Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 8/15 kur. 377-380
  • Kuongozwa na Dhamiri Katika Kufanya Mema kwa Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuongozwa na Dhamiri Katika Kufanya Mema kwa Wote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUKUZA TUMBAKO
  • JARIBU LA IMANI
  • KUCHEZA KAMARI NA DHAMIRI
  • KUHESHIMU UHAI
  • Tumbako na Uchunguzi wa Kama Yafaa Kutumiwa
    Amkeni!—1990
  • Maadili ya Tumbaku?
    Amkeni!—1992
  • Mungu atahisije nikitumia tumbaku?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Watetea Tumbaku Waanzisha Puto la Hewa-Joto
    Amkeni!—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 8/15 kur. 377-380

Kuongozwa na Dhamiri Katika Kufanya Mema kwa Wote

KAMA wewe ungefanya kazi katika soko la nyama, je! ungeuza kipande cha nyama kilichooza? Au ungemwelekeza msafiri wa kwenda mguu usiku kwenye barabara unayojua inapita katika eneo la hatari sana, lenye uhalifu mwingi?

Haielekei sana kuwa ungeweza kufanya haya. Kwa nini? Kwanza, kwa sababu dhamiri yako​—maono yako ya ndani ya yaliyo haki na makosa​—inakuambia kwamba matendo haya ni makosa.

Lakini, mtu, kwa sababu ya malezi yake na mazingira, huenda akafanya mambo yaliyo makosa kulingana na sheria ya Mungu bila ya dhamiri yake kusumbuliwa nayo. Lakini yampasa Mkristo kufanya marekebisho ifaavyo anapojifunza namna ambavyo Mungu anavyoyaona mambo. Maono yake ya ndani ya yaliyo haki na makosa yamepaswa yamsukume afanye yampendezayo Mungu. Je! dhamiri yako inafanya hivyo? Je! wewe unaongozwa na dhamiri katika kufanya mema kwa wote?​—Gal. 6:10.

KUKUZA TUMBAKO

Katika miaka ya majuzi mengi yamechapwa yakiitaja tumbako na kuonyesha ni yenye kudhuru afya. Kwa kweli, Royal College of Physicians in Great Britain (chuo kikuu cha madaktari) kilisema hivi juu ya jambo hili: “Uvutaji wa sigareti sasa ni sababu kubwa ya kifo sawa na yalivyokuwa magonjwa ya kipuku kama vile homa ya matumboni, kipindupindu, kifua kikuu yaliyovipata vizazi vilivyotangulia katika nchi hii.” Zaidi ya hayo, mtu aendeleaye kuvuta sigareti haishi kupatana na onyo la Maandiko la ‘kujitakasa nafsi yake na uchafu wote wa mwili na roho, huku akitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.’​—2 Kor. 7:1.

Kwa sababu hii, je! Mungu anapendezwa iwapo mtu anakuza tumbako inayotumiwa, na ambayo, kama matokeo, inatia sumu katika watu kidogo kidogo na kuharibu afya yao?

Wakristo wengi katika miezi na miaka ya majuzi wameazimia kwamba hawawezi wakakuza tumbako wakiongozwa na dhamiri. Anaandika hivi mtumishi wa huduma mmoja katika Harrodsburg, Kentucky, kundi la mashahidi wa Yehova:

“Kwa muda wa miaka 21 tumbako ndiyo iliyokuwa imekuwa chanzo chetu kikubwa cha mapato. Tulipojifunza kweli ya Biblia katika miaka ya majuzi, tuliona kwamba kukuza tumbako hakukufaa, kwa maana kuvuta sigara hakupatani na kanuni za Biblia. Lakini, haikuwa mpaka Aprili 1971 tulipokata maneno tusikuze tumbako tena. Mwaka uliofuata, wa 1972, tulikodisha shamba letu la tumbako, ambalo ni haki kutoka kwa serikali ya kukuza kadiri fulani ya tumbako.

“Lakini sasa dhamiri zetu hazitaturuhusu tufanye hivyo, kwa maana tungekuwa tungali twakusanya fedha kutokana na tumbako. Kwa hiyo tuliamua kuiacha kabisa haki yetu ya, shamba hili la tumbako.”

Ikiwa wewe ungekuwa mkuzi wa tumbako, je! ungefanya uamuzi kama huo? Mashahidi wa Yehova hawakujaribu kuweka kanuni na sheria juu ya mtu anavyoweza au asivyoweza kufanya katika mambo haya ya kazi. Lakini katika visa vingi dhamiri za watu mmoja mmoja zimewasukuma kupoteza mali ya kimwili kuliko kutiwa hatiani kwa njia yo yote ya kukuza tumbako. Mzee mmoja katika kundi la Stanford, Kentucky anaeleza alivyokuja kuona juu ya kushiriki ko kote katika ukuzi wa tumbako:

“Kwa muda wa miaka 13 iliyopita nimekodisha shamba langu la tumbako, nami nilipokea nusu moja ya mapato. Lakini, sioni tena inafaa kupokea mapato kutokana na zao lililohakikishwa kuwa lenye kuharibu afya. Mimi siwezi hata nikiongozwa na dhamiri kukodisha shamba langu la tumbako kwa mkulima mwingine hata kama ningekubali nisilipwe cho chote. Mimi sitashughulika na tumbako kwa vyo vyote.”

Vile vile, mmojawapo wa mashahidi wa Yehova katika Brooks, Kentucky, anaandika hivi: “Mara tu nilipoiona ile picha katika Mnara wa Mlinzi ya mwanamume na fungu la tumbako pamoja na lile ulizo, ‘Je! inapatana kuzungumza juu ya upendo wa jirani na wakati ule ule kutokeza tumbako ambayo huenda iharibu afya ya jirani yako?’ mambo yalikomea pale kwangu. Katika kipande cha nchi palipokuwa na tumbako nilipanda alfalfa, mmea wenye majani yafaayo sana kwa chakula cha ng’ombe. Tumbako si yangu tena hata iwe ya namna gani.”

JARIBU LA IMANI

Lakini, si vyepesi kwa watu wengine kufanya rekebisho hilo. Maisha yao yote yametegemea tumbako. Kwa hiyo ili waweze kushika dhamiri safi imehitaji imani kweli kweli. Hii yashuhudiwa na mfano wa mzee wa Kikristo katika Wilmore, Kentucky, anayeandika hivi:

“Mimi ninaondoka shambani ikiisha kupita miaka mingi. Tumekuwa tukifuga mifugo, kukuza nafaka na tumbako. Kwa maana tulikuwa tukifanya kazi kama wapangaji wa shamba, mwenye shamba alitaka bado tumbako ikuzwe. Nyuma ya kuuangalia Mnara wa Mlinzi kwa uangalifu juu ya dhamiri, hatuwezi tena kukuza tumbako kwa maana twaweza kuona kwamba hii isingekuwa ni kupatana na kuonyesha kwetu upendo kwa mwanadamu mwenzetu.

“Mimi sina uwezo wa kupata kazi ya kiserikali kwa sababu ya mwili wangu. Tunakusudia kuondoka shambani karibuni, tukijua kwamba kwa msaada wa Yehova mke wangu na mimi tutaweza kujiangalia wenyewe katika muda mfupi uliobakia kwa hii taratibu ya kale ya mambo.”

Kama dhamiri yako ingeitikia kwa njia hii katika hali kama hizi, je! wewe ungekuwa na imani ya kufanya rekebisho hilo katika kazi yako? Namna gani kama ungekuwa na jamaa kubwa ya kuruzuku? Mmoja wa mashahidi wa Yehova katika kundi la Williamstown, Kentucky, anaeleza kwa nini alifanya uamuzi huu wa kipekee:

“Mke wangu na mimi na watoto sita tuliishi miaka mingi katika shamba moja katika Owen County, Kentucky. Kazi yangu ilitia ndani upanzi na ukuzi wa ekari tatu za tumbako mbali na kufanya kazi katika shamba kama seremala, kazi iliyo nyingi ikiwa ni kutengeneza ghala za tumbako. Nilipewa nyumba tukae na mke wangu na watoto kama sehemu ya mshahara na tajiri wangu, nalo hili lilituwezesha kujisikia salama na wasiolemewa.

“Lakini, nilipoisoma makala katika Mnara wa Mlinzi wa Aprili 1, 1973 juu ya dhamiri nilijua kwamba nisingeweza kuendelea kukuza zao la tumbako au kufanya kazi katika ghala za tumbako na wakati ule ule nishike dhamiri njema mbele za Yehova. Kwa hiyo nilipopata nafasi ya kwanza nilimweleza msimamizi wa shamba kwamba nisingeweza kukuza zao jingine la tumbako au kufanya kazi katika ghala za tumbako kwa sababu ya dhamiri, naye akakubali.

“Najua kabisa hii yamaanisha kuondoka katika nyumba iliyomo shambani niliyopewa na tajiri wangu na kwamba itanipasa kutafuta kazi mpya ya kimwili ili niiruzuku jamaa yangu. Mimi sina mashaka yo yote au hofu juu ya kufanya rekebisho hili kwa maana najua kwamba Yehova anawaangalia kweli kweli wale walio na nia ya kumtii yeye.”

Nyakati nyingine, maono ya kipekee ya dhamiri yamesukuma wengi wa mashahidi wa Yehova kuacha kufanya kazi na kampani za sigareti na sigara. Mmoja wao (mwanamke), aliyekuwa ameajiriwa kwa muda wa miaka kumi na sita katika General Cigar Company katika Kingston, Pennsylvania, alieleza maono yake ya kipekee kwa njia hii: “Kutengeneza sigara hakukuwa kuishi kulingana na amri ya Yesu ‘kupenda jirani yako kama ujipendavyo nafsi yako.’”

KUCHEZA KAMARI NA DHAMIRI

Namna gani juu ya kucheza kamari? Je! kukuendeleza kweli kunaweza kulinganishwa na kumwelekeza mtu akaingie katika eneo ambamo maisha yake yangekuwa katika hatari kubwa?

Mfanya kazi wa mchezo wa kamari wa Las Vegas ambaye amekuwa hivyo kwa muda mrefu, aliyepanda ngazi na kusimamia wafanya kazi kadha, anasema: “Kucheza kamari kunachochea pupa. Mimi nilipata kutazama wafanya kazi wakiibiana na kuiibia kampani. Wanaume wanapoteza nyumba, jamaa, na kukosa kujiheshimu wenyewe, kwa sababu ya mchezo wa karata.”

Msimamizi huyu wa Las Vegas alikuwa akichuma shilingi 175,000 kwa mwaka. Lakini akaanza kujifunza Biblia na mashahidi wa Yehova naye akapata habari za maoni ya Mungu juu ya mambo. Alijua kwamba asingeweza kuwa mfuasi wa kweli wa Yesu Kristo akifanya kazi iliyokamatana moja kwa moja na kucheza kamari. Akijitahidi apate dhamiri safi alikiacha cheo chake na kutafuta kazi nyingine. Kuna mambo mengi yanayofanana na hili yaliyoonwa. Mkaaji wa Reno, Nevada, anaandika hivi:

“Mke wangu na mimi tulikuwa wafanya kazi wa kamari katika Harold’s Club, tukiwa imara sana katika njia za ulimwengu. Halikuwa jambo lisilo la kawaida kwa mfanya kazi mwenye urafiki kupeleka nyumbani mamia kadha ya shilingi baada ya zamu ya kufanya kazi. Makadirio yetu tusiyotaka yabadilike ya mapato yetu tukiwa pamoja yalikuwa shilingi 280,000 kwa mwaka.

“Kisha, mwaka wa 1968, tulipata pendeleo la kujifunza kweli za Neno la Mungu. Yalipokwisha mafunzo kadha ya Biblia tulifahamu ilitupasa kufanya mageuzi katika kazi yetu, Kwa kuwa mimi sikuwa nimepata mazoezi yo yote wala ufundi, kwanza niliona shida kupata kazi ya kuridhisha, lakini nilipokwisha kuvumilia katika jitihada zangu na katika sala kwa Yehova, nikawa dereva wa gari kubwa nami sasa naweza kuiruzuku jamaa yangu sawasawa.”

Je! wewe unaongozwa na dhamiri kwa kadiri gani juu ya kufanya mema kwa wote? Je! ungekuwa na nia ya kuacha cheo cha mshahara mnono ili uepuke kufanya kazi inayoshiriki moja kwa moja kutia moyo pupa na ufisadi?

KUHESHIMU UHAI

Je! kutengeneza silaha za kuharibu kunapatana na kutenda mema kwa wote? Je! dhamiri yako ingekuruhusu katika utengenezaji wa silaha?

Mwanamume mmoja aliyeajiriwa na kampani moja katika United States aliyejitoa atengeneze vifaa vya vita alisumbuliwa na ulizo hili alipoanza kujifunza Biblia. “Nilipoendelea kujifunza,” alieleza, “nilizidi kuwaza ikiwa mtu fulani angeniuliza ninapofanya kazi ni wapi, ningewezaje kumwambia nampenda jirani yangu na huku nashiriki kutengeneza vitu vya kuumiza wengine?” Kwa hiyo akaiacha kazi yake yenye mshahara mnono, na kutafuta kazi nyingine.

Wengine wengi wamefanya lile lile. Msimamizi wa kuhifadhi vifaa katika kiweko kimoja cha kijeshi katika Albany, Georgia, alitafuta kazi nyingine kwa maana alijua kwamba kama alitaka awe mfuasi wa Yesu Kristo, Mfalme wa Amani, asingeweza kushiriki tena na matayarisho ya vita. (Isa. 2:2-4; 9:6, 7) Naye mwanamume mmoja katika Robbins Air Force Base aliondoka vile vile kwa sababu kama hizo “Sasa nafanya kazi ya kuhifadhi vifaa mahali pengine nami napokea karibu nusu ya mshahara niliokuwa nikipokea,” anasema.

Mtu anakutana na maamuzi mengi yanayotia ndani mwenendo na uchaguzi wa kazi. Yako mambo yanayokatazwa waziwazi katika Biblia, kama vile kuiba na kusema uongo. (Efe. 4:28; Kol. 3:9) Na kunazo kanuni za Biblia zinazoonyesha kwamba haifai kuichafua miili yetu, zinazoonyesha waziwazi kwamba kuchafua miili yetu na mazao yenye kudhuru kama vile tumbako ni kosa.​—2 Kor. 7:1.

Lakini, katika sehemu nyingine, mambo hayako wazi sana na lazima sisi kama watu mmoja mmoja tuongozwe na dhamiri zetu juu ya tutakayoyafanya. Dhamiri yetu inaposumbuliwa na mambo tunayoyafanya, sisi tutaitikiaje? Ni kwa kadiri gani ambavyo upendo wetu utakavyoyapasa maamuzi tunayoyafanya? Je! tu wenye nia ya kujinyima ili tufanye yampendezayo Mungu na kushika dhamiri safi? Yehova Mungu atawabariki milele wale wanaotenda kwa njia ya kuwa na dhamiri safi mbele zake katika taratibu yake mpya ya haki.​—1 Yohana 2:17; 2 Pet. 3:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki