Wakristo Wenye Bidii wa Uingereza
Kati ya wale watu milioni 56 wa Uingereza ni asilimia inayopungua 10 ambao ni Wakristo wenye bidii wakati huu, kulingana na The Economist. Katika Jumapili ya kawaida, watu wanaopungua milioni nne huhudhuria mahubiri ya kanisani. Kati ya hao, ni milioni 1.1 tu walio Waanglikana. Hata hiyo, ijapokuwa hali hiyo ya uagnosti [kuamini kwamba ya Mungu hayajulikani], Kanisa la Uingereza laendelea kuwa na daraka lalo thabiti likiwa dini ya Serikali. “Uingereza haijawa jamii ya Kikristo kwa miaka kadhaa lakini yakataa kukubali kuwa na imani ya uagnosti, hasa kwa sababu ya kukumbuka ya zamani,” ladai gazeti lilo hilo la habari. Si ajabu kwamba wanasiasa wa kisasa na magazeti ya habari hutaka Kanisa hilo litengwe na Serikali.
“Ulimwengu ulio wa kimwili kwelikweli, ambao hudai kuwa wa Kikristo, ni ulimwengu ulio mbaya zaidi ya wote,” akaomboleza Walter Bagehot, mhariri wa The Economist wa karne ya 19. Lakini katika karne ya kwanza W.K., Yesu Kristo alisema kwamba wanafunzi wake hawakuwa ‘sehemu ya ulimwengu, kama vile asivyokuwa sehemu ya ulimwengu.’ (Yohana 17:16, NW) Hata hivyo, aliwatuma ulimwenguni ili kuhubiri juu ya Ufalme wa Mungu. Leo vilevile, Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wajulikana vema kwa ajili ya kuhubiri kwa bidii “waziwazi, na nyumba kwa nyumba.”—Matendo 20:20.
Wale Mashahidi 126,173 katika Uingereza ni wachache, kwa kulinganishwa na Waanglikana. Lakini wao hutumia muda wa saa 20 hivi kwa mwezi wakihudhuria mikutano ya Kikristo. Zaidi ya hayo, katika 1992 kila Shahidi alitumia wastani wa muda wa saa 16 zaidi kwa mwezi akijulisha wengine habari njema za Ufalme wa Mungu, ile serikali ambayo hivi karibuni itasimamisha ulimwengu mpya wenye uadilifu. (Mathayo 24:14; 2 Petro 3:13) Mashahidi wa Yehova watembeleapo nyumba yako wakati ujao, je, utasikiliza ujumbe wao ulio tofauti na kupata kujua kile kinachochochea bidii yao?