Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 11/15 uku. 11
  • Wakristo Wenye Bidii wa Uingereza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakristo Wenye Bidii wa Uingereza
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Kanisa la Anglikana Limegawanyika
    Amkeni!—2001
  • Ni Nani Ataeneza Evanjeli Katika Uingereza?
    Amkeni!—1995
  • Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wanahubiri Nyumba kwa Nyumba?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 11/15 uku. 11

Wakristo Wenye Bidii wa Uingereza

Kati ya wale watu milioni 56 wa Uingereza ni asilimia inayopungua 10 ambao ni Wakristo wenye bidii wakati huu, kulingana na The Economist. Katika Jumapili ya kawaida, watu wanaopungua milioni nne huhudhuria mahubiri ya kanisani. Kati ya hao, ni milioni 1.1 tu walio Waanglikana. Hata hiyo, ijapokuwa hali hiyo ya uagnosti [kuamini kwamba ya Mungu hayajulikani], Kanisa la Uingereza laendelea kuwa na daraka lalo thabiti likiwa dini ya Serikali. “Uingereza haijawa jamii ya Kikristo kwa miaka kadhaa lakini yakataa kukubali kuwa na imani ya uagnosti, hasa kwa sababu ya kukumbuka ya zamani,” ladai gazeti lilo hilo la habari. Si ajabu kwamba wanasiasa wa kisasa na magazeti ya habari hutaka Kanisa hilo litengwe na Serikali.

“Ulimwengu ulio wa kimwili kwelikweli, ambao hudai kuwa wa Kikristo, ni ulimwengu ulio mbaya zaidi ya wote,” akaomboleza Walter Bagehot, mhariri wa The Economist wa karne ya 19. Lakini katika karne ya kwanza W.K., Yesu Kristo alisema kwamba wanafunzi wake hawakuwa ‘sehemu ya ulimwengu, kama vile asivyokuwa sehemu ya ulimwengu.’ (Yohana 17:16, NW) Hata hivyo, aliwatuma ulimwenguni ili kuhubiri juu ya Ufalme wa Mungu. Leo vilevile, Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wajulikana vema kwa ajili ya kuhubiri kwa bidii “waziwazi, na nyumba kwa nyumba.”—Matendo 20:20.

Wale Mashahidi 126,173 katika Uingereza ni wachache, kwa kulinganishwa na Waanglikana. Lakini wao hutumia muda wa saa 20 hivi kwa mwezi wakihudhuria mikutano ya Kikristo. Zaidi ya hayo, katika 1992 kila Shahidi alitumia wastani wa muda wa saa 16 zaidi kwa mwezi akijulisha wengine habari njema za Ufalme wa Mungu, ile serikali ambayo hivi karibuni itasimamisha ulimwengu mpya wenye uadilifu. (Mathayo 24:14; 2 Petro 3:13) Mashahidi wa Yehova watembeleapo nyumba yako wakati ujao, je, utasikiliza ujumbe wao ulio tofauti na kupata kujua kile kinachochochea bidii yao?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki