba John Cowan aliandika kitabu chenye kichwa The Use of Tobacco vs. Purity, Chastity and Sound Health. Kwa sababu ya yale ambayo yamepata kujulikana katika miaka ya hivi karibuni kuhusu matokeo yenye kudhuru ya kutumia tumbaku, maoni yake juu ya kutumiwa kwayo na makasisi yalikuwa yenye kutazama mbele na ni yenye maana kwa kila mtu anayetaka kumtumikia Mungu leo. Katika sura ya 4, inayoshughulikia matokeo ya kiadili ya matumizi ya tumbaku, Dakt. Cowan alisema hivi:

“Ikiwa kutumia tumbaku ni jambo lisilo sawa kimwili—kama ambavyo imeonyeshwa kwa wazi—ni lazima bila shaka kusiwe sawa kiadili; kwani ni sheria ya kisaikolojia kwamba ‘chochote kinachoharibu au kuudhi mwili, hivyo huharibu mfumo wa neva, na kupitia njia hiyo huharibu ubongo, na hivyo akili.’ Akili ya mtu—mawazo yake, usemi wake, matendo yake, huathiriwa na njia anayotumia au kutumia vibaya asili yake ya kimwili. Jina layo lenyewe na mambo yanayoshirikishwa nayo, huonyesha tumbaku ni chafu, na—bila hata kufikiria madhara inayofanya—hisia na matendo safi, yenye utakato, yenye haki, ya kiadili yanaweza kuanzaje au kusitawije katika akili. Pia dhania—ikiwa jambo hilo laweza kudhaniwa—kwamba Kristo, alipokuwa akiishi maisha yake ya kielelezo kizuri duniani—akifundisha na kuhubiri utakato, usafi wa kiadili, upendo na ufadhili—alikuwa akivuta sigareti, kunusa na kutafuna tumbaku. Je! wazo lenyewe halisikiki kuwa kinyume cha dini? Hata hivyo wahudumu—wafuasi, wahubiri, na wafafanuaji wa sheria na mafundisho Yake—huichafua miili yao na kuzitia mawaa nafsi zao kwa magugu hayo machafu yenye sumu. Je! watu hao, au wafuasi wao, waweza kuishi maisha yaliyo kama ya Kristo—maisha yenye kiwango cha juu, ya kiadili? Sidhani hivyo.

“Kwa habari ya utakatifu wa moyo, jaribu, ikiwa waweza, kufikiria mlafi mwenye pupa, mzoevu wa divai, au mwenye kutumia tumbaku? Kuna jambo fulani lisilo la kiasili, lenye kuchukiza sana, lenye kukirihi, katika ushirika wa mawazo hayo. Kama vile hamu za kimwili na fahamu za nje zinavyoharibiwa, ndivyo mtu wa kindani, asili ya kiadili, anavyokuwa mbaya sana. Roho safi haitakaa, haiwezi kukaa, katika nyumba chafu. Kuna ulinganifu wa kiasili kati ya mambo halisi na mambo ya kiroho, hivi kwamba sifa za moja huonyesha sifa za lile jingine. Profesa wa dini na mtumwa wa tumbaku . . . Huenda akakubali, katika unyoofu na moyo mweupe wote, kwamba kutumia tumbaku ni desturi yenye kudhuru, isiyo sawa kiadili; hata hivyo huenda akapata msukumo kutoka ndani, sheria ya viungo vyake, uliotokezwa kwa njia isiyo ya kiasili, ukimchochea kwa tamaa za kilafi aendeleze zoea hilo, na sheria hiyo isiyo ya kiasili huenda ikawa yenye nguvu zaidi ya kusababu kwake kwa asili na ufahamu wake zikiwa pamoja. Je! kutumia tumbaku si kuhalifu kidhahiri mojayapo sheria za Mungu zilizomo mwilini mwetu? Je! kuhalifu yoyote kati ya sheria za Mungu si kosa na dhambi? Na mtu akiishi kidesturi kwa kuhalifu mojayapo sheria za Mungu, je haitakuwa rahisi na jambo la kiasili kwake kuhalifu sheria nyinginezo? Na mwishowe, mtu yeyote aweza kuonwaje kuwa mfundishaji wa adili, ambaye, katika mwenendo wake mwenyewe, huwapendekezea viumbe wenzake maisha ya kuhalifu daima sheria za mwili wake?”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki