Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 10/1 kur. 3-4
  • Ufunguo wa maisha ya familia yenye mafanikio

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufunguo wa maisha ya familia yenye mafanikio
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Daraka Zito
  • Namna ya Kuwatunza
  • Kujenga Familia Yenye Nguvu Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Je! Wewe Unafundisha Watoto Wako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Watoto Wetu Ni Urithi Wenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Kutumia Neno la Mungu Katika Jamaa Zetu Wenyewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 10/1 kur. 3-4

Ufunguo wa maisha ya familia yenye mafanikio

“MUUNGANO wetu wa familia unazorota,” akasema mgombea-urais mmoja wa U.S. mwaka jana. Kwa kweli, kadiri ya kuzorota huko kwa familia yashtua sana. “[Ikiwa kungekuwa] mabadiliko ya ukubwa huo katika takwimu za kiuchumi au za kiwanda katika kipindi icho hicho,” likaripoti gazeti Fortune, “yangetuduwaza.”

Mara nyingi hata familia zinazojaribu kufuata kanuni za Biblia huathiriwa kwa njia yenye msiba. Miaka michache iliyopita, baba ya watoto sita katika miaka yao ya kabla ya utineja aliambiwa hivi na Mkristo mwenzake mwenye nia njema: “Waweza kutazamia kuwapoteza wanne wa watoto wako kwa ulimwengu.” Lakini, baba huyo hakuamini kwamba ni lazima ampoteze hata mmoja wa watoto wake. Alieleza ni kwa sababu gani.

“Watoto wetu kwa kweli si wetu,” akasema. “Yehova Mungu aliwakabidhi kwa mke wangu na mimi, ni ‘urithi,’ au zawadi, kutoka kwake. Na alisema kwamba tukiwazoeza katika njia inayofaa, ‘hawataiacha.’ Kwa hiyo sikuzote tumejaribu kuwatunza kana kwamba walikuwa ni mali ya Yehova.”—Zaburi 127:3; Mithali 22:6.

Hapo baba huyo alitambulisha ufunguo wa maisha ya familia yenye mafanikio—wazazi wanapaswa kuwatunza watoto wao kana kwamba walikuwa wanatunza mali ya Mungu. Ingawa hilo halimaanishi kwamba watoto watatii mwelekezo wenu mwema kila mara, mna daraka la kuwatunza watoto ambao Mungu amewapa nyinyi kama amana.

Daraka Zito

Mnaandaa utunzaji huo ifaavyo kwa staha na ufikirio wenye kina, si kwa kutojali au kwa ubaridi. Mnajitahidi katika hilo mking’amua kwamba mtamtolea Mungu hesabu kwa ajili ya urithi, au zawadi yake, kwenu. Si lazima kujaribu-jaribu njia mbalimbali za kuwalea watoto. Wazazi wanahitaji maagizo ya Mungu tu kama yalivyoandaliwa katika Neno lake, Biblia, na wapaswa kuyafuata kwa uangalifu.

Agizo la Yehova Mungu ndilo hilo: “[Ni lazima, New World Translation] uwafundishe watoto wako [maneno yangu] kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo. Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako. Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako.” Biblia huhimiza hivi pia: “Nyinyi, akina baba, . . . endeleeni kuwalea [watoto wenu] katika nidhamu na rekebisho la akilini la Yehova.”—Kumbukumbu la Torati 6:7-9; Waefeso 6:4, NW.

Kwa hiyo kuwalea watoto kwahitaji uangalifu wa kila siku; naam, kwamaanisha kuwapa kwa wingi wakati wako na hasa upendo na ufikirio wako wenye kina. Wazazi wanaowapa watoto wao mahitaji hayo ya msingi wanafanya lile ambalo Mungu husema linahitajika ili kufurahia maisha ya familia yenye mafanikio.

Je! waamini kwamba hiyo ni kudai mengi mno? Wazazi wengi huonyesha kwamba wanahisi hivyo kwa matendo yao. Lakini, zawadi hizo zitokazo kwa Mungu—yaani, watoto wako—zastahili kwelikweli uangalifu zaidi wa pekee.

Namna ya Kuwatunza

Kwa hekima, fikiria kielelezo cha wale ambao wamefanikiwa katika kuwalea watoto. Gazeti moja, katika makala ya kichwa cha jalada “Familia za Ajabu,” lilionyesha mambo manne yaliyo ya maana katika kuwalea wachanga kwa mafanikio: “ Mazungumzo ya wakati wa mlo yanayoamsha akili, kusoma vitabu vizuri, kichocheo cha watu wenye vielelezo vinavyostahili kuigwa walio na uwezo wa kubuni mambo, kujua kwamba kuna utaratibu fulani wa familia upasao kudumishwa.”—U.S.News & World Report, Desemba 12, 1988.

Kuhusu “mazungumzo ya wakati wa mlo,” kumbuka kwamba Mungu huwaagiza wazazi wafundishe watoto wao waketipo nyumbani. Je! familia yako huketi mezani kikawaida nyakati za mlo, hivyo kuandaa fursa za kila siku za ushirika na mazungumzo ya kuamsha akili? Nyakati hizo ni muhimu na zenye kukumbukwa kwa watoto, zikiwapa hisi ya uthabiti na usalama. Mvulana mmoja wa miaka sita alisema kwamba alipenda nyakati za mlo “kwa sababu hamhitaji kuhangaikiana,” kwa kuwa wote wako pamoja.

Namna gani ubora wa mazungumzo yenu ya wakati wa mlo? Je! hayo mara nyingi hukazia yaliyomo katika “vitabu vizuri,” kutia ndani Biblia na fasihi yenye msingi wa Biblia inayozungumzia huduma yetu kwa Mungu au mambo yanayohusiana na vitu vilivyoumbwa na Mungu? Kuongezea mazungumzo ya aina hiyo ya wakati wa mlo, wazazi wanahitaji kusitawisha ndani ya watoto wao kumpenda Yehova na sheria zake zenye uadilifu, kupitia programu ya funzo ya kawaida.

“Kula pamoja kwa kawaida hakukuwa tatizo,” akaeleza yule baba ya watoto sita aliyetajwa mapema. “Lilikuwa jambo la kiasili, na lilisaidia kutuunganisha. Lakini ilikuwa vigumu kuwa na programu ya kawaida ya funzo la Biblia.” Nyakati nyingine alilala usingizi wakati wa funzo, kwa sababu ya kuchoka sana baada ya siku yenye kazi ngumu. Lakini, hakuacha kamwe kuongoza funzo la Biblia la kawaida pamoja na watoto wake, na alizungumza nao mmoja-mmoja kwa kawaida na kuwasikiliza kwa vipindi virefu vya wakati.

Zaidi ya kuongoza katika mazungumzo yenye maana ya wakati wa mlo na kuandaa vitabu vizuri, je, wewe huhakikisha kwamba watoto wako wanapokea “kichocheo cha watu wenye vielelezo vinavyostahili kuigwa walio na uwezo wa kubuni mambo”? Ukweli ni kwamba, kupangia watoto wako ushirika wa kawaida pamoja na wale wanaomwiga yule mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi, Yesu Kristo, ni muhimu ikiwa watakuwa watu wazima wenye mafanikio.

Mwishowe, namna gani kule “kujua kwamba kuna utaratibu fulani wa familia upasao kudumishwa”? Watoto wako wanahitaji kuelewa kwamba kuna viwango vya familia wanavyotazamiwa kudumisha—kwamba kuna mwenendo, usemi, mavazi, tabia, na kadhalika, zisizokubalika na zinazovunja utaratibu wa familia. Wanahitaji kung’amua kwamba kuvunja utaratibu wa familia ni jambo zito—kwamba wewe ungehuzunika sana, kama yule mzee wa ukoo wa kale Yakobo, ambaye wana wake walimfanya ‘anuke vibaya kati ya watu wa nchi hiyo’ kwa mwenendo wao wa aibu.—Mwanzo 34:30.

Yule baba ya watoto sita aliyewaona watoto wake kuwa mali ya Mungu hasa alikazia “utaratibu wa familia.” Alisababu pamoja na watoto wake daima juu ya jinsi kiwango cha familia cha mavazi, kujipamba, na kujitenga na njia za ulimwengu kilivyopatana na roho na mwelekezo wa Muumba, Yehova Mungu. Watoto wote sita waliitikia kwa ‘kutoiacha njia iwapasayo,’ kwa sababu ya ule wakati, upendo, na ufikirio mwingi sana waliotolewa—wakizoezwa katika njia waliyopaswa kwenda.—Mithali 22:6.

Ulimwenguni pote, kuna maelfu ya miungano imara ya familia ya jinsi hiyo. Hiyo humletea Muumba wayo sifa kama nini, nayo ni thawabu kama nini kwa wazazi wenye upendo, wasio na ubinafsi! Miaka ipitapo, wazazi hao wanazidi kuthaminiwa na watoto ambao wamenufaika kutokana na jitihada zao. Sasa tafadhali angalia masimulizi ya mwanamke mmoja aliyelelewa na wazazi wanaomwogopa Mungu, na ona masomo yenye thamani yanayoweza kupatikana kwayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki